TAREHE 20-26/10
MUHUBIRI 9-10
Wimbo 30 na Sala | Maneno ya Utangulizi (Dak. 1)
1. Ukuwe na Mawazo ya Muzuri Juu ya Magumu Yako
(Dak. 10)
Kama tunapata magumu, ile haimaanishe kama Yehova hatukubali (Muh 9:11; w23.01 uku. 15 fu. 4)
Juu tuko naishi mu ulimwengu muovu wa Shetani, tujue kama magumu itatufikia tu (Muh 10:7; w19.09 uku. 5 fu. 10)
Hata wakati tuko napitia mu magumu, tujikaze kufurahia mambo ya muzuri yenye Yehova alishatupatia (Muh 9:7, 10; w11 15/10 uku. 8 fu. 1-2)
2. Mali ya Kiroho
(Dak. 10)
Muh 10:12-14—Hii andiko inapatia onyo gani mutu mwenye anasemaka mingi? (it-F “Bavardage, Calomnie” fu. 4, 8)
Mu usomaji wa Biblia wa hii juma, ulipata mali gani ya kiroho yenye ungependa kuzungumuzia?
3. Usomaji wa Biblia
(Dak. 4) Muh 10:1-20 (th somo ya 11)
4. Kuanzisha Mazungumuzo
(Dak. 3) MAHUBIRI YA MAHALI PA WATU WENGI. Anzisha mazungumuzo na mutu mwenye iko na huzuni. (lmd somo ya 3 nukta ya 4)
5. Kuanzisha Mazungumuzo
(Dak. 4) MAHUBIRI YA WAKATI WOWOTE. Zungumuzia kweli moya kati ya “Kweli Zenye Tunapendaka Kufundisha” yenye kuwa mu nyongeza ya A ya broshua Penda Watu, pamoya na mutu mwenye anakuambia kama iko na magumu juu ya kupata makuta. (lmd somo ya 4 nukta ya 4)
6. Kufanya Banafunzi
(Dak. 5) lff somo ya 17 kwa kifupi, maulizo ya kujikumbusha, na pima kufanya hivi. (lmd somo ya 12 nukta ya 3)
Wimbo 47
7. Yehova Atakusaidia mu Wakati wa Magumu
(Dak. 15) Mazungumuzo.
Kila siku, tunakuwaka na aina mbalimbali ya magumu. Lakini, kunakuwaka magumu ingine ya nguvu yenye inaweza kutokea kwa kushitukia, na inaweza kutuhangaisha kiakili, kimwili, na hata kiroho. Sasa ni nani anaweza kutusaidia? Na tunaweza kufanya nini kama magumu ya vile inatokea?
Hata kama tunapata magumu gani, tujue kama Yehova njo mwenye ‘anafanyaka nyakati zetu kuwa imara.’ (Isa 33:6) Juu atusaidie, Yehova anapenda tukuwe na usawaziko. (Mez 11:2) Kama tunapata magumu ya kushitukia, tuko na lazima ya wakati juu ya kukamata maamuzi ya muzuri, juu ya kujihangaikia siye benyewe ao kuhangaikia mutu mwenye tunapendaka. Tuko pia na lazima ya wakati juu ya kuhuzunikia mambo yenye inatufikia. (Muh 4:6)
Yehova anatumiaka bandugu na badada juu ya kutiana moyo. Njo maana tunapaswa kuitika musaada wabo ao kuomba batusaidie. Kumbuka kama bandugu na badada yako banakupendaka sana, na batafurahia sana kukusaidia.
Musome 2 Wakorinto 4:7-9. Kisha uliza basikilizaji:
Juu ya nini tunapaswa kuendelea kuwa na programu ya muzuri ya kiroho hata mu wakati ya magumu?
Muangalie VIDEO Yehova Iko Karibu na Bale Benye Kuvunjika Moyo. Kisha uliza basikilizaji:
Namna gani Yehova alisaidia ndugu Septer na bibi yake?
Namna gani bandugu na badada balibasaidia?
Mufano wa ndugu Septer na bibi yake unakufundisha nini ingine?
8. Funzo ya Biblia ya Kutaniko
(Dak. 30) lfb somo ya 28, utangulizi wa sehemu ya 6, na somo ya 29