WIMBO WA SULEMANI
1 Wimbo wa nyimbo,* ambao ni wa Sulemani:+
2 “Anibusu kwa busu za kinywa chake,
Kwa maana maonyesho yako ya upendo ni ya muzuri zaidi kuliko divai.+
3 Harufu ya mafuta yako ni yenye kupendeza.+
Jina lako ni kama mafuta yenye harufu ya muzuri yenye yanamwangwa.+
Ndiyo sababu vijana wanamuke wanakupenda.
4 Unishike tuende pamoja;* tukimbie.
Mufalme ameniingiza katika vyumba vyake vya ndani!
Tufurahi na kushangilia katika wewe.
Tusifu* maonyesho yako ya upendo kuliko divai.
Ndio maana wao* wanakupenda.
5 Mimi ni mweusi, lakini mwenye kupendeza, Enyi mabinti wa Yerusalemu,
Kama mahema ya Kedari,+ kama vitambaa vya mahema+ ya Sulemani.
6 Musinishangae kwa sababu mimi ni mweusi,
Kwa sababu jua limeniangalia sana.
Wana wa mama yangu walinikasirikia;
Walinifanya kuwa mulinzi wa mashamba ya mizabibu,
Lakini sikulinda shamba langu mwenyewe la mizabibu.
7 Uniambie, wewe mwenye ninapenda* sana,
Mahali unakulishia kundi lako,+
Mahali unawalalisha katikati ya muchana.
Sababu gani nikuwe kama mwanamuke mwenye amejifunika kitambaa cha kufunika kichwa*
Kati ya makundi ya wenzako?”
8 “Kama haujue, Ee mwanamuke mwenye sura na umbo ya muzuri sana kuliko wanamuke wote,
Uende ukifuata njia za kundi
Na ukulishe mbuzi wako wadogo karibu na mahema ya wachungaji.”
9 “Mupenzi wangu, ninakufananisha na farasi-dike* kati ya magari ya Farao.+
10 Mashavu yako yanapendeza kwa mapambo,*
Shingo yako kwa kamba za shanga.
11 Tutakutengenezea mapambo* ya zahabu
Yenye kupambwa kwa feza.”
12 “Wakati mufalme anakaa kwenye meza yake ya muviringo,
13 Mupenzi wangu ni kama mufuko wa manemane wenye harufu ya muzuri;+
Analala katikati ya maziwa yangu.
15 “Angalia! Uko mwenye sura na umbo ya muzuri, mupenzi wangu.
Angalia! Uko mwenye sura na umbo ya muzuri. Macho yako ni kama ya njiwa.”+
16 “Angalia! Uko mwenye sura na umbo ya muzuri,* mupenzi wangu, na unapendeza sana.+
Kitanda chetu kiko kati ya majani.
17 Nguzo za nyumba yetu* ni miti ya mierezi,
Miti ya sehemu ya juu ya nyumba yetu ni miti ya miberoshi.
3 “Kama muti wa tofaa kati ya miti ya pori,
Ni vile mupenzi wangu iko* kati ya wana.
Ninatamani sana kukaa katika kivuli chake,
Na tunda lake ni tamu katika kinywa changu.
4 Aliniingiza katika nyumba ya karamu,*
Na bendera yake juu yangu ilikuwa upendo.
5 Uniburudishe kwa keki za zabibu;+
Unitegemeze kwa matunda ya matofaa,
Kwa maana ninagonjwa ugonjwa wa mapenzi.
Musijaribu kuamusha ao kuchochea upendo ndani yangu mupaka wakati huo wenyewe utataka.+
8 Sauti ya mupendwa wangu!
Angalia! Anakuja,
Akipanda milima, na kuruka vilima.
9 Mupenzi wangu ni kama swala, kama paa mudogo.+
Yeye ule, amesimama nyuma ya ukuta wetu,
Anachungulia katika madirisha,
Anaangalia kupitia kayungio za madirisha.
10 Mupenzi wangu anasema, ananiambia:
‘Simama, mupenzi wangu,
Muzuri wangu, kuja tuende zetu.
11 Angalia! Kipindi cha baridi* kimepita.
Mvua imeisha na imeenda zake.
12 Maua yametokea katika inchi,+
Wakati wa kukata matawi umefika,+
Na wimbo wa njiwa-tetere umesikiwa katika inchi yetu.+
13 Muti wa tini unakomalisha tini za kwanza-kwanza;+
Mizabibu imetoa maua na inatoa harufu ya muzuri.
Simama, mupenzi wangu, na ukuje.
Muzuri wangu, kuja tuende zetu.
14 Ee njiwa wangu, katika mapango ya miamba,+
Sehemu za ndani kabisa za muteremuko mukali,
Acha nikuone na kusikia sauti yako,+
Kwa maana sauti yako ni yenye kupendeza na sura yako ni yenye kuvutia.’”+
15 “Mutukamatie mbweha,
Mbweha wadogo wenye wanaharibu mashamba ya mizabibu,
Kwa maana mashamba yetu ya mizabibu yametoa maua.”
16 “Mupenzi wangu ni wangu na mimi ni wake.+
Anachunga wanyama+ kati ya maua ya mayungiyungi.+
17 Mupaka wakati upepo mutulivu utavuma* na vivuli kukimbia,
Rudia haraka, Ee mupenzi wangu,
3 “Usiku nikiwa kwenye kitanda changu,
Nilitafuta ule mwenye ninapenda.+
Nilimutafuta, lakini sikumupata.+
2 Nitaamuka na kuzunguka katika muji;
Katika barabara na katika viwanja vya watu wote,
Acha nitafute ule mwenye ninapenda.*
Nilimutafuta, lakini sikumupata.
3 Walinzi wenye walikuwa wanazunguka katika muji walikutana na mimi.+
‘Mumeona ule mwenye ninapenda?’*
4 Kisha tu kuwapita
Nilipata ule mwenye ninapenda.*
Nikamushika, sikupenda kumuacha aende,
Mupaka wakati nilimuingiza katika nyumba ya mama yangu,+
Katika chumba cha ndani cha mwenye alibeba mimba yangu.
5 Ninawaapisha, Enyi mabinti wa Yerusalemu,
Kwa swala na paa wa pori:
Musijaribu kuamusha ao kuchochea upendo ndani yangu mupaka wakati huo wenyewe utataka.”+
6 “Ni kitu gani hiki chenye kupanda kutoka katika jangwa kama nguzo za moshi,
Chenye marashi ya manemane na ubani,
7 “Muangalie! Ni kitanda cha Sulemani.
Wanaume wenye nguvu makumi sita (60) wanakizunguka,
Kutoka kati ya wanaume wenye nguvu wa Israeli,+
8 Kila mumoja wao iko* na upanga,
Wote wamezoezwa kupigana vita,
Kila mumoja iko* na upanga kwenye upande wake
Ili kujilinda na mambo yenye kuogopesha sana ya usiku.”
10 Alitengeneza nguzo zake kwa feza,
Viegemeo vyake kwa zahabu.
Kiti chake ni cha manyoya ya kondoo ya rangi ya zambarau
Sehemu yake ya ndani ilipambwa kwa upendo
Na mabinti wa Yerusalemu.”
11 “Muende inje, Enyi mabinti wa Sayuni,
Mumuone Mufalme Sulemani
Amevaa taji* la arusi lenye mama yake+ alimutengenezea
Siku ya ndoa yake,
Siku yenye moyo wake ulifurahi sana.”
4 “Angalia! Uko mwenye sura na umbo ya muzuri, mupenzi wangu.
Angalia! Uko mwenye sura na umbo ya muzuri.
Macho yako ni kama ya njiwa nyuma ya kitambaa chako cha kufunika kichwa.
Nywele zako ni kama kundi la mbuzi
Wenye wanashuka kwenye milima ya Gileadi.+
2 Meno yako ni kama kundi la kondoo wenye wamekatwa manyoya sasa hivi
Wenye wametoka kunawishwa,
Wote wamezaa mapacha,
Na hakuna mwenye amepoteza kitoto chake.
3 Midomo yako ni kama uzi ya rangi nyekundu yenye kungaa,
Na maneno yako yanapendeza sana.
Kama kipande cha tunda la komamanga
Ni vile mashavu yako yanaonekana nyuma ya kitambaa chako cha kufunika kichwa.
4 Shingo yako+ ni kama munara wa Daudi,+
Wenye ulijengwa kwa mistari ya majiwe
Ngao elfu (1 000) zimetundikwa juu yake,
Ngao zote za muviringo za wanaume wenye nguvu.+
5 Maziwa yako mbili ni kama paa wawili wadogo,
Mapacha wa paa,+
Wenye wanakulia majani kati ya maua ya mayungiyungi.”
6 “Mupaka wakati upepo mutulivu utavuma* na vivuli kukimbia,
Nitaenda zangu kwenye mulima wa manemane
Na kwenye kilima cha ubani.”+
8 Unifuate kutoka Lebanoni, bibi-arusi wangu,
Unifuate kutoka Lebanoni.+
Shuka kutoka kwenye kichwa cha Amana,*
Kutoka kwenye kichwa cha Seniri, kutoka kwenye kichwa cha Hermoni,+
Kutoka katika mashimo ya simba, kutoka kwenye milima ya chui.
9 Umebeba moyo wangu,+ dada yangu, bibi-arusi wangu,
Umebeba moyo wangu kwa kuniangalia mara moja tu,
Kwa kidani kimoja cha mukufu wako.
10 Maonyesho yako ya upendo ni ya muzuri sana,+ dada yangu, bibi-arusi wangu!
Maonyesho yako ya upendo ni ya muzuri zaidi kuliko divai,+
Na marashi yako yananuka muzuri kuliko manukato yoyote!+
11 Midomo yako, bibi-arusi wangu, inaangusha matone-matone ya asali ya sega.+
Asali na maziwa viko chini ya ulimi wako,+
Na harufu ya muzuri ya nguo zako ni kama harufu ya muzuri ya Lebanoni.
12 Dada yangu, bibi-arusi wangu, ni kama bustani yenye kufungwa,
Bustani yenye kufungwa, chemchemi yenye kufungwa kwa muhuri.
13 Machipukizi* yako ni paradiso* ya matunda ya makomamanga
Yenye matunda ya muzuri sana, yenye mimea ya hina pamoja na mimea ya nardo,
14 Nardo+ na zafarani, kane*+ na mudalasini,+
Na miti yote ya ubani, manemane, na udi,+
Pamoja na manukato yote ya muzuri sana.+
15 Wewe ni chemchemi ya bustani, kisima cha maji safi,
Na mito midogo yenye kutiririka kutoka Lebanoni.+
16 Amuka, Ee upepo wa kaskazini;
Ingia, Ee upepo wa kusini.
Vuma* juu ya bustani yangu.
Acha manukato ya bustani hiyo yasambae.”
“Acha mupenzi wangu akuje kwenye bustani yake
Na akule matunda ya muzuri sana ya bustani hiyo.”
5 “Nimeingia katika bustani yangu,+
Ee dada yangu, bibi-arusi wangu.
Nimechuma manemane pamoja na manukato yangu.+
Nimekula sega la asali na asali yangu;
Nimekunywa divai yangu na maziwa yangu.”+
“Mukule, marafiki wangu!
Mukunywe na mulewe maonyesho ya upendo!”+
2 “Nimelala, lakini moyo wangu uko macho.+
Kuko sauti ya mupenzi wangu akipiga hodi!
‘Unifungulie, Ee dada yangu, mupenzi wangu,
Njiwa wangu, wangu mwenye hana kasoro!
Kwa maana kichwa changu kimelowana umande,
Mashungi ya nywele zangu yamejaa umajimaji wa usiku.’+
3 Nimetosha kanzu yangu.
Niivae tena?
Nimenawisha miguu yangu.
Niichafue tena?
4 Mupenzi wangu aliondoa mukono wake kwenye tundu la mulango,
Na hisia zangu kumuelekea zikaamushwa.
5 Nilisimama ili nimufungulie mupenzi wangu;
Mikono yangu ikaangusha matone-matone ya manemane,
Na vidole vyangu manemane ya maji,
Ikaangukia kwenye mikono ya kifungio cha mulango.
6 Nilimufungulia mupenzi wangu,
Lakini mupenzi wangu alikuwa amegeuka, alikuwa ameenda zake.
Nilivunjika moyo* wakati alienda.*
Nilimutafuta, lakini sikumupata.+
Nikamuita, lakini hakunijibu.
7 Walinzi wenye walikuwa wanazunguka katika muji walinipata.
Wakanipiga, wakaniumiza.
Walinzi wa kuta wakaninyanganya kitambaa changu kikubwa.*
8 Ninawaapisha, Enyi mabinti wa Yerusalemu:
Kama munamupata mupenzi wangu,
Mumuambie kwamba ninagonjwa ugonjwa wa mapenzi.”
9 “Mupenzi wako anashindia wapenzi wengine wote na nini,
Wewe mwenye sura na umbo ya muzuri sana kuliko wanamuke wote?
Mupenzi wako anashindia wapenzi wengine wote na nini,
Ili utuapishe vile?”
10 “Mupenzi wangu anangaa na ni mwekundu;
Anavutia zaidi kati ya wanaume elfu kumi (10 000).
11 Kichwa chake ni zahabu, zahabu safi sana.
Mashungi ya nywele zake ni kama majani ya muti wa mutende yenye kutikisika.*
Ni meusi kama kunguru.
12 Macho yake ni kama njiwa pembeni ya mito midogo ya maji,
Wananawa miili yao ndani ya maziwa,
Wamekaa pembeni ya kiziwa cha maji chenye kujaa sana.*
13 Mashavu yake ni kama bustani ya manukato,+
Vilima vya mimea yenye harufu ya muzuri.
Midomo yake ni maua ya mayungiyungi, yanaangusha matone-matone ya manemane ya maji.+
14 Mikono yake ni viviringo vya zahabu, vyenye kupambwa na krisolito.
Tumbo lake ni pembe ya tembo yenye kungarishwa na kupambwa na yakuti.
15 Miguu yake ni nguzo za marumaru zenye kuwekwa kwenye vikalio vya zahabu safi.
Sura yake ni kama Lebanoni, ni ya muzuri sana kama miti ya mierezi.+
Huyo ndiye mupenzi wangu, huyo ndiye mupendwa wangu, Enyi mabinti wa Yerusalemu.”
6 “Mupenzi wako ameenda wapi,
Ee mwenye sura na umbo ya muzuri sana kuliko wanamuke wote?
Mupenzi wako amefuata njia gani?
Acha tumutafute pamoja.”
2 “Mupenzi wangu ameenda kwenye bustani yake,
Kwenye bustani yenye mimea yenye kutoa harufu ya muzuri,
Ili kuchunga kondoo kati ya mabustani
Na kuchuma maua ya mayungiyungi.+
3 Mimi ni wa mupenzi wangu,
Na mupenzi wangu ni wangu.+
Anachunga wanyama kati ya maua ya mayungiyungi.”+
4 “Uko mwenye sura na umbo ya muzuri kama Tirza,*+ mupendwa wangu,+
Unapendeza kama Yerusalemu,+
Unashangaza kama majeshi yenye kukusanyika kuzunguka bendera zao.+
Nywele zako ziko kama kundi la mbuzi
Wenye kushuka kwenye milima ya Gileadi.+
6 Meno yako ni kama kundi la kondoo
Wenye wametoka kunawishwa,
Wote wamezaa mapacha,
Na hakuna mwenye amepoteza kitoto chake.
7 Kama kipande cha tunda la komamanga
Ni vile mashavu yako yanaonekana nyuma ya kitambaa chako cha kufunika kichwa.
8 Kunaweza kuwa malkia makumi sita (60)
Na masuria* makumi munane (80)
Na vijana wanamuke wenye hawana hesabu,+
9 Lakini mumoja tu ndiye njiwa wangu,+ wangu mwenye hana kasoro.
Mutoto wa pekee wa mama yake.
Anapendwa sana na* ule mwenye alimuzaa.
Mabinti wanamuona, na wanamutangaza kuwa mwenye furaha;
Malkia na masuria,* na wanamusifu.
10 ‘Ni mwanamuke gani mwenye kungaa* kama mapambazuko,*
Mwenye sura na umbo ya muzuri kama mwezi wenye kuenea,
Mwenye kutakata kama mwangaza wa jua,
Mwenye kushangaza kama majeshi yenye kukusanyika kuzunguka bendera zao?’”+
11 “Nilishuka kwenye bustani ya miti ya lozi+
Ili nione machipukizi katika bonde,*
Ili nione kama muzabibu umechipuka*
Kama miti ya mikomamanga imetoa maua.
13 “Rudia, rudia, Ee Mushulami!
Rudia, rudia,
Ili tukuone!”
“Sababu gani munamuangalia Mushulami?”+
“Yeye ni kama dansi ya vikundi mbili!”*
7 “Miguu yako inapendeza sana katika viatu vyako,
Ee binti mwenye cheo!
Mikunjo ya mapaja yako ni kama mapambo,
Kazi ya mikono ya fundi.
2 Kitofu chako ni bakuli la muviringo.
Lisikose hata kidogo divai yenye kuchanganywa.
Tumbo lako ni rundo la ngano,
Lenye kuzungukwa na maua ya mayungiyungi.
3 Maziwa yako mbili ni kama paa wadogo wawili,
Mapacha wa paa.+
4 Shingo yako+ ni kama munara wa pembe ya tembo.+
Pua yako ni kama munara wa Lebanoni,
Wenye unaelekea Damasko.
5 Kichwa chako kinakuvalisha taji kama Karmeli,+
Na mashungi ya nywele zako*+ ni kama manyoya ya kondoo ya rangi ya zambarau.+
Mufalme amevutiwa* na nywele zako zenye kulembelea.
6 Wewe ni mwenye sura na umbo ya muzuri sana, na unapendeza sana,
Ee kijana mwanamuke mupendwa, unapita vitu vyote vyenye kupendeza!
8 Nilisema: ‘Nitapanda juu ya muti wa mutende
Ili nishike vitawi vyake vya matunda.’
Maziwa yako yakuwe kama vishada vya mizabibu,
Pumuzi yako ikuwe na harufu ya muzuri kama matunda ya matofaa,
9 Na kinywa chako* kama divai ya muzuri sana.”
“Acha itiririke polepole kwa ajili ya mupenzi wangu,
Itiririke kwa vyepesi juu ya midomo ya wale wenye kulala usingizi.
10 Mimi ni wa mupenzi wangu,+
Naye ananitamani.
12 Tuamuke asubui sana na kuenda kwenye mashamba ya mizabibu
Ili tuone kama muzabibu umechipuka,*
Kama maua yamefunguka,+
Kama miti ya mikomamanga imetoa maua.+
Kule nitakuonyesha upendo wangu.+
13 Matunda ya dudai+ yanatoa harufu yake ya muzuri,
Kwenye milango yetu kuko kila namna ya matunda ya muzuri sana.+
Ya mupya na ya zamani vilevile,
Ee mupenzi wangu, nimekuwekea.
8 “Ikiwa tu ungekuwa kama ndugu yangu,
Mwenye alinyonya maziwa ya mama yangu!
Basi kama ningekukuta inje, ningekubusu.+
Na hakuna mwenye angenizarau.
Ningekupatia divai yenye kutiwa manukato ili ukunywe,
Maji safi ya matunda ya makomamanga.
3 Mukono wake wa kushoto ungekuwa chini ya kichwa changu,
Na mukono wake wa kuume ungenikumbatia.+
4 “Ninawaapisha, Enyi mabinti wa Yerusalemu:
Musijaribu kuamusha ao kuchochea upendo ndani yangu mupaka wakati huo wenyewe utataka.”+
5 “Ni nani huyu mwenye anapanda kutoka katika jangwa,
Akiwa ameegemea mupenzi wake?”
“Chini ya muti wa mutofaa nilikuamusha.
Kule, mama yako alikuwa katika uchungu wa kukuzaa.
Kule, mwenye alikuzaa alikuwa katika uchungu wa kuzaa.
6 Unitie kama muhuri juu ya moyo wako,
Kama muhuri juu ya mukono wako,
Kwa maana upendo uko na nguvu kama kifo,+
Na tamaa ya mutu ya kutaka washikamane na yeye tu ni yenye kudai kama Kaburi.*
Miali yake ni moto wenye kuwaka sana, mwali wa moto wa Yah.*+
Kama mutu angetoa mali yote ya nyumba yake kwa ajili ya upendo,
Ingezarauliwa* kabisa.”
8 “Tuko na dada mudogo,+
Na hana maziwa.
Tutamufanyia nini dada yetu
Siku yenye watamuomba?”
9 “Kama yeye ni ukuta,
Tutajenga juu yake munara wa feza,
Lakini kama yeye ni mulango,
Tutamuzuia kwa mbao ya muti wa mwerezi.”
10 “Mimi ni ukuta,
Na maziwa yangu ni kama minara.
Basi mbele ya macho yake nimekuwa
Kama mutu mwenye anapata amani.
11 Sulemani alikuwa na shamba la mizabibu+ kule Baal-hamoni.
Alipatia watunzaji shamba hilo la mizabibu.
Kila mumoja wao alikuwa analeta vipande elfu moja (1 000) vya feza kwa ajili ya matunda yake.
12 Niko na shamba langu mwenyewe la mizabibu.
Vile vipande elfu moja (1 000) vya feza ni vyako, Ee Sulemani,
Na vipande mia mbili (200) ni vya wale wenye wanatunza matunda yake.”
13 “Ee wewe mwenye kukaa katika mabustani,+
Marafiki wanasikiliza sauti yako.
Acha niisikie.”+
14 “Fanya haraka, mupenzi wangu,
Na ukimbie mbio kama swala+
Kama paa mudogo
Juu ya milima ya manukato.”
Ao “Wimbo wa muzuri kuliko nyimbo zote.”
Tnn., “Unikokote.”
Ao “Tusimulie.”
Ni kusema, vijana wanamuke.
Ao “mwenye nafsi yangu inapenda.”
Ao “kitambaa cha kufunika kichwa wakati wa maombolezo.”
Ao “farasi-dike wangu.”
Ao pengine, “kati ya nywele zenye kusukwa.”
Ao “mapambo ya muviringo.”
Tnn., “Nardo.”
Ao “murembo.”
Ao “nyumba yetu kubwa.”
Ao “eko.”
Ao “eko.”
Tnn., “nyumba ya divai.”
Ao “kipindi cha mvua.”
Tnn., “siku itapumua.”
Ao pengine, “milima yenye mipasuko.” Ao “milima ya Beteri.”
Ao “mwenye nafsi yangu inapenda.”
Ao “mwenye nafsi yangu inapenda.”
Ao “mwenye nafsi yangu inapenda.”
Ao “poda.”
Ao “eko.”
Ao “eko.”
Kitanda chenye kufunikwa ambacho kilitumiwa kubebea mutu wa maana.
Ao “taji la maua.”
Tnn., “wakati siku itapumua.”
Ao “Anti-Lebanoni.”
Ao pengine, “Ngozi.”
Ao “bustani.”
Kane ni utete wenye harufu ya muzuri.
Ao “Vuma polepole.”
Ao “Nafsi yangu ilizimia.”
Ao pengine, “nafsi yangu ilinitoka wakati alisema.”
Ao “kitambaa cha kufunika kichwa.”
Ao pengine, “vishada vya tende.”
Ao pengine, pembeni ya chemchemi.
Tnn., “Kaakaa lake.” Kaakaa ni sehemu ya juu ndani ya kinywa.
Ao “Muji Wenye Kupendeza.”
Angalia Maana ya Maneno.
Tnn., “Yeye ndiye mwenye kuwa safi wa.”
Angalia Maana ya Maneno.
Tnn., “kuangalia chini.”
Mapambazuko ni wakati mwangaza wa asubui unaanza kutokea.
Ao “bonde la muto.”
Ao “umetokeza matumba.”
Ao “Nafsi.”
Ao “watu wangu wenye kujipendea.”
Ao “dansi ya Mahanaimu.”
Tnn., “kichwa chako.”
Ao “amenaswa.”
Tnn., “kaakaa lako.” Kaakaa ni sehemu ya juu ndani ya kinywa.
Ao “umetokeza matumba.”
Ao “Sheoli,” ni kusema, kaburi la wanadamu wote. Angalia Maana ya Maneno.
“Yah” ni kifupi cha jina Yehova.
Ao pengine, “Angezarauliwa.”