Mapendekezo Ili Kutolea Watu Broshua—Sehemu 2
ICHUNGWE
Mapendekezo mbalimbali yanatolewa katika nyongeza hii ili kukusaidia kutayarisha utoaji mbalimbali kwa ajili ya kutolea watu broshua. Mapendekezo haya yanaweza kurekebishwa kulingana na hali ya kwenu.—Ona Huduma Yetu ya Ufalme ya Januari 2005, uku. 8 na ya Juni 2005, uku. 3, 4.
Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai—Wewe Waweza Kulipataje?
Baada ya kumsalimu mwenye nyumba, unaweza kusema:
“Bila shaka maisha leo ni yenye kujaa matatizo na vivunja moyo. Je, unafikiri kwamba hivi ndivyo maisha yangepaswa kuwa? [Acha mtu ajibu.] Broshua hii inaonyesha kwamba kusudi la Mungu la mwanzoni kuhusu wanadamu na dunia bado litatimizwa. [Zungumzieni picha kwenye ukurasa wa 20-21. Kisha soma fungu la 9, ukikazia Isaya 14:24 na 46:11.] Siku ingine nitakapokuja, nitapenda kukuonyesha mahali ambapo Biblia inasema kuhusu jinsi Mungu atakavyorudisha Paradiso duniani.” Tolea mtu broshua, na ufanye mpango wa kurudi.
Unaporudi, unaweza kusema:
“Wakati wa mazungumzo yetu yaliyopita nilikwambia kwamba kusudi la Mungu kuhusu wanadamu ni kwamba waishi milele katika paradiso duniani. [Onyesha tena picha kwenye ukurasa wa 20-21.] Ona kwamba Yesu, Petro, na Daudi walizungumza kuhusu Paradiso.” Mwombe achukue broshua yake. Kisha mfungue kwenye ukurasa wa 21-22, na mchunguze fungu la 10-13. Umtolee funzo la Biblia, au fanya mpango ili kuchunguza kimoja cha vichwa vidogo kwenye ukurasa wa 29-30 kwenye ziara ifuatayo.
Mhubiri kijana anaweza kusema:
“Watu wengi wa umri wangu hawana uhakika kuhusu wakati ujao. Je, unafikiri kwamba maisha yatakuwa bora kwa kizazi kinachokuja? [Acha mtu ajibu.] Biblia inazungumza kuhusu wakati ujao mzuri kwa ajili ya wanadamu wote. [Fungua picha kwenye ukurasa wa 31 wa broshua, na usome maneno yaliyoandikwa ndani ya picha. Kisha soma 2 Petro 3:13.] Broshua hii inatoa habari kuhusu baraka ambazo Mungu anawekea wanadamu. [Onyesha vichwa vidogo vinavyoandikwa kwa herufi nzito nyeusi kwenye ukurasa wa 29-30, na umtolee broshua.] Ningependa kukutembelea tena ili tuzungumze pamoja kuhusu ahadi ya Mungu ya kumaliza vita.” Fanya mipango ili kurudi.
Unaporudi, unaweza kusema:
“Wakati wa mazungumzo yetu ya kwanza nilipokutembelea, nilionyesha kwa kifupi kusudi la Mungu la kurudisha paradiso duniani. [Zungumzia tena picha kwenye ukurasa wa 31.] Ningependa kusikia mawazo yako kuhusu ahadi ya Mungu ya kumaliza vita.” Mwombe achukue broshua yake. Kisha msome na kuzungumzia fungu la 3-6 kwenye ukurasa wa 29. Fanya mipango ili kuchunguza fungu la 7-8 kwenye ziara ifuatayo.
Mtu mwenye umri mkubwa anapohubiri na mtoto, anaweza kujitambulisha yeye na mtoto na kusema:
“Ukiruhusu, ________ angependa kukuonyesha picha na kusoma andiko moja kutoka katika Biblia. [Mtoto anaonyesha picha na kusoma maneno yanayoandikwa ndani ya picha kwenye ukurasa wa 31 na kisha anasoma Ufunuo 21:4.] Broshua hii inazungumzia yale ambayo Mungu atafanya kuhusu matatizo tunayopambana nayo leo. [Onyesha kwa kifupi vichwa vidogo vinavyoandikwa kwa herufi nzito nyeusi kwenye ukurasa wa 29-30, na umtolee broshua.] Tutakaporudi, nitapenda kukuonyesha yale Biblia inayosema kuhusu mwisho wa matatizo yote ya kiafya.”
Kwenye ziara ya kurudia, mtu mwenye umri mkubwa anaweza kusema:
“Wakati wa mazungumzo yetu ya kwanza, nilisema kwamba nilipenda kukuonyesha yale Biblia inayosema kuhusu mwisho wa matatizo yote ya kiafya. Ona jambo linalosemwa hapa.” Mwombe achukue broshua yake. Kisha mchunguze fungu la 9-14 kwenye ukurasa wa 29. Umtolee funzo la Biblia, au fanya mipango ili kuchunguza fungu la 15-17 kwenye ziara ifuatayo.