Ezekieli
24 Neno la Yehova likakuja tena kwangu katika mwaka wa kenda (9), katika mwezi wa kumi (10), siku ya kumi ya mwezi huo, na kusema: 2 “Mwana wa binadamu, andika tarehe* hii, siku hii ya leo. Mufalme wa Babiloni ameanza kushambulia Yerusalemu siku hii ya leo.+ 3 Na ueleze mezali* kuhusu nyumba yenye kuasi, na useme kuwahusu:
“‘Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi:
“Tia chungu cha kupikia* juu ya moto; ukitie juu ya moto na umwange maji ndani yake.+
4 Tia vipande vya nyama ndani yake,+ kila kipande kizuri,
Paja na bega; ukijaze kwa mifupa ya muzuri sana.
5 Kamata kondoo wazuri sana wa kundi,+ na urundike kuni chini ya chungu kuzunguka pande zote.
Tokotesha vipande hivyo, na upike mifupa yenye kuwa ndani yake.”’”
6 “Kwa hiyo Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi:
‘Ole wa muji wenye kumwanga damu,+ chungu cha kupikia chenye kutu, chenye kutu yake haijaondolewa!
Tosha nyama ndani yake, kipande kwa kipande;+ usipige kura kwa ajili ya vipande hivyo vya nyama.
7 Kwa maana damu yake iko ndani yake;+ aliimwanga juu ya mwamba wenye kuwa wazi.
Hakuimwanga chini, ili kuifunika kwa mavumbi.+
8 Ili kuchochea kasirani kali kwa ajili ya kulipiza kisasi,
Nimetia damu yake juu ya mwamba wenye kungaa, wenye kuwa wazi
Ili isifunikwe.’+
9 “Kwa hiyo, Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi:
‘Ole wa muji wenye kumwanga damu!+
Nitarundika rundo la murefu la kuni.
10 Rundika kuni na uwashe moto.
Tokotesha nyama kabisa, mwanga muchuzi, na uache mifupa iungue.
11 Weka chungu chenye hakina kitu kwenye makaa ili kikuwe moto
Ili shaba yake ikuwe moto sana.
Uchafu wake utayeyuka ndani yake,+ na kutu yake itateketezwa.
12 Inakatisha tamaa na inachokesha,
Kwa maana kutu yake nyingi haitatoka.+
Ukitupe ndani ya moto pamoja na kutu yake!’
13 “‘Uchafu wako ulitokana na mwenendo wako muchafu.+ Nilijaribu kukusafisha lakini haukukuwa safi kutokana na uchafu wako. Hautakuwa safi mupaka wakati kasirani yangu kali juu yako itatulia.+ 14 Mimi mwenyewe, Yehova, nimesema. Itatendeka. Nitatenda bila kujizuia, bila huruma, bila kusikitika.+ Watakuhukumu kulingana na njia zako na matendo yako,’ ni vile Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema.”
15 Na neno la Yehova likakuja tena kwangu, na kusema: 16 “Mwana wa binadamu, kwa pigo moja niko karibu kumuondoa mupendwa wako kutoka kwako.+ Haupaswe kuomboleza;* wala haupaswe kulia ao kutoa machozi. 17 Lia kwa maumivu kimya-kimya, na usifanye desturi za kuombolezea wafu.+ Ujifunge kilemba chako,+ na uvae viatu vyako.+ Haupaswe kufunika masharubu,*+ na usikule mukate wenye watu wengine walikuletea.”*+
18 Na mimi nikazungumuza na watu asubui, na bibi yangu akakufa mangaribi. Basi asubui nikafanya kama vile nilikuwa nimeamuriwa. 19 Watu walikuwa wananiambia: “Je, hautatuambia namna mambo haya yenye unafanya yanatuhusu?” 20 Nikawajibu: “Neno la Yehova limekuja kwangu, na kusema, 21 ‘Ambia nyumba ya Israeli: “Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi: ‘Niko karibu kuchafua patakatifu pangu,+ chanzo cha majivuno yenu makubwa, kitu chenye munapenda na chenye moyo wenu unatamani.* Watoto wenu wanaume na watoto wenu wanamuke wenye muliacha nyuma wataanguka kwa upanga.+ 22 Halafu mutalazimika kufanya kama vile nimefanya. Hamutafunika masharubu* yenu, na hamutakula mukate wenye watu wengine waliwaletea.+ 23 Vilemba vyenu vitakuwa kwenye vichwa vyenu na viatu vyenu kwenye miguu yenu. Hamutaomboleza wala kulia. Tofauti na hilo, mutaoza katika makosa yenu,+ na ninyi mutalia kwa maumivu kila mutu na mwenzake. 24 Ezekieli amekuwa alama kwenu.+ Mutafanya kama vile amefanya. Wakati jambo hilo litatokea, mutalazimika kujua kwamba mimi ndiye Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova.’”’”
25 “Na sasa wewe, mwana wa binadamu, siku yenye nitaondoa ngome yao kutoka kwao—kitu kizuri cha furaha yao, kitu chenye wanapenda, tamaa ya moyo wao*—pamoja na watoto wao wanaume na watoto wao wanamuke,+ 26 utajulishwa jambo hilo na ule mwenye ameponyoka.+ 27 Siku hiyo utafungua kinywa chako na kuzungumuza na ule mwenye aliponyoka, na hautakuwa bubu tena.+ Utakuwa alama kwao, nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.”