Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • hf sehemu 9 uku. 29-31
  • Mumuabudu Yehova Katika Familia

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Mumuabudu Yehova Katika Familia
  • Familia Yenu Inaweza Kuwa na Furaha
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • 1 MUKOMALISHE URAFIKI WENU NA YEHOVA
  • 2 MUFURAHIE IBADA YENU YA FAMILIA
  • Msaada kwa Familia
    Huduma Yetu ya Ufalme—2011
  • Ibada ya Familia Ni Nini?
    Ni Nani Wanafanya Mapenzi ya Yehova Leo?
  • Ibada ya Familia—Namna Gani Unaweza Kuifanya Ifurahishe Zaidi?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Ibada ya Kweli Itaongeza Furaha Yako
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2022
Ona Habari Zaidi
Familia Yenu Inaweza Kuwa na Furaha
hf sehemu 9 uku. 29-31
Bibi na bwana wanajifunza Biblia pamoja

SOMO LA 9

Mumuabudu Yehova Katika Familia

‘Mumuabudu yeye aliyezifanya mbingu na dunia.’​—Ufunuo 14:7

Umejifunza katika broshua hii kwamba Biblia ina kanuni nyingi ambazo zitakusaidia wewe na familia yako. Yehova anataka muwe na furaha. Anaahidi kwamba ikiwa munatia ibada yake pa nafasi ya kwanza, ‘mutaongezewa hivi vitu vingine vyote.’ (Mathayo 6:33) Kwa kweli, anataka muwe rafiki zake. Mufaidike na kila nafasi inayojitokeza ili kukomalisha urafiki wenu naye. Hilo ndilo pendeleo kubwa zaidi ambalo mutu anaweza kuwa nalo.​—Mathayo 22:37, 38.

1 MUKOMALISHE URAFIKI WENU NA YEHOVA

Bibi na bwana wanahubiri pamoja

MAMBO AMBAYO BIBLIA INASEMA: Yehova anatuambia hivi: ‘Nitakuwa baba kwenu, nanyi mutakuwa wana na mabinti kwangu.’ (2 Wakorintho 6:18) Mungu anataka muwe rafiki zake wa karibu. Sala ni njia moja ya kumukaribia. Yehova anatuomba ‘tusali bila kuacha.’ (1 Wathesalonike 5:17) Iko tayari kukusiliza unapomuelezea mawazo yako ya ndani na mahangaiko yako. (Wafilipi 4:6) Wakati unasali pamoja na familia yako, wataona ni kwa kadiri gani Mungu iko halisi kwako.

Zaidi ya kuzungumuza na Mungu katika sala, ni lazima kumusikiliza. Unaweza kumusikiliza kwa kujifunza Neno lake Biblia na vichapo vinavyotegemea Biblia. (Zaburi 1:1, 2) Tafakari juu ya mambo ambayo unajifunza. (Zaburi 77:11, 12) Tena, ili kumusikiliza Mungu, ni lazima kuhuzuria mikutano kwa ukawaida.​—Zaburi 122:1-4.

Kuwaelezea wengine kuhusu Yehova ni njia nyingine ya maana ya kufanya urafiki wetu naye ukomae. Kadiri tunawaelezea wengine kumuhusu, ndivyo tunamukaribia zaidi.​—Mathayo 28:19, 20.

MAMBO YA KUFANYA:

  • Panga wakati wa kujifunza Biblia na kusali kila siku

  • Mukiwa familia, muhangaikie kwanza mambo ya kiroho kuliko mambo ya kujifurahisa

2 MUFURAHIE IBADA YENU YA FAMILIA

Baba anajitayarisha ili kuongoza funzo la familia na kisha wanafanya ibada ya familia

MAMBO AMBAYO BIBLIA INASEMA: ‘Mumukaribie Mungu, naye atawakaribia ninyi.’ (Yakobo 4:8) Ni vizuri kupanga programu ya ibada ya familia ya kila juma na kuifanya kwa ukawaida. (Mwanzo 18:19) Lakini hiyo haitoshe. Ni lazima mumupatie Mungu nafasi katika maisha yenu ya kila siku. Mukomalishe uhusiano wenu na Yehova kwa kuzungumuza kumuhusu ‘munapoketi katika nyumba yenu na munapotembea barabarani na munapolala na munapoamuka.’ (Kumbukumbu la Torati 6:6, 7) Muazimie kumuiga Yoshua, ambaye alisema hivi: ‘Lakini mimi na nyumba yangu, tutamutumikia Yehova.’​—Yoshua 24:15.

MAMBO YA KUFANYA:

  • Muwe na ibada ya familia inayofanywa kwa ukawaida na ambayo inafikiria mahitaji ya kila mushiriki wa familia

Mama anamusomea mutoto wake; familia inafanya muchezo wa Biblia; Baba anajifunza na mutoto wake mwanamuke

WATUMISHI WA YEHOVA WENYE FURAHA

Hakuna jambo nzuri zaidi kuliko kumuabudu Yehova Mungu. Anafurahi anapokuona na familia yako mukimutumikia kwa moyo wote. Kwa kufanya hivyo, mutamupenda na kumuiga Yehova zaidi na zaidi. (Marko 12:30; Waefeso 5:1) Kumupatia Mungu nafasi katika ndoa yenu kunafanya vifungo vya ndoa yenu viwe nguvu. (Mhubiri 4:12; Isaya 48:17) Wewe na familia yako munaweza kuwa na furaha milele mukijua kwamba ‘Yehova Mungu wenu amewabariki.’​—Kumbukumbu la Torati 12:7.

JIULIZE . . .

  • Ni wakati gani tulisali tukiwa familia kwa mara ya mwisho?

  • Ni mambo gani ninaweza kujifunza na familia yangu ambayo yatatia nguvu imani yetu katika Yehova?

KWA BABA YA FAMILIA

  • Usiruhusu jambo fulani lizuie ibada yenu ya familia

  • Acha kila mushiriki wa familia ajue mbele ya wakati mambo ambayo mutazungumuzia kwenye ibada ili ajitayarishe

  • Hakikisha kwamba kila mushiriki wa familia iko kwenye ibada ya familia

  • Ongoza ibada katika hali yenye utulivu ambayo wote watafurahia

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2026)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine