Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • Ezekieli 36
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

Habari Zenye Kuwa Katika Ezekieli

      • Unabii kuhusu milima ya Israeli (1-15)

      • Kurudishwa kwa Israeli (16-38)

        • “Nitatakasa jina langu kubwa” (23)

        • “Kama bustani ya Edeni” (35)

Ezekieli 36:2

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yer 49:1; Eze 35:10

Ezekieli 36:3

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “mabaki; wenye walibakia.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kum 28:37; 1 Fal. 9:7; Omb 2:15; Da. 9:16

Ezekieli 36:4

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yer 25:9
  • +Zab 79:4; Eze 34:28

Ezekieli 36:5

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “zarau katika nafsi.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Sef 3:8
  • +Oba 12
  • +Eze 25:12, 13; 35:10, 11; Amo 1:11

Ezekieli 36:6

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Zab 74:10; 123:4

Ezekieli 36:7

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yer 25:9; 49:17

Ezekieli 36:8

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Isa 44:23; 51:3; Eze 36:30

Ezekieli 36:10

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Zek 8:4
  • +Isa 51:3; Yer 30:18, 19; Amo 9:14

Ezekieli 36:11

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yer 31:27
  • +Isa 54:7; Yer 30:18
  • +Hag 2:9
  • +Ho 2:20; Yoe 3:17

Ezekieli 36:12

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yer 32:44; Oba 17
  • +Isa 65:23

Ezekieli 36:15

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Isa 54:4; 60:14; Mik 7:8; Sef 2:8; 3:19

Ezekieli 36:17

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “hezi.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Zab 106:38; Isa 24:5; Yer 2:7; 16:18
  • +Law. 12:2; Isa 64:6

Ezekieli 36:18

Maelezo ya Chini

  • *

    Pengine neno la Kiebrania lenye linatumiwa hapa linahusiana na maneno “mavi ya wanyama” na linatumiwa ili kuonyesha zarau.

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Isa 42:24, 25
  • +Eze 23:37

Ezekieli 36:19

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Law. 26:38; Eze 22:15

Ezekieli 36:20

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Isa 52:5; Rom. 2:24

Ezekieli 36:21

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Zab 74:18; Isa 48:9; Eze 20:9

Ezekieli 36:22

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Zab 106:7, 8

Ezekieli 36:23

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Isa 5:16; Eze 20:41
  • +Zab 102:13-15

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Munara wa Mulinzi (2007 ),

    1/8/2007, uku. 11

    “Kila Andiko,”

    uku. 137

Ezekieli 36:24

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kum 30:3; Isa 43:5; Yer 23:3; Eze 34:13; Ho 1:11

Ezekieli 36:25

Maelezo ya Chini

  • *

    Kunyunyiza ni kumwanga kidogo-kidogo kitu cha majimaji ao ungaunga.

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Hes 19:13; Zab 51:7
  • +Isa 4:4; Yer 33:8
  • +Eze 6:4

Ezekieli 36:26

Maelezo ya Chini

  • *

    Ni kusema, moyo wenye kutii muongozo wa Mungu.

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yer 32:39
  • +Zab 51:10; Eze 11:19, 20
  • +Zek 7:12

Ezekieli 36:27

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yer 31:33

Ezekieli 36:28

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yer 30:22; Eze 37:25, 27

Ezekieli 36:29

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Eze 34:29

Ezekieli 36:30

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Eze 34:27

Ezekieli 36:31

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Ezr 9:6; Ne 9:26; Yer 31:18; Eze 6:9

Ezekieli 36:32

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kum 9:5; Da. 9:19

Ezekieli 36:33

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Zek 8:8
  • +Isa 58:12; Yer 33:10, 11; Amo 9:14

Ezekieli 36:35

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mwa 2:8
  • +Isa 51:3

Ezekieli 36:36

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Eze 28:26; 37:14

Ezekieli 36:38

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao pengine, “Kama vile makundi ya kondoo wa zabihu kule Yerusalemu.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kut 23:17
  • +Yer 30:18, 19

Maandiko ingine

Eze. 36:2Yer 49:1; Eze 35:10
Eze. 36:3Kum 28:37; 1 Fal. 9:7; Omb 2:15; Da. 9:16
Eze. 36:4Yer 25:9
Eze. 36:4Zab 79:4; Eze 34:28
Eze. 36:5Sef 3:8
Eze. 36:5Oba 12
Eze. 36:5Eze 25:12, 13; 35:10, 11; Amo 1:11
Eze. 36:6Zab 74:10; 123:4
Eze. 36:7Yer 25:9; 49:17
Eze. 36:8Isa 44:23; 51:3; Eze 36:30
Eze. 36:10Zek 8:4
Eze. 36:10Isa 51:3; Yer 30:18, 19; Amo 9:14
Eze. 36:11Yer 31:27
Eze. 36:11Isa 54:7; Yer 30:18
Eze. 36:11Hag 2:9
Eze. 36:11Ho 2:20; Yoe 3:17
Eze. 36:12Yer 32:44; Oba 17
Eze. 36:12Isa 65:23
Eze. 36:15Isa 54:4; 60:14; Mik 7:8; Sef 2:8; 3:19
Eze. 36:17Zab 106:38; Isa 24:5; Yer 2:7; 16:18
Eze. 36:17Law. 12:2; Isa 64:6
Eze. 36:18Isa 42:24, 25
Eze. 36:18Eze 23:37
Eze. 36:19Law. 26:38; Eze 22:15
Eze. 36:20Isa 52:5; Rom. 2:24
Eze. 36:21Zab 74:18; Isa 48:9; Eze 20:9
Eze. 36:22Zab 106:7, 8
Eze. 36:23Isa 5:16; Eze 20:41
Eze. 36:23Zab 102:13-15
Eze. 36:24Kum 30:3; Isa 43:5; Yer 23:3; Eze 34:13; Ho 1:11
Eze. 36:25Hes 19:13; Zab 51:7
Eze. 36:25Isa 4:4; Yer 33:8
Eze. 36:25Eze 6:4
Eze. 36:26Yer 32:39
Eze. 36:26Zab 51:10; Eze 11:19, 20
Eze. 36:26Zek 7:12
Eze. 36:27Yer 31:33
Eze. 36:28Yer 30:22; Eze 37:25, 27
Eze. 36:29Eze 34:29
Eze. 36:30Eze 34:27
Eze. 36:31Ezr 9:6; Ne 9:26; Yer 31:18; Eze 6:9
Eze. 36:32Kum 9:5; Da. 9:19
Eze. 36:33Zek 8:8
Eze. 36:33Isa 58:12; Yer 33:10, 11; Amo 9:14
Eze. 36:35Mwa 2:8
Eze. 36:35Isa 51:3
Eze. 36:36Eze 28:26; 37:14
Eze. 36:38Kut 23:17
Eze. 36:38Yer 30:18, 19
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
  • 28
  • 29
  • 30
  • 31
  • 32
  • 33
  • 34
  • 35
  • 36
  • 37
  • 38
Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
Ezekieli 36:1-38

Ezekieli

36 “Sasa wewe, mwana wa binadamu, toa unabii kuhusu milima ya Israeli na useme, ‘Enyi milima ya Israeli, musikie neno la Yehova. 2 Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi: “Adui amesema juu yenu, ‘Aha! Hata mahali pa juu pa zamani pamekuwa mali yetu!’”’+

3 “Kwa hiyo toa unabii na useme, ‘Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi: “Kwa sababu, wamewafanya wakuwe ukiwa na kuwashambulia kutoka kila upande, ili mukuwe mali ya wale wenye waliokoka* kutoka kati ya mataifa na watu wanaendelea kusema kuwahusu na kuwachongea,+ 4 kwa hiyo, Enyi milima ya Israeli, musikie neno la Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova! Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anaambia hivi milima na vilima, mito midogo na mabonde, mabomoko yenye ukiwa,+ na miji yenye iliachwa yenye vitu vyake vimenyanganywa na yenye imechekelewa na wale wenye waliokoka wa mataifa yenye kuwazunguka;+ 5 Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anawaambia hivi: ‘Katika moto wa bidii yangu+ nitasema juu ya wale wenye waliokoka wa mataifa na juu ya Edomu yote, wale wenye kwa kufurahi sana na kwa zarau kamili*+ wamesema kama inchi yangu ni mali yao wenyewe, ili wakamate malisho yake na kuyanyanganya.’”’+

6 “Kwa hiyo toa unabii kuhusu inchi ya Israeli, na uambie milima na vilima, mito midogo na mabonde, ‘Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi: “Angalia! Nitazungumuza katika bidii yangu na katika kasirani yangu kali, kwa sababu mumepatishwa haya na mataifa.”’+

7 “Kwa hiyo Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi: ‘Mimi mwenyewe ninainua mukono wangu ili kuapa kwamba mataifa yenye kuwazunguka yatapata haya yao wenyewe.+ 8 Lakini ninyi, Enyi milima ya Israeli, mutatoa matawi na kuzaa matunda yenu kwa ajili ya watu wangu Israeli,+ kwa maana watarudia hivi karibuni. 9 Kwa maana niko pamoja na ninyi, na nitageuka kuwaelekea, na ninyi mutalimwa na kupandwa mbegu. 10 Nitafanya watu wako waongezeke​—⁠nyumba yote ya Israeli, nyumba yote​—⁠na miji itaikaliwa+ na mabomoko yatajengwa upya.+ 11 Ndiyo, nitafanya watu wenu na mifugo yenu viongezeke;+ wataongezeka na kuzaana. Na nitafanya muikaliwe kama vile muliikaliwa zamani,+ na nitafanya musitawi zaidi kuliko zamani;+ na ninyi mutalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.+ 12 Nitafanya watu​—⁠watu wangu Israeli​—⁠watembee juu yenu, nao watawariti ninyi.+ Mutakuwa uriti wao, na hamutafanya tena wakose watoto hata kidogo.’”+

13 “Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi: ‘Kwa sababu wanawaambia ninyi, “Wewe ni inchi yenye kumeza watu na kufanya mataifa yako yakose watoto,”’ 14 ‘kwa hiyo, hautameza tena watu wala kufanya mataifa yako yakose watoto,’ ni vile Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema. 15 ‘Sitaruhusu tena utukanwe na mataifa wala uchekelewe na watu,+ na hautafanya tena mataifa yako yajikwae,’ ni vile Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema.”

16 Na neno la Yehova likakuja tena kwangu, na kusema: 17 “Mwana wa binadamu, wakati nyumba ya Israeli walikuwa wanaishi katika inchi yao, waliichafua kupitia njia zao na matendo yao.+ Njia zao zilikuwa kwangu kama vile uchafu wa siku za kuona mwezi.*+ 18 Kwa hiyo nilimwanga kasirani yangu kali juu yao kwa sababu ya damu yenye walikuwa wamemwanga juu ya inchi,+ na kwa sababu walichafua inchi kwa sanamu zao zenye kuchukiza.*+ 19 Kwa hiyo niliwasambaza kati ya mataifa na kuwatawanya kati ya inchi mbalimbali.+ Niliwahukumu kulingana na njia yao na kulingana na matendo yao. 20 Lakini wakati walifika katika mataifa hayo, watu walichafua jina langu takatifu+ kwa kusema kuwahusu, ‘Hawa ndio watu wa Yehova, lakini walilazimika kutoka katika inchi yake.’ 21 Kwa hiyo nitahangaikia jina langu takatifu, lenye nyumba ya Israeli ilichafua kati ya mataifa kwenye wameenda.”+

22 “Kwa hiyo ambia nyumba ya Israeli, ‘Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi: “Sitende kwa ajili yenu, Ee nyumba ya Israeli, lakini kwa ajili ya jina langu takatifu, lenye mumechafua kati ya mataifa kwenye mumeenda.”’+ 23 ‘Hakika nitatakasa jina langu kubwa,+ lenye lilichafuliwa kati ya mataifa, lenye mulichafua kati yao; na mataifa yatalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova,’+ ni vile Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema, ‘wakati nitatakaswa kati yenu mbele ya macho yao. 24 Nitawatosha katika mataifa na kuwakusanya kutoka katika inchi zote na kuwaingiza katika inchi yenu.+ 25 Nitanyunyiza* maji safi juu yenu, na ninyi mutakuwa safi;+ na nitawatakasa kutokana na uchafu wenu wote+ na kutokana na sanamu zenu zote zenye kuchukiza.+ 26 Nitawapatia moyo mupya+ na kutia roho mupya ndani yenu.+ Nitaondoa moyo wa jiwe+ katika mwili wenu na kuwapatia moyo wa nyama.* 27 Nitatia roho yangu ndani yenu, na nitawafanya mutembee katika masharti yangu,+ na mutashika na kutenda maamuzi yangu ya hukumu. 28 Kisha mutakaa katika inchi yenye nilipatia mababu zenu, na ninyi mutakuwa watu wangu na mimi nitakuwa Mungu wenu.’+

29 “‘Nitawaokoa kutokana na uchafu wenu wote na kuita nafaka na kuifanya ikuwe nyingi, na sitawaletea njaa.+ 30 Nitafanya matunda ya muti na mazao ya shamba yakuwe mingi, ili musipate tena haya ya njaa kati ya mataifa.+ 31 Kisha mutakumbuka njia zenu zenye uovu na matendo yenu yenye hayakukuwa ya muzuri, na ninyi mutajichukia kwa sababu ya hatia yenu na matendo yenu yenye kuchukiza.+ 32 Lakini mujue jambo hili: Sifanye vile kwa ajili yenu,’+ ni vile Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema. ‘Tofauti na hilo, musikie haya na mufezeheke kwa sababu ya njia zenu, Ee nyumba ya Israeli.’

33 “Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi: ‘Siku yenye nitawatakasa kutokana na hatia yenu yote, nitafanya miji ikaliwe+ na mabomoko yajengwe upya.+ 34 Inchi yenye kuwa ukiwa, yenye ilikuwa imeachwa ukiwa yenye kila mutu mwenye alipita aliiona italimwa. 35 Na watu watasema: “Inchi yenye kuwa ukiwa imekuwa kama bustani ya Edeni,+ na miji yenye ilikuwa mabomoko na yenye ilikuwa ukiwa na yenye ilibomolewa sasa ni mahali kwenye ngome na inaikaliwa na watu.”+ 36 Na mataifa yenye yalibakia kukuzunguka yatalazimika kujua kwamba mimi mwenyewe, Yehova, nimejenga kile chenye kilibomolewa, na nimepanda kile chenye kilikuwa ukiwa. Mimi mwenyewe, Yehova, nimesema, na nimetenda jambo hilo.’+

37 “Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi: ‘Nitaacha pia nyumba ya Israeli waniombe niwafanyie jambo hili: Nitafanya watu wao waongezeke kama kundi. 38 Kama kundi la watakatifu, kama kundi la Yerusalemu* wakati wa sikukuu zake,+ miji yenye ilikuwa mabomoko itajaa makundi ya watu;+ nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.’”

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine