Zaburi
Wimbo. Muziki wa wana wa Kora.+ Kwa kiongozi; kwa mutindo wa Mahalati,* uimbwe kwa kubadilishana. Maskili* ya Hemani+ Mwezra.
88 Ee Yehova, Mungu wa wokovu wangu,+
Wakati wa muchana ninalia kwa sauti,
Na usiku ninakuja mbele yako.+
4 Tayari nimehesabiwa kati ya wale wenye kushuka katika shimo;*+
Nimekuwa mutu mwenye hana uwezo,*+
5 Mwenye ameachwa kati ya wafu
Kama watu wenye waliuawa ambao wanalala katika kaburi,
Wenye haukumbuke tena
Na wenye wametengwa mbali na utunzaji* wako.
6 Umenitia katika shimo lenye kuwa chini sana,
Sehemu zenye giza, katika abiso kubwa.
7 Kasirani yako kali inanilemea sana,+
Na unanilemea kupitia mawimbi yako yenye nguvu. (Sela)
8 Umefukuza wenye kunijua mbali sana na mimi;+
Umenifanya kuwa kitu chenye kuwachukiza.
Nimenaswa na siwezi kuponyoka.
9 Jicho langu limechoka kwa sababu ya mateso yangu.+
Ee Yehova, ninakuitia muchana wote;+
Ninakunyooshea mikono yangu.
10 Je, utatenda mambo ya ajabu kwa ajili ya wafu?
Je, wale wenye hawana uwezo katika kifo wanaweza kusimama ili kukusifu?+ (Sela)
11 Je, upendo wako mushikamanifu utatangazwa katika kaburi,
Uaminifu wako mahali pa uharibifu?*
12 Je, mambo yako ya ajabu yatajulikana katika giza
Ao haki yako katika inchi ya usahaulifu?+
14 Sababu gani, Ee Yehova, unanikataa?*+
Sababu gani unanificha uso wako?+
15 Tangu ujana wangu,
Nimeteseka na niko karibu kuangamia;+
Sihisi chochote kwa sababu ya mambo yenye kuogopesha yenye unaruhusu yanipate.
16 Kasirani yako yenye kuwaka inanilemea;+
Mambo yako yenye kuogopesha sana yananiharibu.
17 Yananizunguka kama maji muchana wote;
Yananizunguka kutoka pande zote.*
18 Umefukuza marafiki wangu na wenzangu mbali sana na mimi;+
Giza limekuwa mwenzangu.