Zaburi
Kwa kiongozi; iimbwe kwa vyombo vya kamba. Maskili.* Ya Daudi.
2 Unisikilize na unijibu.+
Hangaiko langu linanifanya nikose utulivu,+
Na nimevurugika
3 Kwa sababu ya mambo yenye adui anasema
Na mukazo kutoka kwa muovu.
Kwa maana wanarundika taabu juu yangu,
Na kwa kasirani wananiwekea chuki.+
5 Woga na kutetemeka vinakuja juu yangu,
Na kutetemeka kunanishika.
6 Ninaendelea kusema: “Kama tu ningekuwa na mabawa kama njiwa!
Ningeruka mbali na kukaa kwa usalama.
7 Angalia! Ningekimbia na kuenda mbali sana.+
Ningekaa katika jangwa.+ (Sela)
8 Ningeenda haraka mahali pa kujificha
Mbali na upepo mukali, mbali na zoruba.”
10 Usiku na muchana wanazunguka juu ya kuta zake;
Ndani yake kuko nia mubaya na taabu.+
11 Uharibifu uko ndani yake;
Ukandamizaji na udanganyifu haviondoke hata kidogo katika kiwanja chake cha watu wote.+
12 Kwa maana haiko adui ndiye ananichokoza;+
Ingekuwa vile ningevumilia.
Haiko adui ndiye amesimama ili kunishambulia;
Ingekuwa vile ningejificha asinipate.
14 Tulikuwa tunafurahia pamoja urafiki wa karibu sana;
Katika nyumba ya Mungu tulikuwa tunatembea pamoja na kikundi cha watu.
15 Uharibifu uwapate!+
Washuke katika Kaburi* wakiwa wazima;
Kwa maana uovu unakaa kati yao na ndani yao.
16 Lakini mimi, nitamuita Mungu,
Na Yehova ataniokoa.+
17 Mangaribi na asubui na katikati ya muchana, ninahangaika na kulia kwa maumivu,*+
Na anasikia sauti yangu.+
18 Ataniokoa* na kunipatia* amani mbali na wale wenye kupigana na mimi,
Kwa maana vikundi vya watu vinakuja kunishambulia.+
Watakataa kubadilika,
Wale wenye hawajamuogopa Mungu.+
21 Maneno yake ni laini kuliko siagi,+
Lakini muzozo uko katika moyo wake.
Maneno yake ni laini kuliko mafuta,
Lakini ni panga zenye kuchomolewa.+
Hataruhusu hata kidogo mwenye haki aanguke.*+
23 Lakini wewe, Ee Mungu, utawashusha chini kwenye shimo la murefu kabisa.+
Watu hao wenye hatia ya damu wenye ni wadanganyifu hawataishi nusu ya siku zao.+
Lakini mimi, nitakutegemea wewe.