Mwezi wa 11
Siku ya Posho, 1 Mwezi wa 11
Kutoka katika kinywa cha watoto wadogo na watoto wenye kunyonya umetokeza sifa.—Mt. 21:16.
Kama uko muzazi, usaidie watoto wako watayarishe maelezo yenye kufaa kulingana na miaka yao. Wakati fulani, mambo mazito sawa vile magumu ya ndoa ao namna ya kuwa na mwenendo safi inazungumuziwaka wakati ya funzo. Hata vile, kunaweza kuwa fungu moya ao mbili kwenye mutoto anaweza kutoa maelezo. Tena, usaidie watoto wako waelewe juu ya nini kiongozi hatawataya kila mara wakati wananyangula mikono. Kufanya vile, kunaweza kuwasaidia wasikasirike wakati kiongozi anataya wengine. (1 Ti. 6:18) Siye wote tunaweza kutayarisha maelezo yenye itamutukuza Yehova na yenye itajenga Wakristo wenzetu. (Mez. 25:11) Kama tunazungumuzia jambo yenye inatuhusu, tunapaswa kuepuka kusema mambo mingi juu yetu. ( Mez. 27:2; 2 Ko. 10:18) Kuliko kufanya vile, tutakaza akili juu ya Yehova, Neno yake, na watu wake.—Ufu. 4:11. w23.04 24-25 fu. 17-18
Siku ya Yenga, 2 Mwezi wa 11
Tusiendelee kulala usingizi kama wengine, lakini tukae macho na kulinda akili zetu.—1 Te. 5:6.
Upendo ni wa maana ili tukuwe macho na kulinda akili zetu. (Mt. 22:37-39) Kumupenda Mungu kunatusaidia tuhubiri kwa uvumilivu hata kama ile inaweza kufanya tupate magumu. (2 Ti. 1:7, 8) Tunaendelea kuhubiri kwa kutumia telefone na hata barua juu tunapenda pia wale wenye hawamutumikie Yehova. Tunatumainia kama siku moya majirani wetu watabadilika na kuanza kufanya mambo ya muzuri. (Eze. 18:27, 28) Tunapenda pia ndugu na dada zetu. Tunaonyesha ule upendo kwa “kutiana moyo na kujengana.” (1 Te. 5:11) Sawa vile maaskari wenye hawaachanake mu vita, siye pia tunatianaka moyo. Hatuwezi kukwaza ndugu na dada zetu kwa kupenda ao kurudisha ubaya kwa ubaya. (1 Te. 5:13, 15) Tunaonyesha pia kama tuko na upendo kwa kuheshimia ndugu wenye wanasimamia kutaniko.—1 Te. 5:12. w23.06 10 fu. 6; 11 fu. 10-11
Siku ya Kwanza, 3 Mwezi wa 11
Wakati [Yehova] anasema jambo fulani, je, hatalifanya?—Hes. 23:19.
Jambo moya yenye inaweza kufanya imani yetu ikuwe nguvu ni kutafakari juu ya bei ya ukombozi. Bei ya ukombozi inatuhakikishia kama ahadi za Mungu zitatimia. Wakati tunafikiria kwa uangalifu sababu yenye ilifanya Yehova atoe bei ya ukombozi na mambo yenye ile iliomba, tutaamini kabisa kama atatimiza ahadi ya kutupatia uzima wa milele mu dunia mupya. Juu ya nini tunasema vile? Bei ya ukombozi iliomba nini? Yehova alituma Mwana wake muzaliwa-pekee, mwenye alipenda sana na mwenye alikuwa rafiki yake wa karibu sana, ili azaliwe hapa ku dunia akiwa mwanadamu mukamilifu. Wakati Yesu alikuwa hapa ku dunia, alivumilia magumu ya kila aina. Kisha, aliteseka na kufa kifo ya maumivu. Yehova alilipa bei kubwa sana! Mungu wetu mwenye upendo hangeacha Mwana wake ateseke na kufa juu tu tukuwe na maisha ya muzuri kwa wakati mufupi sana. (Yoh. 3:16; 1 Pe. 1:18, 19) Juu Yehova alilipa bei kubwa vile, ile inaonyesha kama atatupatia uzima wa milele mu dunia mupya. w23.04 27 fu. 8-9
Siku ya Pili, 4 Mwezi wa 11
Ee Kifo, uko wapi uwezo wako wa kuumiza?—Ho. 13:14.
Yehova anapenda kabisa kufufua wafu? Bila shaka anapenda. Alipatia waandikaji wengi wa Biblia roho yake takatifu ili waandike ahadi yake ya kufufua wafu wakati yenye kuya. (Isa. 26:19; Ufu. 20:11-13) Kila mara, Yehova anatimizaka ahadi zote zenye anatoaka. (Yos. 23:14) Kusema kweli, anapenda kabisa kufufua wafu. Fikiria maneno yenye Yobu alisema. Alikuwa hakika kuwa hata kama anakufa Yehova angetamani kumufufua. (Yob. 14:14, 15, maelezo ya chini.) Yehova hayabadilika. Anatamani kufufua waabudu wake wenye walishakufa. Anapenda sana kuwafufua na kuwapatia afya ya muzuri na maisha yenye furaha. Tuseme nini juu ya mamiliare ya watu wenye hawakupata nafasi ya kujifunza kweli juu ya Yehova mbele wakufe? Yehova Mungu wetu wa upendo anapenda kuwafufua pia. (Mdo. 24:15) Anapenda kuwapatia nafasi ya kuwa marafiki wake na kuishi milele ku dunia.—Yoh. 3:16. w23.04 9 fu. 5-6
Siku ya Tatu, 5 Mwezi wa 11
Kwa musaada wa Mungu tutapata nguvu.—Zb. 108:13.
Namna gani unaweza kutia nguvu tumaini yako? Kwa mufano, kama uko na tumaini ya kuishi milele ku dunia, usome na utafakari maandiko ya Biblia yenye kufasiria namna Paradiso itakuwa. (Isa. 25:8; 32:16-18) Fikiria namna maisha itakuwa mu dunia mupya. Ujiwazie uko pale. Kama tunaendelea kukazia akili tumaini ya dunia mupya yenye tuko nayo, magumu yetu itakuwa “ya wakati kidogo na ya nyepesi.” (2 Ko. 4:17) Yehova atakutia nguvu kupitia tumaini yenye amekupatia. Amekupatia mambo yenye uko nayo lazima ili upate nguvu kutoka kwake, kwa hiyo wakati uko na lazima ya musaada ili kutimiza mugao fulani, kuvumilia magumu, ao kuendelea kuwa na furaha, usali kwa Yehova kwa moyo wote na utafute muongozo wake kupitia funzo ya kipekee. Ukubali vitia moyo vyenye ndugu na dada wanakutolea. Tafakari juu ya tumaini yako ya wakati wenye kuya. Kisha “utafanywa kuwa imara kwa nguvu zote kulingana na uwezo [wa Mungu] wenye utukufu ili uvumilie kwa ukamili kwa subira na furaha.”—Kol. 1: 11. w23.10 17 fu. 19-20
Siku ya Ine, 6 Mwezi wa 11
Mushukuru kwa kila jambo.—1 Te. 5:18.
Tuko na sababu mingi za kumushukuru Yehova mu sala. Tunaweza kumushukuru juu ya jambo yoyote ya muzuri yenye tuko nayo. Zaidi ya ile, zawadi yote ya muzuri inatokaka kwake. (Yak. 1:17) Kwa mufano, tunaweza kumushukuru juu ya dunia na juu ya vitu vya muzuri vyenye aliumba. Tunaweza pia kumushukuru juu ya uzima wetu, familia yetu, marafiki wetu, na tumaini yetu. Na tunapenda pia kumushukuru Yehova juu anaturuhusu tukuwe marafiki wake. Inaweza kuwa muzuri kujikaza sana ili kufikiria sababu zenye zinatufanya siye kipekee tumushukuru Yehova. Tunaishi mu dunia yenye watu wengi hawakuwake na shukrani. Mara mingi watu wanahangaikia mambo yenye wanapenda kuliko kuhangaikia mambo yenye wanaweza kufanya ili kuonyesha shukrani juu ya mambo yenye wako nayo. Kama na siye tunaanza kuwa vile, tutakuwa nasali Yehova juu tu ya kumuomba mambo fulani. Juu ya kuepuka ile, tunapaswa kuendelea kumushukuru Yehova juu ya mambo yote yenye anatufanyiaka.—Lu. 6:45. w23.05 4 fu. 8-9
Siku ya Tano, 7 Mwezi wa 11
[Endelea] kuomba kwa imani, bila kuwa na mashaka hata kidogo.—Yak. 1:6.
Juu Yehova ni Baba yetu mwenye upendo, hafurahi wakati anatuona tuko nateseka. (Isa. 63:9) Hata vile, haiko mateso yote njo Yehova anazuiaka isitupate, mateso yenye inaweza kulinganishwa na mito ao moto. (Isa. 43:2) Lakini, anatuahidi kama atatusaidia “kupita” mu ile mateso. Na hataruhusu ile mateso iharibu uhusiano wetu pamoya naye. Yehova anatupatia pia roho yake takatifu yenye nguvu ili kutusaidia kuvumilia. (Lu. 11:13; Flp. 4:13) Kwa hiyo, tunaweza kuwa hakika kama sikuzote tutakuwa na yote yenye tuko nayo lazima ili tuendelee kuvumilia na kuendelea kuwa waaminifu kwa Yehova. Yehova anatazamia tumutumainie. (Ebr. 11:6) Wakati fulani tunaweza kuona kama magumu yetu ni ya nguvu sana, yenye hatuwezi kuvumilia. Tunaweza kuanza kujiuliza ikiwa Yehova atatusaidia kabisa. Lakini Biblia inatuhakikishia kama kupitia nguvu ya Mungu tunaweza “kupanda ukuta.” (Zb. 18:29) Kwa hiyo, kuliko kuwa na mashaka tunapaswa kusali kwa imani kabisa na kuwa hakika kabisa kama Yehova atajibia sala zetu.—Yak. 1:6, 7. w23.11 22 fu. 8-9
Siku ya Posho, 8 Mwezi wa 11
Miali ya [upendo] ni moto wenye kuwaka sana, mwali wa moto wa Yah. Maji mengi hayawezi kuzima upendo, wala mito haiwezi kuufagilia mbali.—Wim. 8:6, 7.
Ile ni mafasirio ya muzuri sana ya upendo wa kweli! Na inahakikishia bibi na bwana kama wanaweza kuonyeshana upendo wa kweli. Inaomba kujikaza sana juu bibi na bwana wapendane maisha yao yote. Kwa mufano, moto unaweza kuendelea kuwaka kama mutu anaongeza kuni; kama hafanye vile, unaweza kuzimika. Vilevile, upendo kati ya bibi na bwana unaweza kuendelea kuwa nguvu maisha yao yote kama tu wako nafanya uhusiano wao ukuwe nguvu. Wakati fulani, bibi na bwana wanaweza kuona kama upendo wao uko napunguka, zaidi sana wakati wako na magumu ya kupata makuta, magumu ya afya, ao magumu ya kukomalisha watoto. Juu “mwali wa moto wa Yah” usizimike, bibi na bwana wanapaswa kuwa na uhusiano wa nguvu pamoya na Yehova. w23.05 20-21 fu. 1-3
Siku ya Yenga, 9 Mwezi wa 11
Usiogope.—Da. 10:19.
Juu tuonyeshe uhodari, tunapaswa kufanya nini? Wazazi wetu wanaweza kutuambia tukuwe na uhodari, lakini hata kama wako na uhodari, ile haimaanishe kama na siye tutakuwa tu na ile sifa. Kuwa na uhodari ni sawa vile kujifunza jambo fulani ya mupya. Jambo moya yenye inaweza kusaidia mutu akuwe na ufundi kuhusu jambo yenye iko najifunza ni kuangalia kwa uangalifu mambo yenye mwalimu wake iko nafanya na kumuiga. Vilevile, tutakuwa na uhodari, kama tunaangalia kwa uangalifu namna wengine wako naonyesha ile sifa na kuwaiga. Sawa vile Daniel, tunapaswa kujua muzuri Neno ya Mungu. Tunapaswa kufanya urafiki wa karibu sana pamoya na Yehova kwa kuongea naye kila mara na kumuambia vile tuko najisikia kabisa. Na tunapaswa kumutumainia kwa kuwa hakika kama ataendelea kutusaidia. Kama tunafanya vile, wakati imani yetu itajaribiwa tutaonyesha uhodari. Mara mingi watu wanaheshimiaka mutu mwenye kuwa na uhodari. Mutu mwenye uhodari anaweza pia kusaidia wengine wamujue Yehova. Bila shaka ni jambo ya maana kuonyesha uhodari. w23.08 2 fu. 2; 4 fu. 8-9
Siku ya Kwanza, 10 Mwezi wa 11
Muchunguze mambo yote.—1 Te. 5:21.
Neno ya Kigiriki yenye inatafsiriwa “muchunguze” ilikuwa natumiwa ili kuonyesha namna watu walikuwa napima metali sawa vile zahabu na feza ili kujua kama zilikuwa za kweli. Kwa hiyo, siye pia tunapaswa kujaribu ao kuchunguza maneno yenye tunasikia ao mambo yenye tunasoma ili kuona kama ni ya kweli ao hapana. Ile itaendelea kuwa ya maana zaidi sana kwetu kadiri taabu kubwa iko nakaribia. Kuliko kuamini kila jambo yenye watu wanasema, tunatumia uwezo wetu wa kufikiri ili kulinganisha mambo yenye tunasoma ao yenye tunasikia na mambo yenye Biblia na tengenezo ya Yehova inasema. Kama tunafanya vile, hatutapotoshwa na habari yoyote ya uongo yenye kuongozwa na pepo muchafu. (Mez. 14:15; 1 Ti. 4:1) Tunajua kama watumishi wa Mungu wataokoka taabu kubwa. Lakini, hakuna mwenye anajua mambo ya kesho. (Yak. 4:14) Hata vile, ikuwe tutakuwa tungali wazima wakati wa taabu kubwa ao kama tutakufa mbele ianze, tutapata zawabu ya uzima wa milele kama tunaendelea kuwa waaminifu. Tuendelee basi kukaza akili yetu juu ya tumaini yetu ya muzuri na tuendelee kuwa tayari kwa ajili ya siku ya Yehova! w23.06 13 fu. 15-16
Siku ya Pili, 11 Mwezi wa 11
[Anafunulia] watumishi wake manabii jambo lake la siri.—Amo. 3:7.
Hatujue namna maunabii fulani yenye kuwa mu Biblia itatimia. (Da. 12: 8, 9) Lakini, kushindwa kuelewa kabisa namna unabii fulani utatimia, haimaanishe kama ule unabii hautatimia. Bila shaka, tunaweza kuwa hakika kama kwa wakati wenye kufaa kabisa Yehova atatusaidia kuelewa mambo yenye tunapaswa kujua, sawa vile alifanyaka zamani. Mataifa itafanya tangazo ya “amani na usalama.” (1 Te. 5:3) Kisha, serikali za ulimwengu zitashambulia dini ya uongo na kuiharibu. (Ufu. 17:16, 17) Na kisha watashambulia watu wa Mungu. (Eze. 38:18, 19) Ile matukio itaongoza moja kwa moja ku vita ya mwisho ya Armagedoni. (Ufu. 16:14, 16) Tuko hakika kama ile mambo itatokea hivi karibuni. Mbele itokee, tuendelee basi kumushukuru Baba yetu wa mbinguni mwenye upendo kwa kuchunguza kwa uangalifu maunabii yenye kuwa mu Biblia na kwa kusaidia wengine wafanye pia vile. w23.08 13 fu. 19-20
Siku ya Tatu, 12 Mwezi wa 11
Tuendelee kupendana, kwa sababu upendo unatoka kwa Mungu.—1 Yo. 4:7.
Wakatimutume Paulo alikuwa nazungumuzia imani, tumaini, na upendo, alimazia kwa kusema hivi: “Jambo la mukubwa zaidi kati ya mambo hayo [ao zile sifa] ni upendo.” (1 Ko. 13:13) Juu ya nini Paulo alisema vile? Wakati wenye kuya hatutakuwa na lazima ya kuwa na imani katika ahadi za Mungu kuhusu ulimwengu mupya ao kuwa na tumaini kama zile ahadi zitatimia, kwa sababu zitakuwa zilishatimia. Lakini tutaendelea kuwa na lazima ya kumupenda Yehova na kuendelea kupenda watu. Na hata upendo wetu kwao utaendelea kuongezeka milele. Pia, sababu moya ni kwamba upendo unatutambulisha kuwa Wakristo wa kweli. Yesu aliambia hivi mitume wake: “Kwa jambo hili wote watajua kama ninyi ni wanafunzi wangu—kama muko na upendo kati yenu.” (Yoh. 13:35) Zaidi ya ile, upendo unatusaidia tuendelee kuwa na umoja. Paulo alisema kama upendo “ni kifungo kikamilifu cha umoja.” (Kol. 3:14) Mutume Yohana aliandikia hivi waamini wenzake: “Yeyote mwenye anamupenda Mungu anapaswa pia kumupenda ndugu yake.” (1 Yo. 4:21) Wakati tunaonyeshana upendo, tunaonyesha kama tunamupenda Mungu. w23.11 8 fu. 1, 3
Siku ya Ine, 13 Mwezi wa 11
Tutupe kila uzito na zambi.—Ebr. 12:1.
Biblia inalinganisha maisha ya Mukristo na mbio. Wakimbiaji wenye watafika mupaka mwisho watapata uzima wa milele. (2 Ti. 4:7, 8) Njo maana, tunapaswa kujikaza sana ili kuendelea kukimbia zaidi sana juu mwisho wa ile mbio unakuwa karibu sana. Mutume Paulo alitaya mambo yenye itatusaidia kupata ushindi mu ile mbio. Alituambia “tutupe . . . kila uzito na . . . tukimbie kwa uvumilivu shindano la mbio lenye limewekwa mbele yetu Paulo alipenda kusema kama hakuna muzigo wenye Mukristo anapaswa kubeba? Hapana hakupenda kusema vile.” Lakini, alipenda kusema kama tunapaswa kutupa muzigo wowote wenye hauko wa lazima. Muzigo wa vile unaweza kutuchokesha na kufanya tusikimbie mbio sana. Ili kuvumilia, tunapaswa kutambua haraka muzigo wowote wenye hauko wa lazima wenye unaweza kutufanya tukimbie polepole na tunapaswa kuutupa. Lakini, wakati uleule hatupaswe kutupa mizigo yenye kwa kawaida tunapaswa kubeba. Juu kama tunaitupa, hatutastahili tena kuendelea mu ile mbio.—2 Ti. 2:5. w23.08 26 fu. 1-2
Siku ya Tano, 14 Mwezi wa 11
Kujipamba kwenu kusikuwe kwa inje.—1 Pe. 3:3.
Kuwa na usawaziko kunatusaidia kuheshimia mawazo ya wengine. Kwa mufano, dada fulani wanapendaka kujipodoa, lakini wengine hawapendake. Wakristo fulani wanapendaka kunywa pombe kwa kiasi, lakini wengine hawakunywake hata kidogo. Wakristo wote wanapendaka kuwa na afya ya muzuri, lakini wanahangaikiaka afya yao mu njia tofauti. Ikiwa tunawaza kama siye tu njo tunakuwaka na sheria na ikiwa tunapendaka ndugu na dada waanze kufanya mambo sawa vile siye, tunaweza kuwakwaza na kuleta migawanyiko mu kutaniko. (1 Ko. 8:9; 10:23, 24) Kwa hiyo, Yehova hatuambie manguo yenye tunapaswa kuvala, lakini anatupatia kanuni za kufuata. Tunapaswa kuvala mu njia yenye inamuletea sifa, yenye inaonyesha usawaziko, kiasi, na “akili ya muzuri.” (1 Ti. 2:9, 10) Njo maana, hatupendake kuvala mu njia yenye itafanya watu watukazie tu uangalifu. Kanuni za Biblia zinasaidia pia wazee waepuke kuweka sheria juu ya manguo ao juu ya namna ya kukata na kutengeneza nywele. w23.07 23-24 fu. 13-14
Siku ya Posho, 15 Mwezi wa 11
Munisikilize kwa uangalifu, na mukule mambo ya muzuri, na mutapata furaha nyingi katika vitu vyenye kujenga mwili kabisa.—Isa. 55:2.
Yehova anatumia mifano ya wale wanamuke wawili ili kuonyesha mambo yenye tunaweza kufanya juu tukuwe na furaha wakati wenye kuya. Wale wenye wanakubali mualiko wa “mwanamuke mujinga” wanapenda kujifurahisha kwa kufanya uasherati. Matendo yao itawafikisha mu “sehemu za chini kabisa za Kaburi.” (Mez. 9:13, 17, 18) Lakini, ile haitawafikia wale wenye wanakubali mualiko wa mwanamuke mwenye hekima! (Mez. 9:1)Tuko najifunza kupenda mambo yenye Yehova anapenda na kuchukia mambo yenye anachukia. (Zb. 97:10) Na tuko nafuraha juu tunaweza kualika wengine wajifunze kupitia “hekima ya kweli.” Zaidi ya ile, tuko sawa vile watumishi wenye wako “naita kwa sauti kubwa kutoka nafasi za juu za muji: Mutu yeyote mwenye hana uzoefu, aingie humu.” Faida zenye tuko napata na zenye wale wenye kukubali mualiko watapata haziko za leo tu, ni za lote. Zitafanya “tuishi” milele juu tutaendelea “kutembea moja kwa moja katika njia ya uelewaji.”—Mez. 9:3, 4, 6. w23.06 24 fu. 17-18
Siku ya Yenga, 16 Mwezi wa 11
Mutu mwenye hakasirike haraka ni muzuri zaidi kuliko mwanaume mwenye nguvu, na mutu mwenye kuzuia kasirani yake ni muzuri zaidi kuliko mutu mwenye anashinda muji.—Mez. 16:32.
Unajisikiaka namna gani wakati mwanafunzi mwenzako ao mufanyakazi mwenzako anakuuliza juu ya mambo yenye unaamini? Unakuwaka na wasiwasi? Haiko weye peke. Lakini, maulizo ya vile inaweza kukusaidia ujue mawazo yake na mambo yenye anaamini. Inaweza kukupatia nafasi ya kuzungumuza naye juu ya habari njema. Lakini wakati fulani mutu anaweza kukuuliza ulizo juu tu ya kupinga mambo yenye unaamini ao juu tu anapenda kubishana na weye. Ile haipaswe kutushangaza juu watu wengi wameambiwa habari za uongo juu ya mambo yenye tunaamini. (Mdo. 28:22) Zaidi ya ile, tunaishi mu “siku za mwisho,” wakati wenye watu wengi “hawataki makubaliano yoyote” na hata ni “wakali.” (2 Ti. 3:1, 3) Unaweza kujiuliza hivi: ‘Nini njo itanisaidia nibakie mwenye kutulia wakati mutu anapinga mambo yenye kutegemea Biblia yenye ninaamini?’ Sifa ya upole. Mutu mupole hakasirikake haraka. Lakini anaweza kujizuia wakati anachokozwa ao wakati hajue namna ya kujibia. w23.09 14 fu. 1-2
Siku ya Kwanza, 17 Mwezi wa 11
Utawaweka kuwa wakubwa katika dunia yote.—Zb. 45:16.
Wakati fulani, tunapewa mashauri yenye inatulinda ili tusiangukie mu mutego wa kupenda vitu vya kimwili na tuepuke mambo yenye inaweza kufanya tuvunje sheria za Mungu. Wakati tunafuata ile miongozo yenye Yehova anatutolea, tunapata baraka mingi. (Isa. 48:17, 18; 1 Ti. 6:9, 10) Bila shaka Yehova ataendelea kutumia wanadamu wenye wanamuwakilisha ili kututolea muongozo wakati wa taabu kubwa na hata mu Utawala wa Miaka Elfu. Je! Tutaendelea kufuata muongozo wake? Itakuwa mwepesi kufanya vile ikiwa tuko najikaza kufuata muongozo wenye Yehova anatutolea leo. Kwa hiyo, tuendelee kufuata muongozo wenye Yehova anatutolea, hata muongozo wenye anatutolea kupitia wanaume wenye ameweka ili kutuongoza. (Isa. 32:1, 2; Ebr. 13:17) Na wakati tuko nafanya vile, tutumainie kabisa Kiongozi wetu Yehova mwenye iko natuongoza ili tuepuke hatari zenye zinaweza kuharibu hali yetu ya kiroho. Pia Yehova iko natuongoza ili tufike kwenye tuko naenda, ni kusema mu dunia mupya kwenye tutapata uzima wa milele. w24.02 25 fu. 17-18
Siku ya Pili, 18 Mwezi wa 11
Mumeokolewa kupitia fazili zenye hazistahiliwe.—Efe. 2:5.
Mutume Paulo alikuwa na furaha wakati alikuwa namutumikia Yehova, lakini alipata magumu mingi. Mara mingi Paulo alikuwa nafanya safari za murefu, na ile wakati haikukuwa mwepesi kusafiri. Na wakati fulani mu safari zake, alijikuta “katika hatari kutokana na mito” na “katika hatari kutoka kwa wanyanganyi.” Tena, wakati fulani maadui wake walikuwa namupiga. (2 Ko. 11:23-27) Zaidi ya ile, Wakristo wenzake hawakukuwa namushukuru juu ya mambo yenye alifanya ili kuwasaidia. (2 Ko. 10:10; Flp. 4:15) Nini njo ilimusaidia Paulo aendelee kumutumikia Yehova? Mambo mingi yenye alijifunza mu Maandiko juu ya utu wa Yehova na mambo yenye alijionea njo yenye ilimusaidia sana. Alifikia kuwa hakika kama Yehova Mungu alimupenda. (Ro. 8:38, 39; Efe. 2:4, 5) Naye alifikia kumupenda sana. Alionyesha kama anamupenda Yehova “kwa kutumikia na kuendelea kutumikia watakatifu.”—Ebr. 6:10. w23.07 9 fu. 5-6
Siku ya Tatu, 19 Mwezi wa 11
Kwa mamlaka zenye kuwa kubwa.—Ro. 13:1.
Watu wengi wanajua kama tuko na lazima ya wakubwa wa serikali na kama tunapaswa kutii sheria fulani zenye “mamlaka zenye kuwa kubwa” zinaweka. Lakini walewale watu wanasita kutii sheria zenye wanaona kuwa hazifae ao zenye zinawaomba mambo mingi. Kwa mufano, fikiria sheria ya kulipa kodi ao taxe. Biblia inaonyesha kama serikali za wanadamu zinaongozwa na Shetani, zinaletea watu mateso, na kama hivi karibuni zitaharibiwa. (Zb. 110:5, 6; Muh. 8:9; Lu. 4:5, 6) Lakini inasema pia kama “mutu yeyote mwenye anapinga mamlaka amepinga mupango wa Mungu.” Kwa sasa Yehova ameruhusu serikali za wanadamu zitawale juu kukuwe utaratibu na anatuomba tutii zile serikali. Kwa hiyo, tunapaswa “kuwapatia wote haki zao,” kutia ndani kulipa taxe, kuwaheshimia, na kuwatii. (Ro. 13:1-7) Tunaweza kuona sheria fulani kuwa haifae, haiko ya haki, ao iko nguvu kutii. Lakini tunamutii Yehova, na Yehova anatuomba tutii wenye mamlaka wakati hawatuombe tufanye jambo yenye inavunja sheria yake.—Mdo. 5:29. w23.10 8 fu. 9-10
Siku ya Ine, 20 Mwezi wa 11
Roho ya Yehova ikamutia nguvu.—Amu. 15:14.
Wakati Samsoni alizaliwa, Wafilisti walikuwa natawala Waisraeli na walikuwa wanawagandamiza. (Amu. 13:1) Juu walikuwa wanawatawala kwa ukali, ile ililetea Waisraeli mateso mingi. Yehova alichagua Samsoni ili “aongoze katika kuokoa Israeli katika mukono wa Wafilisti.” (Amu. 13:5) Juu ya kutimiza ule mugao, Samsoni alipaswa kumutegemea Yehova. Siku moya, maaskari Wafilisti walikuya kumukamata Samsoni wakati alikuwa Lehi, yenye inawezekana ilikuwa katika Yuda. Watu wa Yuda waliogopa, kwa hiyo wakaamua kumutoa Samsoni kwa maadui. Ndugu zake mwenyewe walimufunga nguvu sana kwa kutumia kamba mbili za mupya, na wakamupeleka kwa Wafilisti. (Amu. 15:9-13) Lakini, “roho ya Yehova ikamutia nguvu,” na akajifungua zile kamba. Kisha “akaona mufupa wa mubichi wa taya ya punda-dume,” akaulokota na akautumia ili kuua Wafilisti 1000!—Amu. 15:14-16. w23.09 2 fu. 3-4
Siku ya Tano, 21 Mwezi wa 11
Hii ni kulingana na kusudi la milele lenye alifanyiza kuhusiana na Kristo, Yesu Bwana wetu.—Efe. 3: 11.
Yehova ametufunulia mu Biblia hatua kwa hatua “kusudi [lake] la milele.” (Efe. 3:11) Hata kama anaweza kutumia njia tofauti, mambo inakuwaka tu vile anapenda kwa sababu “amefanya kila kitu kitimize kusudi lake.” (Mez. 16:4) Na matokeo ya mambo yenye Yehova iko nafanya itadumu milele. Kusudi ya Yehova ni nini, na ni njia gani tofauti zenye alitumia ili kuitimiza? Mungu aliambia wanadamu wa kwanza kusudi yake kwa ajili yao. Walipaswa “kuzaa na kuwa wengi, kujaza dunia na kuitawala, na kutawala . . . kila kiumbe chenye uzima” ku dunia. (Mwa. 1:28) Wakati Adamu na Eva waliasi, ile ilifanya zambi iingie mu familia ya wanadamu. Lakini ile haikuzuia Yehova kutimiza kusudi yake. Alitafuta njia ingine ya kutimiza kusudi yake. Palepale alisema kama atasimamisha Ufalme mbinguni wenye utatimiza kusudi yenye alikuwa nayo ku mwanzo kwa ajili ya wanadamu na dunia.—Mt. 25:34. w23.10 20 fu. 6-7
Siku ya Posho, 22 Mwezi wa 11
Kama Yehova hangekuwa musaidizi wangu, Kisha wakati kidogo tu ningekuwa nimekufa.—Zb. 94:17.
Yehova anaweza kutusaidia tuendelee kumutumikia. Inaweza kuwa nguvu kuendelea kumutumikia Yehova, zaidi sana ikiwa tumepambana na uzaifu fulani kwa wakati murefu. Wakati fulani, uzaifu wetu unaweza kuonekana kuwa wa nguvu kupita uzaifu wenye mutume Petro alipambana nao. Lakini Yehova anaweza kutupatia nguvu ili tuendelee kuupiganisha. (Zb. 94:18, 19) Kwa Mufano, mbele ndugu fulani ajifunze kweli alikuwa na tabia ya kufanya ngono na wanaume wenzake kwa miaka mingi. Aliamua kabisa kuachana na ule mwenendo muchafu, lakini wakati fulani alipambana na tamaa za mubaya. Ni nini ilimusaidia aendelee kuzipiganisha? Anasema hivi: “Yehova alinitia nguvu. Kwa musaada wa roho ya Yehova . . . , nimejifunza kama inawezekana kuendelea kuishi maisha yenye Yehova anapenda . . . Yehova amenitumia mu njia mbalimbali. Hata kama niko na uzaifu, anaendelea kunitia nguvu.” w23.09 23 fu. 12
Siku ya Yenga, 23 Mwezi wa 11
Matokeo ya unyenyekevu na kumuogopa Yehova ni utajiri na utukufu na uzima.—Mez. 22:4.
Ndugu kijana, hauwezi kuwa Mukristo mwenye kukomaa kiroho kama haujikaze. Unapaswa kuchagua mifano mizuri ya kuiga, kukomalisha uwezo wa kufikiri, kujifunza ufundi fulani wa maana, na kujitayarisha kwa ajili ya madaraka ya wakati wenye kuya. Wakati unafikiria mambo yote yenye unapaswa kufanya, unaweza kuwaza kama iko nguvu kwako. Lakini utaweza. Kumbuka kama Yehova iko tayari kukusaidia. (Isa. 41:10, 13) Ndugu na dada mu kutaniko watakusaidia pia. Wakati utafikia kuwa mwanaume Mukristo mwenye kukomaa kiroho, utakuwa na maisha yenye kufurahisha sana. Ndugu kijana, tunakupenda! Yehova na akubariki sana wakati uko unafanya yako yote ili kufikia kuwa mwanaume Mukristo mwenye kukomaa kiroho. w23.12 29 fu. 19-20
Siku ya Kwanza, 24 Mwezi wa 11
Kuachilia kosa.—Mez. 19:11.
Wazia munakutana pamoya na ndugu na dada ili kujifurahisha. Munapitisha wakati ya muzuri pamoja, munakamata picha pamoja. Juu haujue kama ile picha ya kwanza itatoka muzuri, unakamata picha mbili zingine. Sasa uko na picha tatu. Lakini mu picha moya unaona kama ndugu fulani alifunga sura. Utavuta ile picha juu ungali na picha zingine mbili kwenye kila mutu iko nacheka, kutia ndani ule ndugu. Mara mingi tunachungaka mu akili wakati za muzuri zenye tulipitisha pamoya na ndugu na dada zetu. Lakini wazia wakati moya kati ya zile, ndugu ao dada alisema ao kufanya jambo fulani yenye haukufurahia. Utafanya nini juu ya ile? Hauone kama ni muzuri uivute mu akili sawa vile ulivuta ile picha moya? (Efe. 4:32) Juu tuko na wakati zingine za mingi za muzuri zenye tumepitisha pamoja naye. Na zile njo tunapaswa kuweka mu akili na kuzifurahia. w23.11 12-13 fu. 16-17
Siku ya Pili, 25 Mwezi wa 11
Wanamuke wajipambe kwa nguo zenye kufaa, . . . kwa njia yenye kufaa wanamuke wenye wanasema kama wanashikamana na Mungu.—1 Ti. 2:9, 10.
Neno ya kigiriki yenye kutumiwa mu hii andiko inaonyesha kama nguo zenye mwanamuke Mukristo anavaa zinapaswa kuonyesha kama anaheshimia wengine na anahangaikia mawazo yao. Tunawafurahia sana nyiye dada zetu Wakristo wenye kukomaa kiroho juu munavaa kwa kiasi! Utambuzi ni sifa ingine yenye dada wote wenye kukomaa kiroho wanaonyesha. Utambuzi ni nini? Ni uwezo wa kutofautisha jambo ya muzuri na ya mubaya na kuchagua kufanya jambo ya muzuri. Tuchunguze mufano wa Abigaili. Bwana yake alikamata uamuzi wa mubaya wenye ungekuwa na matokeo ya mubaya sana juu ya watu wote wa nyumba yake. Abigaili alitenda bila kukawia. Juu alitambua jambo ya muzuri ya kufanya, aliokoa maisha ya watu wengi. (1 Sa. 25:14-23, 32-35) Utambuzi unatusaidia pia kujua wakati wa kusema na wakati wa kunyamaza. Na unatusaidia tuhangaikie wengine bila kuingia mu mambo yao ya kipekee.—1 Te. 4:11. w23.12 20 fu. 8-9
Siku ya Tatu, 26 Mwezi wa 11
Tufurahi basi, kwa kutegemea tumaini la utukufu wa Mungu.—Ro. 5:2.
Mutume Paulo aliandikia hii maneno kutaniko yenye ilikuwa Roma. Kule, ndugu na dada walikuwa wamejifunza kuhusu Yehova na Yesu, walionyesha imani, na walifikia kuwa Wakristo. Kwa hiyo Mungu ” aliwatangaza kuwa wenye haki kupitia imani” na aliwatia mafuta kwa roho takatifu. (Ro. 5:1) Kwa kweli, walipata tumaini ya muzuri sana. Kisha Paulo aliandikia Wakristo watiwa-mafuta wa Efeso kuhusu tumaini yenye Mungu alikuwa amewapatia. Ile tumaini ilitia ndani uriti kwa ajili ya watakatifu. (Efe. 1:18) Pia, Paulo aliambia Wakolosai fasi kwenye tumaini yao itatimia kwa kusema hivi: “Tumaini lenye linawekwa kwa ajili yenu mbinguni.” (Kol. 1:4, 5) Tumaini ya Wakristo watiwa-mafuta ni kwamba watafufuliwa ili waishi milele mbinguni, kwenye watatawala pamoya na Kristo.—1 Te. 4:13-17; Ufu. 20:6. w23.12 9 fu. 4-5
Siku ya Ine, 27 Mwezi wa 11
Amani ya Mungu yenye kupita uelewaji wote italinda mioyo yenu na nguvu zenu za akili.—Flp. 4:7.
Neno ya kwanza-kwanza yenye inatafsiriwa “kulinda,” ilikuwa neno ya kijeshi yenye ilitumiwa ili kuzungumuzia maaskari wenye walikuwa nalinda muji ili usishambuliwe. Watu wenye waliishi mu muji wenye kulindwa, walilala kwa amani juu walijua kama maaskari walikuwa kwenye milango mikubwa ya muji. Vilevile, wakati amani ya Mungu inalinda moyo wetu na akili yetu, tunatulia juu tunajua kama tuko salama. (Zb. 4:8) Kama vile habari ya Hana inaonyesha, hata kama hali yetu haibadilike palepale tunaweza kuwa na amani kwa kadiri fulani. (1 Sa. 1:16-18) Na wakati tunatulia, mara mingi inakuwaka mwepesi zaidi kufikiri na kukamata maamuzi yenye hekima. Tunaweza kufanya nini? Wakati uko na mahangaiko, tafuta mulinzi wa mufano. Namna gani? Sali mupaka wakati utapata amani ya Mungu. (Lu. 11:9; 1 Te. 5:17) Kama uko napambana na magumu, endelea kusali na utaona namna amani ya Yehova italinda moyo wako na akili yako.—Ro. 12:12. w24.01 21 fu. 5-6
Siku ya Tano, 28 Mwezi wa 11
Baba yetu mwenye kuwa mbinguni, jina lako litakaswe.—Mt. 6:9.
Juu ya kutakasa jina ya Baba yake, Yesu alivumilia wakati aliteswa, wakati alitukanwa, na kushitakiwa mambo ya uongo. Alijua kama alikuwa amemutii Baba yake mu mambo yote; hakukuwa na sababu ya kusikia haya. (Ebr. 12:2) Alijua kama Shetani alikuwa namujaribu moja kwa moja mu ile wakati ya nguvu sana. (Lu. 22:2-4; 23:33, 34) Shetani alitumainia kama Yesu atavunja ushikamanifu wake, lakini mambo haikukuwa vile hata kidogo! Yesu alionyesha waziwazi kama Shetani ni muongo kabisa na kama Yehova iko na watumishi washikamanifu wenye wanaendelea kuwa washikamanifu hata wakati wanapatwa na majaribu ya nguvu sana! Na weye unapenda kumufurahisha Mufalme wetu mwenye iko natawala? Endelea kusifu jina ya Yehova kwa kusaidia wengine wajue Mungu wetu iko namna gani. Wakati unafanya vile, unafuata hatua za Yesu. (1 Pe. 2:21) Kama Yesu, uko namufurahisha Yehova na kuonyesha kama adui yake Shetani ni muongo kabisa! w24.02 11-12 fu. 11-13
Siku ya Posho, 29 Mwezi wa 11
Nitamulipa Yehova nini kwa mema yote yenye amenitendea?—Zb. 116:12.
Kwa miaka tano yenye imepita, zaidi ya watu milioni moya wamebatizwa na kuwa Mashahidi wa Yehova. Wakati unajitoa kwa Yehova, unachagua kuwa mwanafunzi wa Yesu Kristo, na kufanya mapenzi ya Mungu njo inakuwa jambo ya maana zaidi mu maisha yako. Wakati Mukristo anajitoa kwa Yehova, ile inaonyesha kama iko tayari kufanya nini? Yesu alisema hivi: “Kama mutu yeyote anataka kunifuata, lazima ajikane mwenyewe.” (Mt. 16:24) Musemwa ya Kigiriki wenye kutafsiriwa “lazima ajikane mwenyewe” unaweza pia kutafsiriwa “anapaswa kujiambia hapana.” Juu umejitoa sasa kwa Yehova na umekuwa mutumishi wake, unapaswa kusema hapana kwa kila kitu yenye inapingana na mapenzi yake. (2 Ko. 5:14, 15) Ile inatia ndani kusema hapana ku “matendo ya mwili” sawa vile uasherati. (Gal. 5:19-21; 1 Ko. 6:18) Kuepuka ile mambo kutafanya maisha yako ikuwe nguvu? Hapana, haitakuwa nguvu kama unamupenda Yehova na uko hakika kama sheria zenye anatoa zinakuletea faida.—Zb. 119:97; Isa. 48:17, 18. w24.03 2 fu. 1; 3 fu. 4
Siku ya Yenga, 30 Mwezi wa 11
Nimekukubali.—Lu. 3:22.
Yehova anapatia roho takatifu wale wenye anakubali. (Mt. 12:18) Tunaweza kujiuliza hivi: ‘Nimeweza kuonyesha sehemu fulani ya tunda la roho ya Mungu mu maisha yangu?’ Umetambua kama unavumilia wengine zaidi kuliko vile ulikuwa mbele umujue Yehova? Kwa kweli, kadiri unajifunza kuonyesha zaidi sifa za tunda la roho ya Mungu, ni vile inaonekana wazi zaidi kama Yehova anakukubali! Yehova anatumia samani ya bei ya ukombozi kwa wale wenye anakubali. (1 Ti. 2:5, 6) Lakini tutafanya nini ikiwa moyo wetu unakatala kuamini kama Yehova anatukubali, hata kama tuko na imani katika bei ya ukombozi na tumebatizwa? Kumbuka kama wakati fulani hatupaswe kutumainia moyo wetu, lakini tunapaswa kumutumainia Yehova. Anaona wale wenye kuamini bei ya ukombozi kuwa wenye haki na anaahidi kuwabariki.—Zb. 5:12; Ro. 3:26. w24.03 30 fu. 15; 31 fu. 17