Niache Kutembeza?
KULISHAPITA miaka mingi tangu unatembezaka gari. Unafurahia kufanya vile juu unaweza kuenda kote kwenye unapenda weye peke. Lakini batu ya familia yako na barafiki yako biko na wasiwasi juu ya usalama wako, na banawaza kama inaomba uache kutembeza. Hauelewe juu ya nini banawaza vile.
Na weye uko mu ile hali? Kama ni vile, nini njo itakusaidia uamue kama inaomba uache kutembeza gari ao hapana?
Kulingana na sheria ya inchi fulani, batu benye balishafikisha miaka fulani biko na lazima ya ruhusa ya munganga juu baendelee kutembeza. Bakristo benye banaishi mu inchi za vile banatii zile sheria, na banatii maamuzi yenye bakubwa ya serikali banakamata. (Ro. 13:1) Lakini hata kama mu inchi yenu hamuna zile sheria kuko mambo yenye inaweza kukusaidia ujue ikiwa inaomba uache kutembeza ao hapana.
CHUNGUZA NAMNA YAKO YA KUTEMBEZA
Shirika moya kwa ajili ya batu benye kuzeeka, inapendekeza batu benye kuzeeka benye banatembezaka bajiulize hii maulizo:
- Niko na magumu ya kusoma alama za mu barabara ao kuona busiku? 
- Haiko tena mwepesi kwangu kujigeuza, na ile inafanya ikuwe nguvu kwangu kugeuza kichwa juu ya kuangalia mu kioo ya gari ao fasi za pembeni-pembeni zenye hazionekane mu kioo? 
- Ni nguvu kwangu kutenda haraka, kwa mufano kutosha haraka mugulu ku accélérateur na kuitia ku pédale ya frein? 
- Natembezaka polepole mupaka ninazuia magari ingine kupita? 
- Nilishaponyoka mara mingi kufanya aksida ao gari yangu inachubuka-chubuka juu ya kugonga-gonga bitu? 
- Polisi alishakanisimamisha juu ya namna yangu ya kutembeza? 
- Nilishakasinzia na niko natembeza? 
- Ninakunywaka madawa yenye inaweza kuwa na matokeo ya mubaya juu ya namna yangu ya kutembeza? 
- Batu ya familia na barafiki bameniambia kama biko na wasiwasi juu ya namna yangu ya kutembeza? 
Kama unajibia ndiyo ku ulizo moya ao mbili kati ya ile maulizo, pengine ni lazima ufanye mabadiliko fulani. Kwa mufano unaweza kuamua kama hautakuwa natembeza tena mara mingi, zaidi sana busiku. Ujichunguze mara kwa mara juu ya kuona ikiwa namna yako ya kutembeza ingali muzuri. Unaweza kuuliza mutu wa familia ao rafiki akuambie iko na mawazo gani juu ya namna yako ya kutembeza; na unaweza hata kujiandikisha ku masomo kwenye banafundishaka namna ya kutembeza kwa usalama zaidi. Lakini kama ulijibia ndiyo ku zaidi ya ulizo mbili kati ya ile maulizo, inaweza kuwa muzuri uamue kuacha kutembeza.a
ACHA KANUNI ZA BIBLIA ZIKUONGOZE
Inaweza kuwa nguvu kutambua kama hatuko natembeza tena muzuri sawa zamani. Na wazo ya kuacha kutembeza ni wazo yenye haiko mwepesi kuzungumuzia. Sasa ni kanuni gani za Biblia njo zinaweza kukusaidia kuona mambo vile iko kabisa na kukamata uamuzi wa muzuri? Tuzungumuzie kanuni mbili.
Ukuwe na kiasi. (Mez. 11:2) Vile tuko nakomala mwili yetu inabadilikaka. Inakuwaka nguvu kwetu kuona muzuri, kusikia muzuri, nguvu yetu inapungukaka, na inakuwaka nguvu kwetu kutenda haraka sawa vile tulikuwa nafanya zamani. Kwa mufano, wakati batu fulani banaeneza miaka fulani banaachaka kucheza michezo fulani, juu banatambua kama vile biko nakomala inakuwa mwepesi kwabo kulumia. Ni vile pia juu ya kutembeza gari. Mutu mwenye iko na kiasi anaweza kuamua kuacha kutembeza wakati anatambua kama haiko tena salama kwake kufanya vile. (Mez. 22:3) Zaidi ya ile kama bengine banakuambia kama biko na wasiwasi juu ya namna yako ya kutembeza, ukuwe tayari kusikiliza, ile pia itaonyesha kama uko na kiasi.—Linganisha na 2 Samweli 21:15-17.
Epuka hatia ya damu (Kum. 22:8) Gari ni silaha hatari, kama mutu hatembeze muzuri anaweza kuumiza ao hata kuua mutu. Njo maana kama mutu anaendelea kutembeza na japo haiko tena natembeza muzuri sawa zamani, anaweza kutia maisha yake mu hatari na hata maisha ya bengine. Na kama anafanya aksida na mutu anakufa mu ile aksida, anaweza kuwa na hatia ya damu.
Kama inaomba uamue kuacha kutembeza, usiwaze kama ile itafanya bengine basikuheshimie tena ao itaonyesha kama hauko tena wa maana. Yehova anakupenda juu uko na sifa za muzuri. Kwa mufano uko na kiasi, uko munyenyekevu, na unahangaikia usalama wa bengine. Na Yehova anaahidi kama atakutegemeza na kukufariji. (Isa. 46:4) Hatakuacha hata kidogo. Kwa hiyo umuombe akusaidie utumikishe hekima yenye kutenda na kanuni za Biblia juu uweze kuamua ikiwa inaomba uache kutembeza.
a Juu ya kupata habari zaidi ona habari “Aksidenti za Magari Je, U Salama?” mu Amuka! ya tarehe 22 Mwezi wa 8, 2002.