Zaburi
Kwa kiongozi; imepatanishwa na
“Paa Dike wa Mapambazuko.”*
Muziki wa Daudi.
22 Mungu wangu, Mungu wangu, sababu gani umeniacha?+
Sababu gani uko mbali usiweze kuniokoa,
Mbali na vilio vyangu vya uchungu?+
2 Mungu wangu, ninaendelea kuita wakati wa muchana, na wewe haunijibu;+
Na wakati wa usiku sinyamaze.
8 “Alijitia katika mikono ya Yehova. Acha Yeye amukomboe!
Acha Yeye amuokoe, kwa sababu Yeye anamupenda sana!”+
9 Wewe ndiye ulinitosha katika tumbo la uzazi,+
Ni Wewe ulinifanya nijisikie salama kwenye maziwa ya mama yangu.
10 Nimewekwa chini ya utunzaji wako* tangu kuzaliwa kwangu;
Tangu wakati nilikuwa katika tumbo la uzazi la mama yangu, umekuwa Mungu wangu.
12 Ngombe-dume wengi wadogo wananizunguka;+
Ngombe-dume wenye nguvu wa Bashani wananizunguka kwa ajili ya vita.+
13 Wanafungua vinywa vyao wazi juu yangu,+
Kama simba mwenye kunguruma mwenye anapasua mawindo yake vipande-vipande.+
14 Nimemwangwa kama maji;
Mifupa yangu yote imeteguka.
15 Nguvu zangu zimekauka kama kipande cha chombo cha udongo;+
Ulimi wangu unashikamana na fizi* zangu;+
Unanishusha chini kwenye mavumbi ya kifo.+
16 Kwa maana imbwa wananizunguka;+
Wananizunguka kwa ajili ya vita kama kikundi cha watenda maovu,+
Kama vile simba, wako kwenye mikono yangu na miguu yangu.+
17 Ninaweza kuhesabu mifupa yangu yote.+
Wananiangalia na kunikazia macho.
19 Lakini wewe, Ee Yehova, usiendelee kukaa mbali.+
Wewe ni nguvu zangu; kuja haraka unisaidie.+
20 Uniokoe* kutokana na upanga,
Uzima wangu wenye samani* kutokana na muguu wa* imbwa;+
21 Uniokoe kutoka katika kinywa cha simba+ na pembe za ngombe-dume wa pori;
Unijibu na uniokoe.
23 Ninyi wenye kumuogopa Yehova, mumusifu!
Ninyi wote uzao wa* Yakobo, mumutukuze!+
Mumuogope sana, ninyi wote uzao wa* Israeli.
Wakati alimulilia amusaidie, alisikia.+
25 Nitakusifu katika kutaniko kubwa;+
Nitatimiza naziri zangu mbele ya wale wenye kumuogopa.
Mufurahie maisha* milele.
27 Miisho yote ya dunia itakumbuka na kumuendea Yehova.
Familia zote za mataifa zitainama mbele yako.+
28 Kwa maana ufalme ni wa Yehova;+
Anatawala juu ya mataifa.
29 Watu wote wenye kufanikiwa* katika dunia watakula na kumuinamia;
Wale wote wenye kushuka katika mavumbi watapiga magoti mbele yake;
Hakuna mutu yeyote kati yao mwenye anaweza kulinda uzima wao.*
30 Wazao wao watamutumikia;*
Kizazi chenye kitakuja kitaambiwa kuhusu Yehova.
31 Watakuja na kusimulia kuhusu haki yake.
Wataambia watu wenye bado hawajazaliwa mambo yenye amefanya.