Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • od sura 16 uku. 162-168
  • Familia ya Ndugu na Dada Yenye Umoja

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Familia ya Ndugu na Dada Yenye Umoja
  • Tengenezo Yenye Kufanya Mapenzi ya Yehova
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • KUBADILISHA NAMNA YA KUWAZA
  • TULINDE UMOJA WETU MU DUNIA YOTE
  • TUHANGAIKIANE
  • MUNGU ALITUCHAGUA ILI TUFANYE MAPENZI YAKE
  • Umoja wa Kweli Kati ya Wakristo—Jinsi Gani?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2003
  • ‘Tupende Ushirika Muzima wa Akina Ndugu’
    Huduma Yetu ya Ufalme—2013
  • “Mungu Hana Ubaguzi”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” juu ya Ufalme wa Mungu
  • ‘Tunda la Roho’ Linamtukuza Mungu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
Tengenezo Yenye Kufanya Mapenzi ya Yehova
od sura 16 uku. 162-168

SURA YA 16

Familia ya Ndugu na Dada Yenye Umoja

KWA kipindi ya miaka 1 500 hivi, Yehova Mungu alihangaikia Waisraeli; walikuwa taifa kwa ajili ya jina yake. Kisha, Yehova “alielekeza uangalifu wake kwa mataifa ili achukue kati yao watu kwa ajili ya jina lake.” (Mdo. 15:14) Wale watu kwa ajili ya jina ya Yehova, ni mashahidi wake; wako na umoja mu mawazo na matendo fasi yote kwenye wanaishi. Kazi yenye Yesu alipatia wanafunzi wake njo yenye inafanya kukuwe wale watu wenye kuitwa kwa jina ya Yehova na wenye kuwa na umoja. Yesu alisema hivi: “Kwa hiyo, muende, na mufanye wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote, na muwabatize katika jina la Baba na la Mwana na la roho takatifu, na muwafundishe kushika mambo yote yenye nimewaamuru ninyi. Na muangalie! niko pamoja na ninyi sikuzote mupaka umalizio wa mupangilio wa mambo.”​—Mt. 28:19, 20.

Uko sasa mu familia ya ndugu na dada, ni kusema Wakristo wenye kuishi kwa umoja mu dunia yote. Ikuwe wengine ni matajiri ao maskini, ni wa taifa ao kabila ingine, ile mambo haifanye tugawanyike

2 Wakati ulijitoa kwa Yehova na kubatizwa, ulionyesha wazi kama uko mwanafunzi wa Yesu Kristo. Uko sasa mu familia ya ndugu na dada, ni kusema Wakristo wenye kuishi kwa umoja mu dunia yote. Ikuwe wengine ni matajiri ao maskini, ni wa taifa ao kabila ingine, ile mambo haifanye tugawanyike. (Zb. 133:1) Njo maana mu kutaniko, tunapendana na kuheshimiana. Pengine zamani haungewakubali wengine kati yao juu ya rangi yao ya ngozi, taifa yao ao juu hawakusoma sawa vile weye. Lakini sasa siye wote tuko mu familia ya ndugu na dada yenye kuunganishwa na upendo wenye kuwa nguvu sana. Mu hii dunia, hakuna kabila, dini ao familia yenye inaunganishwa sawa vile siye.​—Mk. 10:29, 30; Kol. 3:14; 1 Pe. 1:22.

KUBADILISHA NAMNA YA KUWAZA

3 Kama watu fulani wangali na ubaguzi wa rangi ya ngozi, ya kabila, ubaguzi mu mambo ya politike, ao tabia ingine, ni muzuri wafikirie Wakristo Wayahudi wa wakati wa mitume. Wale Wakristo waliachana kabisa na mafundisho ya dini yao ya Kiyahudi yenye iliwafanya wakuwe na ubaguzi na kuwazia mubaya watu wa mataifa ingine. Yehova alimutayarisha kwa upendo mutume Petro ili atimize muzuri mugawo wa kuenda kwa Kornelio, mukubwa wa kikundi fulani ya maaskari wa Roma.​—Matendo, sura ya 10.

4 Mu maono, mutume Petro aliambiwa achinje na kula wanyama fulani, wenye hawakukuwa safi kulingana na sheria ya Wayahudi. Wakati ule mutume alikatala, alisikia sauti kutoka mbinguni inamuambia: “Acha kuita vitu vyenye Mungu ametakasa kuwa ni vichafu.” (Mdo. 10:15) Iliomba Mungu amusaidie mutume Petro ili abadilishe mawazo yake juu atimize mugawo wenye angemupatia, ni kusema, kutembelea mutu wa mataifa. Mutume Petro alitii muongozo wa Yehova, na aliambia hivi watu wenye walikuwa mu nyumba ya Kornelio: “Munajua muzuri kwamba Muyahudi haruhusiwe kushirikiana ao kukaribia mutu wa jamii ingine, lakini Mungu amenionyesha kwamba sipaswe kuita mutu yeyote kuwa muchafu ao haiko safi. Basi nilikuja, kwa kweli bila kupinga, wakati watu walitumwa waniite.” (Mdo. 10:28, 29) Kwa hiyo, mutume Petro alijionea mambo ya kuhakikisha kama Yehova alikubali Kornelio na watu wa nyumba yake.

5 Sauli wa Tarso, alikuwa Mufarisayo na alisoma masomo ya juu. Hata vile, alijishusha ili kujiunga na watu wenye hangeitikaka kujiunga nao zamani. Aliitika hata kuongozwa na wale watu. (Mdo. 4:13; Gal. 1:13-20; Flp. 3:4-11) Fikiria watu, sawa vile Sergio Paulo, Dionisio, Damari, Filemoni, Onesimo na wengine, wenye walibadilisha mawazo yao kisha kukubali habari njema na kuwa wanafunzi wa Yesu Kristo.​—Mdo. 13:6-12; 17:22, 33, 34; Flm. 8-20.

TULINDE UMOJA WETU MU DUNIA YOTE

6 Kusema kweli, upendo wa ndugu na dada mu kutaniko, unaendelea pia kukusaidia umukaribie Yehova na tengenezo yake. Ulishajionea alama ya upendo wa pekee yenye kutambulisha wanafunzi wa kweli wa Yesu Kristo, sawa vile yeye mwenyewe alisema: “Ninawapatia ninyi amri mupya, kwamba mupendane; kama vile nimewapenda ninyi, ninyi pia mupendane vilevile. Kwa jambo hili wote watajua kama ninyi ni wanafunzi wangu​—kama muko na upendo kati yenu.” (Yoh. 13:34, 35) Ulifikia kutambua kama upendo wenye uko mu kutaniko ni sehemu kidogo tu ya upendo wenye kuwa kati ya ndugu na dada wenye kuwa mu dunia yote. Na ile ilifanya umupende hata zaidi Yehova na tengenezo yake. Uko najionea kutimizwa kwa unabii wenye kuwa mu Biblia kuhusu kukusanya watu mu siku za mwisho ili wamuabudu Yehova kwa amani na umoja.​—Mik. 4:1-5.

7 Vile kuko mambo mingi yenye kufanya watu mu dunia wagawanyike, ni nani angeamini kama inawezekana kuunganisha watu “kutoka mataifa yote na makabila na vikundi vya watu na luga”? (Ufu. 7:9) Fikiria tofauti yenye kuwa kati ya watu wenye kutumia teknolojia ya sasa na wale wenye kufuata desturi za zamani za makabila yao. Pia, fikiria namna makanisa iko nagawanya watu wa rangi moya ya ngozi ao watu wa taifa ao inchi moya. Juu watu wanapenda sana inchi zao, politike inaendelea kugawanya sana watu kuliko zamani. Tena, kama unapima kufikiria tofauti yenye kuwa kati ya matajiri na maskini na mambo ingine yenye kufanya watu wajigawanye, utaona kama kuunganisha watu wenye kutoka mu mataifa yote, vikundi na hali mbalimbali katika upendo wenye nguvu na amani, ni muujiza wenye Mungu tu Mweza-Yote njo anaweza kufanya.​—Zek. 4:6.

8 Ile umoja ni jambo ya kweli kabisa, na weye uliingia mu familia yenye iko na ile umoja wakati ulijitoa kwa Mungu na ukabatizwa ili kuwa Shahidi wa Yehova. Juu ile umoja iko nakuletea pia faida, uko na daraka ya kusaidia kulinda umoja yenyewe. Unaweza kufanya vile kwa kufuata hii maneno ya mutume Paulo yenye kuwa mu Wagalatia 6:10: “Wakati tungali na nafasi, tutendee watu wote mambo ya muzuri, lakini zaidi sana wale wenye kuwa wa jamaa yetu katika imani.” Pia, ingine shauri yenye tunatii ni hii: “Musifanye jambo lolote kwa ugomvi ao kwa kutafuta sifa, lakini kwa unyenyekevu muone wengine kuwa wazuri zaidi kuliko ninyi mukiendelea kuangalia, hapana faida zenu ninyi wenyewe tu, lakini pia faida za wengine.” (Flp. 2:3, 4) Kadiri tunaendelea kujikaza ili kuona ndugu na dada zetu vile Yehova anawaona, hapana vile wanaoneka kwa inje, tutaendelea kuwa na urafiki wenye amani na furaha pamoya nao.​—Efe. 4:23, 24.

TUHANGAIKIANE

9 Sawa vile mufano yenye mutume Paulo alitumia inaonyesha, kutaniko haigawanyike, lakini ndugu na dada wanahangaikiana. (1 Ko. 12:14-26). Inawezekana tuishi mbali na Wakristo wenzetu, lakini ile haimaanishe kama hatutahangaikia hali yao. Kama ndugu na dada zetu wanaanza kuteswa mu inchi fulani, siye wote tunahuzunikaka sana. Ikiwa Wakristo fulani wanakosa vitu vya lazima ao wanateseka kwa sababu ya misiba, vita, ao mapigano ya kikabila, Wakristo wenzao wanajikaza sana ili kuwasaidia kimwili na kiroho.​—2 Ko. 1:8-11.

10 Siye wote tuko na daraka ya kusali kwa ajili ya Wakristo wenzetu kila siku. Kati yetu, kuko wale wenye kujaribiwa kufanya mambo ya mubaya. Wamoya wako napata mateso yenye wengine hawajue. Na wengine wako napata upinzani wenye haujulikane muzuri sana kutoka kwa wafanyakazi wenzao ao kutoka mu familia yenye kugawanyika. (Mt. 10:35, 36; 1 Te. 2:14) Ile mambo yote inatuhuzunishaka sana juu tuko mu familia moya ya ndugu na dada mu dunia yote. (1 Pe. 5:9) Zaidi ya ile, kati yetu kuko wale wenye kutumika sana mu kazi ya Yehova, na wengine wenye kusimamia makutaniko na kazi ya kuhubiri. Tena kuko wale wenye kuwa na daraka ya kusimamia kazi ya kuhubiri mu dunia yote. Tunaweza kuonyesha kama tunawapenda na kuwahangaikia kabisa kwa kusali kwa ajili yao. Tutafanya vile hata kama pengine hatuna jambo ingine ya kufanya ili kuwasaidia.​—Efe. 1:16; 1 Te. 1:2, 3; 5:25.

11 Juu kuko mivurugo mingi mu hizi siku za mwisho, watumishi wa Yehova wanapaswa kuwa tayari kusaidiana. Wakati kunatokea misiba fulani, sawa vile, matetemeko ya inchi, mvua kubwa ao misiba ingine, inaomba kukusanya na kutuma vitu mingi vya kimwili ili kusaidia ndugu na dada. Wakristo wa wakati wa mitume walituachia mufano ya muzuri sana juu ya ile jambo. Wakati walikumbuka shauri ya Yesu, wanafunzi wenye walikuwa Antiokia, walitumia kwa furaha ndugu wa Yudea misaada ya kimwili. (Mdo. 11:27-30; 20:35) Kisha, mutume Paulo alitia moyo Wakorinto wategemeze mipango yenye ilikamatwa kwa utararibu ili kusaidia wale Wakristo. (2 Ko. 9:1-15) Leo pia, wakati ndugu na dada wanafikiwa na hali fulani yenye inafanya ikuwe lazima kuwasaidia kimwili, tengenezo na kila Mukristo anajikaza kuwategemeza haraka kwa kuwapatia mambo yenye wako nayo lazima.

MUNGU ALITUCHAGUA ILI TUFANYE MAPENZI YAKE

12 Familia yetu ya ndugu na dada mu dunia yote, ni tengenezo yenye kufanya mapenzi ya Yehova. Leo, mapenzi ya Yehova ni kwamba habari njema ya Ufalme ihubiriwe mu dunia yote yenye kuikaliwa ili kuwa ushahidi kwa mataifa yote. (Mt. 24:14) Wakati tunaendelea kufanya hii kazi, Yehova anapenda pia tukuwe na mwenendo wenye kupatana na kanuni zake. (1 Pe. 1:14-16) Kila Mukristo anapaswa kuwa tayari kujishusha mbele ya mwingine na kufanya nguvu ili kazi ya kuhubiri habari njema iende mbele. (Efe. 5:21) Kwa hiyo, hii njo wakati ya kutia Ufalme wa Mungu pa nafasi ya kwanza mu maisha yetu, kuliko kutafuta faida zetu. (Mt. 6:33) Kama tunaweka ile mu akili na kuendelea kufanya mambo kwa ajili ya habari njema, tutakuwa kabisa wenye furaha sasa, na kisha tutapata baraka za milele.

13 Siye Mashahidi wa Yehova tuko watu wa pekee, watu wenye kuchaguliwa, tuko safi, na wenye bidii mu kazi ya Yehova Mungu. (Tit. 2:14) Ni ibada yenye tunamutolea Yehova njo inatufanya tukuwe tofauti na wengine. Tunatumika kwa umoja pamoya na ndugu na dada mu dunia yote; zaidi ya ile, tuko nazungumuza luga moya ya ile kweli na kujikaza kuishi kulingana na kweli yenye tuko nahubiri. Inapatana kabisa na unabii yenye Yehova alitoa kupitia nabii wake Sefania: “Kwa maana wakati huo nitabadilisha luga ya vikundi vya watu kuwa luga safi, Ili wote waitie jina la Yehova, wamutumikie bega kwa bega.”​—Sef. 3:9.

14 Kisha, Yehova aliongoza nabii Sefania aandike hivi juu ya umoja yenye iko naonekana leo kati ya ndugu na dada mu dunia: “Watu wa Israeli wenye watabakia hawatatenda ukosefu wowote wa haki; hawatasema uongo, wala ulimi wa udanganyifu hautakuwa katika vinywa vyao; watakula na kulala, na hakuna mutu mwenye atawaogopesha.” (Sef. 3:13) Tuko natumika kwa umoja juu tulishaelewa kabisa kweli ya Neno ya Yehova, tulishafanya upya akili zetu, na tuko naishi kulingana na kanuni za Yehova. Mambo yenye haiwezekane kwa nguvu ya mwanadamu njo yenye tuko nafanya. Bila shaka, tuko watu wa Mungu wenye kuwa tofauti kabisa na watu wengine, na tunaheshimia Yehova mu dunia yote.​—Mik. 2:12.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine