HABARI YA KUJIFUNZA YA 9
WIMBO 51 Ninajitoa kwa Mungu!
Batizwa Bila Kukawia
“Sababu gani unakawia? Simama, ubatizwe.”—MDO. 22:16.
WAZO KUBWA
Kuchunguza mufano wa Wasamaria, Sauli wa Tarso, Kornelio na Wakorinto kutakutia moyo juu ufikie kubatizwa.
1. Ubatizo utakuletea faida gani?
UNAMUPENDA Yehova Mungu, mwenye alikupatia mambo yote ya muzuri yenye uko nayo na mwenye alikupatia uzima? Unapenda kumuonyesha kama unamupenda? Namna ya muzuri sana ya kufanya vile ni kujitoa kwake na kubatizwa. Kama unafanya vile, utaingia mu familia ya Yehova. Na Yehova Baba yako na rafiki yako atakuongoza na atakuhangaikia juu sasa unakuwa wake. (Zb. 73:24; Isa. 43:1, 2) Tena, kujitoa kwa Yehova na kubatizwa kunakupatia tumaini ya kuishi milele.—1 Pe. 3:21.
2. Tutazungumuzia nini mu hii habari?
2 Kuko kitu yenye inakuzuia kubatizwa? Kama ni vile, haiko weye peke. Kuko batu mingi sana benye balipaswa pia kubadilisha mwenendo na namna yabo ya kuwaza juu bastahili kubatizwa. Lakini sasa biko namutumikia Yehova kwa furaha na kwa bidii. Mifano ya batu fulani ba mu karne ya kwanza benye balifikia kubatizwa inaweza kukufundisha nini? Acha tuone mambo yenye ingebazuia kubatizwa na mambo yenye mufano wabo unaweza kutufundisha.
WASAMARIA WALIBATIZWA
3. Ni mambo gani ingezuia Wasamaria fulani kubatizwa?
3 Mu siku za Yesu kulikuwa dini ya Wasamaria. Waliishi karibu-karibu na Shekemu ya zamani na Samaria, kaskazini ya Yudea. Mbele Wasamaria wabatizwe, walipaswa kukubali Neno ya Mungu yote na kujifunza mambo mingi juu ya Neno ya Mungu. Wasamaria walikubali kama vitabu tano tu vya kwanza vya Biblia, ni kusema Mwanzo mupaka Kumbukumbu la Torati na pengine pia kitabu ya Yoshua, njo viliongozwa na roho ya Mungu. Lakini, walikuwa pia nangoya Masiya akuye, vile ahadi ya Mungu yenye kuwa mu Kumbukumbu la Torati 18:18, 19 ilionyesha. (Yoh. 4:25) Juu wabatizwe, walipaswa kumukubali Yesu kuwa Masiya mwenye aliahidiwa. “Wengi kati ya Wasamaria” walifanya vile. (Yoh. 4:39) Na juu Wakristo wengi walikuwa Wayahudi, Wasamaria fulani walipaswa kuachana na ubaguzi wa nguvu wenye ulikuwa kati yao na Wayahudi.—Lu. 9:52-54.
4. Kulingana na Matendo 8:5, 6, 14, Wasamaria fulani walitenda namna gani wakati Filipo aliwahubiria?
4 Ni nini ilisaidia Wasamaria wafikie kubatizwa? Wakati Filipo mweneza-injili aliwahubiria “juu ya Kristo,” Wasamaria fulani ‘walikubali neno la Mungu.’ (Soma Matendo 8:5, 6, 14.) Filipo alikuwa Muyahudi, lakini hawakukatala kumusikiliza. Pengine walikumbuka maandiko fulani yenye kuwa mu vitabu tano vya kwanza vya Biblia yenye inaonyesha kama Mungu hana ubaguzi. (Kum. 10:17-19) Ikuwe ni vile ao hapana, walikazia “uangalifu mambo yenye Filipo alisema” juu ya Kristo, na walikubali ushuhuda wenye ulionyesha wazi kama Mungu alikuwa namutegemeza Filipo. Alifanya miujiza mingi, kwa mufano aliponyesha wagonjwa, na kufukuza pepo wachafu.—Mdo. 8:7.
5. Mufano wa Wasamaria, unaweza kukufundisha nini?
5 Ubaguzi na kukosa ujuzi kungezuia Wasamaria kufanya maendeleo. Lakini hawakuacha ile iwazuie. Kisha kuwa hakika kama mambo yenye Filipo aliwafundisha ni ya kweli, Wasamaria hawakukawia kubatizwa. Biblia inasema hivi: “Wakati walimuamini Filipo, mwenye alikuwa anatangaza habari njema ya Ufalme wa Mungu na ya jina la Yesu Kristo, wanaume na vilevile wanamuke walikuwa wanabatizwa.” (Mdo. 8:12) Uko hakika kama Neno ya Mungu ni kweli na kama Mashahidi wa Yehova hawana ubaguzi na wanajikaza kuonyeshana upendo, sifa yenye inatambulisha Wakristo wa kweli? (Yoh. 13:35) Kama uko hakika na ile mambo, usiogope kubatizwa, Yehova atakubariki.
6. Mufano wa Ruben unaweza kukusaidia namna gani?
6 Ruben, wa mu Alemanye, alikomalia mu familia ya Mashahidi. Lakini, wakati alikuwa kijana, alikuwa na mashaka kama Yehova iko. Alifanya nini juu ya kumaliza mashaka yake? Alielewa kama alikosa ujuzi, kwa hiyo, aliamua kufanya jambo fulani. Anasema hivi: “Mu funzo yangu ya kipekee, nilijifunza mambo yenye ingenisaidia nipiganishe mashaka. Mara mingi nilijifunza habari yenye ilihusu mageuzi.” Alisoma kitabu Je, Kuna Muumba Anayekujali? Ile kitabu ilimusaidia sana Ruben. Alijiambia hivi: ‘Ok! Yehova anakuwaka kabisa.’ Na wakati Ruben alitembelea makao makubwa, aliguswa moyo wakati aliona umoja wenye kuwa kati ya bandugu na badada ba mu dunia yote. Wakati Ruben alirudia Alemanye, alibatizwa na miaka 17. Kama uko na mashaka juu ya mambo yenye umejifunza, fanya utafiti mu vichapo vyetu. “Ujuzi wenye hauna makosa” unaweza kumaliza mashaka. (Efe. 4:13, 14) Na wakati unasikia habari juu ya namna batu ya Yehova mu dunia yote biko na upendo na umoja na unajionea ile mu kutaniko yako, utafurahia zaidi familia ya bandugu na badada ba mu dunia yote.
SAULI WA TARSO ALIBATIZWA
7. Sauli alipaswa kubadilisha mawazo gani?
7 Fikiria mufano wa Sauli wa Tarso. Alikuwa nafanya maendeleo ya muzuri mu dini ya Wayahudi na alianza kujulikana sana kati ya Wayahudi. (Gal. 1:13, 14; Flp. 3:5) Wakati Wayahudi walianza kuona Wakristo kuwa waasi-imani, Sauli alitesa sana Wakristo. Aliwaza kama alikuwa nafanya mapenzi ya Mungu, lakini alikosea. (Mdo. 8:3; 9:1, 2; 26:9-11) Sauli alijua kama kumuamini Yesu na kubatizwa, kungemuletea mateso na alipaswa kuwa tayari kuteswa.
8. (a) Nini njo ilisaidia Sauli afikie kubatizwa? (b) Sawa vile Matendo 22:12-16 inasema, namna gani Anania alimusaidia Sauli? (Ona pia picha.)
8 Ni nini ilimusaidia Sauli abatizwe? Wakati Yesu mwenye alikuwa sasa mbinguni alimutokea, Sauli akakuwa kipofu. (Mdo. 9:3-9) Alifunga kwa siku tatu, na bila shaka aliwaza sana juu ya jambo yenye ilimufikia. Sauli akakuwa hakika kama Yesu alikuwa Masiya na kama banafunzi wa Yesu balikuwa mu dini ya kweli. Inawezekana zamiri ilimusumbua sana juu ya namna alichangia kumuua Stefano! (Mdo. 22:20) Ku mwisho wa zile siku tatu, mwanafunzi mwenye kuitwa Anania alikuya kumuona Sauli, alimuponyesha juu aweze tena kuona, na akamutia moyo abatizwe bila kukawia. (Soma Matendo 22:12-16.) Kwa unyenyekevu Sauli alikubali musaada wa Anania na akabatizwa.—Mdo. 9:17, 18.
Utakubali kutiwa moyo ili kubatizwa, sawa vile Sauli alifanya? (Ona fungu ya 8)
9. Mufano wa Sauli unakufundisha nini?
9 Mufano wa Sauli unaweza kutufundisha mambo mingi. Kiburi na kuogopa banadamu vingemuzuia kubatizwa. Lakini hakuruhusu ile mambo imuzuie. Sauli alikuwa munyenyekevu na alikuwa tayari kubadilisha maisha yake juu ya kuwa mwanafunzi wa Yesu. (Mdo. 26:14, 19) Alikuwa tayari kuwa Mukristo hata kama alijua kama kuwa Mukristo kutamuletea mateso. (Mdo. 9:15, 16; 20:22, 23) Kisha kubatizwa, aliendelea kumutumainia Yehova amusaidie kuvumilia majaribu. (2 Ko. 4:7-10) Wakati unabatizwa na kuwa Shahidi wa Yehova, na weye unaweza kupata majaribu ya imani ao magumu; lakini hauko weye peke. Unaweza kuwa hakika kama Yehova na Kristo wataendelea kukutegemeza.—Flp. 4:13.
10. Mufano wa Anna unaweza kukusaidia namna gani?
10 Anna alikomalia mu Ulaya ya Mashariki, mu familia ya Kikurdi. Kisha mama yake kubatizwa, baba yake alimuruhusu aanze kujifunza Biblia wakati alikuwa na miaka 9. Lakini, batu ya jamaa yake benye balikuwa naishi pamoya na familia ya Anna, habakufurahi. Batu ya jamaa yake baliona kama ni laana mutu kuacha dini ya batu ya familia yake. Wakati Anna alikuwa na miaka 12, aliomba baba yake ruhusa juu alipenda kubatizwa. Baba yake alipenda kujua ikiwa ule uamuzi ulikuwa ya Anna ao kulikuwa mutu mwenye alikuwa namuchochea kukamata ule uamuzi. Anna alijibia hivi: “Ninamupenda Yehova.” Baba yake aliitika abatizwe. Kisha pale, batu ya jamaa yake balimuzarau na kumutendea mubaya mu njia mingi. Mutu moya wa mu jamaa yake alimuambia: “Kama ungekuwa hata shindikana na ungekuwa navuta tumbako, ingekuwa muzuri kidogo kuliko kuwa Shahidi wa Yehova.” Nini njo ilisaidia Anna kuvumilia ile hali? Anasema hivi: “Yehova alinisaidia nikuwe na nguvu, na mama yangu na baba yangu balinitegemeza sana.” Anna angali nakumbuka namna alijionea mukono wa Yehova mara mingi mu maisha yake. Anajikumbushaka ile mambo kila wakati juu asisaabu namna Yehova alimusaidia. Kama uko naogopa kama bengine batakutesa, kumbuka kama Yehova atakusaidia na weye.—Ebr. 13:6.
KORNELIO ALIBATIZWA
11. Kornelio alikuwa mu hali gani?
11 Biblia inazungumuzia pia mufano wa Kornelio. Alikuwa “ofisa wa jeshi,” ni kusema, alikuwa nasimamia karibu maaskari 100 mu jeshi ya Roma. (Mdo. 10:1, maelezo ya chini.) Ile ingefanya batu bamujue sana na ajulikane mu jeshi. “Alipatia watu zawadi nyingi za rehema.” (Mdo. 10:2) Yehova alituma mutume Petro amutangazie habari njema. Cheo yenye Kornelio alikuwa nayo, ilimufanya akawie kubatizwa?
12. Nini njo ilimusaidia Kornelio abatizwe?
12 Nini ilisaidia Kornelio abatizwe? Biblia inasema kama “alikuwa anamuogopa Mungu.” Na aliendelea kumulilia Mungu bila kuacha. (Mdo. 10:2) Wakati Petro alimutangazia Kornelio habari njema, Kornelio na familia yake balimukubali Kristo na bila kukawia bakabatizwa. (Mdo. 10:47, 48) Ni wazi kama Kornelio alikuwa tayari kufanya mabadiliko yoyote juu aweze kumuabudu Yehova pamoya na familia yake.—Yos. 24:15; Mdo. 10:24, 33.
13. Mufano wa Kornelio unaweza kukufundisha nini?
13 Kama Sauli, Kornelio naye alikuwa na cheo. Cheo ingeweza kumuzuia kuwa Mukristo. Lakini hakuacha ile imuzuie. Na weye, unapaswa kufanya mabadiliko fulani ya maana mu maisha yako juu ubatizwe? Kama ni vile, Yehova atakusaidia. Yehova atakubariki kama unaazimia kutumikisha kanuni za Biblia mu maisha yako juu umutumikie.
14. Mufano wa Tsuyoshi unaweza kukusaidia namna gani?
14 Tsuyoshi, wa Japani, alipaswa kufanya mabadiliko fulani mu kazi yake juu astahili kubatizwa. Alikuwa musaidizi wa musimamizi wa masomo fulani yenye ilikuwa nafundisha batu namna ya kupanga maua. Wakati musimamizi hakufika ku mazishi, mara mingi Tsuyoshi alienda pa nafasi yake na alifanya desturi za Wabuda. Lakini, wakati Tsuyoshi alijifunza kweli juu ya wafu, zile desturi zilimuzuia kubatizwa. Kwa hiyo aliamua kama hatafanyaka tena zile desturi za Wabuda. (2 Ko. 6:15, 16) Tsuyoshi alizungumuza na musimamizi wake juu ya ile jambo. Matokeo ilikuwa nini? Tsuyoshi alindelea na kazi yake lakini hakukuwa tena nafanya zile desturi. Alibatizwa mwaka moya kisha kuanza kujifunza Biblia.a Kama uko na lazima ya kubadilisha kazi yako juu ya kumufurahisha Yehova, ukuwe hakika kama atakupatia weye na watu wa familia yako mambo yenye muko nayo lazima.—Zb. 127:2; Mt. 6:33.
WAKORINTO WALIBATIZWA
15. Ni nini ingezuia Wakorinto kumutumikia Yehova?
15 Batu ya Korinto ya zamani balijulikana kuwa batu benye balipenda sana bitu ya kimwili na benye kuwa na mwenendo muchafu. Batu mingi ba mu Korinto baliishi maisha yenye Mungu hakukubali. Bila shaka, ile hali ingefanya ikuwe nguvu kwa mutu mwenye kuishi mu ule muji amutumikie Yehova. Lakini, wakati Paulo alifika mu ule muji na kuhubiri habari njema juu ya Kristo, “Wakorinto wengi wenye walisikia wakaanza kuamini na kubatizwa.” (Mdo. 18:7-11) Kisha, Yesu Kristo alimutokea Paulo mu maono na kumuambia hivi: “Niko na watu wengi katika muji huu.” Kwa hiyo Paulo aliendelea kuhubiri mu ule muji kwa mwaka moya na nusu.
16. Ni nini ilisaidia batu fulani ba Korinto baweze kuachana na mambo yenye ingebazuia kubatizwa? (2 Wakorinto 10:4, 5)
16 Nini ilisaidia Wakorinto wabatizwe? (Soma 2 Wakorinto 10:4, 5.) Neno ya Mungu na roho yake yenye nguvu ilibasaidia kufanya mabadiliko makubwa mu maisha yabo. (Ebr. 4:12) Batu ya Korinto benye balikubali habari njema juu ya Kristo baliweza kuacha tabia za mubaya, sawa vile kulewa, kuiba, na tabia ya wanaume kulala na wanaume ao wanamuke kulala na wanamuke.—1 Ko. 6:9-11.b
17. Mufano wa Wakorinto unaweza kukufundisha nini?
17 Hata kama batu fulani ba Korinto balizoea sana kufanya mambo ya mubaya, habakusema kama habataweza hata siku moya kuwa Bakristo. Balifanya nguvu yote juu ya kuingia mu barabara ya mwembamba yenye inaongoza ku uzima wa milele. (Mt. 7:13, 14) Ni nguvu kwako kuachana na tabia fulani ya mubaya juu ustahili kubatizwa? Endelea kujikaza! Umulilie Yehova akupatie roho yake juu ikusaidie kupiganisha tamaa ya kufanya jambo ya mubaya.
18. Mufano wa Monika unaweza kukusaidia namna gani?
18 Monika, wa mu inchi ya Georgia, alijikaza sana kuachana na maneno machafu na mambo ya kujifurahisha yenye haifae juu astahili kubatizwa. Anasema hivi: “Wakati nilikuwa kijana, sala njo ilikuwa nguvu yangu. Yehova alijua kama nilipenda kufanya mambo ya muzuri, na sikuzote alinisaidia na kuniongoza.” Monika alibatizwa na miaka 16. Kuko tabia yenye unapaswa kuachana nayo juu umutumikie Yehova mu njia yenye anakubali? Endelea kumuomba akupatie nguvu yake juu ikusaidie kufanya mabadiliko. Yehova anakuwaka tayari kupatia batu yake roho yake takatifu.—Yoh. 3:34.
IMANI YAKO INAWEZA KUHAMISHA MILIMA
19. Ni nini inaweza kukusaidia kushinda mambo yenye inaweza kukuzuia kubatizwa? (Ona pia picha.)
19 Ukuwe hakika kama Yehova anakupenda na anapenda ukuwe mu familia yake. Hata ukuwe mu hali gani yenye inaweza kukuzuia usibatizwe, usisaabu ile jambo. Yesu aliambia hivi kikundi ya banafunzi yake mu karne ya kwanza: “Kama muko na imani yenye ukubwa wa mbegu ya haradali, mutaambia mulima huu, ‘toka hapa uende pale,’ na utatoka, na hakuna jambo lenye litawashinda.” (Mt. 17:20) Benye balikuwa pale wakati Yesu alisema ile maneno balikuwa balishapitisha na Yesu miaka kidogo tu, kwa hiyo imani yao ilikuwa ingali nakomala. Lakini Yesu alibahakikishia kama ikiwa banajikaza kuwa na imani yenye nguvu, Yehova atabasaidia kushinda mambo yenye iko nabazuia kubatizwa, hata kama ile mambo iko sawa milima. Yehova atakusaidia na weye kufanya vile!
Ukuwe hakika kama Yehova anakupenda na anapenda ukuwe mu familia yake (Ona fungu ya 19)c
20. Mifano ya Wakristo wa karne ya kwanza na wa wakati wetu wenye tumezungumuzia imekusaidia namna gani?
20 Kama unatambua mambo yenye iko nakuzuia kubatizwa, kamata hatua ya kuachana na ile mambo bila kukawia. Mifano ya Wakristo wa mu karne ya kwanza na wa mu siku zetu inaweza kukufariji na kukutia nguvu. Mufano wao ukutie moyo na ukuchochee kujitoa kwa Yehova na kubatizwa. Ule njo uamuzi wa maana sana wenye unaweza kukamata mu maisha!
WIMBO 38 Atakupatia Nguvu
a Habari juu ya maisha ya Ndugu Tsuyoshi Fujii, ilitolewa mu Amuka! ya tarehe 8, Mwezi wa 8, 2005, uku. 20-23.
b Ona ku jw.org video‘Juu ya Nini Unakawia Kubatizwa?’
c MAFASIRIO YA PICHA: Kikundi ya bandugu na badada biko nakaribisha kwa furaha benye banatoka kubatizwa.