Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • hf sehemu 8 uku. 26-28
  • Wakati Musiba Unatokea

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Wakati Musiba Unatokea
  • Familia Yenu Inaweza Kuwa na Furaha
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • 1 MUMUTEGEMEE YEHOVA
  • 2 UJITUNZE WEWE NA FAMILIA YAKO
  • 3 TAFUTA MUSAADA
  • Maulizo ya Wasomaji Wetu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2017
  • Yehova Iko Naona Magumu Yetu na Iko Tayari Kutusaidia
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2022
  • Ninapenda Kufa​—Biblia Inaweza Kunisaidia Wakati Niko na Mawazo ya Kujiua?
    Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
  • Sala— Inaweza Kukuletea Faida Gani?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
Ona Habari Zaidi
Familia Yenu Inaweza Kuwa na Furaha
hf sehemu 8 uku. 26-28
Bibi na bwana wanahuzunika sababu mutoto wao anawaacha

SOMO LA 8

Wakati Musiba Unatokea

‘Munashangilia sana katika jambo hilo, ingawa kwa muda kidogo sasa, ikiwa ni lazima, mumehuzunishwa na majaribu ya namna mbalimbali.’​—1 Petro 1:6

Hata ikiwa unafanya yako yote ili kuwa na ndoa na familia yenye furaha, mambo ambayo hautazamie yanaweza kutokea na kufanya iwe vigumu kulinda furaha yako. (Mhubiri 9:11) Kwa upendo, Mungu anatusaidia wakati tunapambana na matatizo. Kutumikisha kanuni za Biblia kutakusaidia wewe na familia yako mupambane hata na matatizo makali sana.

1 MUMUTEGEMEE YEHOVA

MAMBO AMBAYO BIBLIA INASEMA: ‘Mutupe mahangaiko yenu yote juu yake, kwa sababu yeye anawajali ninyi.’ (1 Petro 5:7) Sikuzote mukumbuke kwamba si Mungu ambaye analeta majaribu. (Yakobo 1:13) Kadiri munaendelea kumukaribia, atawasaidia. (Isaya 41:10) ‘Mumimine mioyo yenu mbele zake.’​—Zaburi 62:8.

Mutapata pia faraja wakati mutasoma na kujifunza Biblia kila siku. Mwishowe, mutatambua namna Yehova ‘anatufariji katika ziki yetu yote.’ (2 Wakorintho 1:3, 4; Waroma 15:4) Anaahidi kuwapatia “amani ya Mungu yenye ubora unaozidi fikira zote.”​—Wafilipi 4:6, 7, 13.

Baba kwenye kitanda cha hospitali anasali pamoja na familia yake

MAMBO YA KUFANYA:

  • Mumuombe Yehova awasaidie kubaki watulivu na kuwa na maoni yanayofaa juu ya misiba

  • Mufikirie mambo yote munayoweza kufanya na mufanye uamuzi muzuri zaidi

2 UJITUNZE WEWE NA FAMILIA YAKO

MAMBO AMBAYO BIBLIA INASEMA: ‘Moyo wa mutu mwenye uelewaji unajipatia ujuzi, nalo sikio la wenye hekima linatafuta kupata ujuzi.’ (Methali 18:15) Tafuta kujua habari zote juu ya familia yako. Jua mahitaji ya kila mushiriki wa familia. Zungumuza nao. Wasikilize.​—Methali 20:5.

Unaweza kufanya nini ikiwa mutu ambaye unapenda anakufa? Usijizuie kuonyesha huzuni yako. Kumbuka kwamba hata Yesu ‘alitokwa na machozi.’ (Yohana 11:35; Mhubiri 3:4) Ni lazima pia kupumuzika na kulala vya kutosha. (Mhubiri 4:6) Kufanya hivyo kutakusaidia upambane na hali yenye kuhuzunisha.

MAMBO YA KUFANYA:

  • Uzoee kuzungumuza na familia yako mbele hata ya musiba kutokea. Wakati matatizo yanatokea, hawataogopa kuongea na wewe

  • Zungumuza na wengine ambao wamekwisha kupambana na hali kama hiyo

3 TAFUTA MUSAADA

MAMBO AMBAYO BIBLIA INASEMA: “Rafiki wa kweli anapenda nyakati zote, naye ni ndugu aliyezaliwa kwa ajili ya wakati wa taabu.” (Methali 17:17) Rafiki zako wanataka kukusaidia, lakini pengine hawajue namna gani wanaweza kukusaidia. Usijizuie kuwaambia mambo ambayo unahitaji kabisa. (Methali 12:25) Tena, tafuta musaada wa kiroho kwa watu ambao wanaelewa Biblia. Muongozo wa Biblia ambao watakutolea utakusaidia.​—Yakobo 5:14.

Utapata musaada ambao unahitaji ikiwa unapitisha wakati kwa ukawaida na watu ambao wanamuamini kabisa Mungu na ambao wanatumainia ahadi zake. Tena, utafarijiwa sana wakati utawasaidia wale wanaohitaji kutiwa moyo. Zungumuza nao juu ya imani yako katika Yehova na katika ahadi zake. Endelea kuwa na mengi ya kufanya katika kuwasaidia wale walio katika uhitaji, na usijitenge na watu ambao wanakupenda na kukuhangaikia.​—Methali 18:1; 1 Wakorintho 15:58.

MAMBO YA KUFANYA:

  • Muelezee rafiki wako wa karibu matatizo yako na ukubali musaada wake

  • Ueleze waziwazi mahitaji yako na useme kweli

UWE NA MAONI YANAYOFAA

Hata ikiwa unajisikia mwenye kushuka moyo, endelea kumufikiria Yehova. Wakati alikuwa katika majaribu, Ayubu alisema hivi: “Jina la Yehova na liendelee kubarikiwa.” (Ayubu 1:21, 22) Kama Ayubu, hangaikia kwanza jina la Yehova na mapenzi yake mbele ya kuhangaikia matatizo yako. Usivunjike moyo wakati mambo yanakuwa namna haukutazamia. Mutumainie Mungu kwa moyo wote. Yehova anatuambia hivi: ‘Mimi ninajua vema mawazo ninayofikiria kuwaelekea ninyi, mawazo ya amani, wala si ya musiba, ili kuwapa ninyi wakati ujao na tumaini.’​—Yeremia 29:11.

JIULIZE . . .

  • Je, ninamutumainia kabisa Yehova hata katika mambo madogo-madogo?

  • Nina sababu gani za kumushukuru Yehova kila siku kwa sababu ya wema wake?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2026)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine