Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w25 Mwezi wa 11 uku. 10-15
  • Uendelee Kuwa na Furaha Wakati Uko Nahangaikia Mupendwa Wako

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Uendelee Kuwa na Furaha Wakati Uko Nahangaikia Mupendwa Wako
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • JUU YA NINI INAWEZA KUWA NGUVU KUENDELEA KUWA NA FURAHA?
  • NAMNA YA KUENDELEA KUWA NA FURAHA
  • NAMNA BENGINE BANAWEZA KUSAIDIA
  • Uendelee Kuwa na Furaha mu Wakati wa Buzee
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
  • Yehova Anaweza Kutusaidia Tukuwe na Furaha ya Kweli
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
  • Utafute Majibu ya hii Maulizo
    Programu ya Mukusanyiko wa Muzunguko wa 2025-2026 Pamoja na Mwangalizi wa Muzunguko
  • Namna ya Kuwatunza Watu Wenye Kuzeeka
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
w25 Mwezi wa 11 uku. 10-15

HABARI YA KUJIFUNZA YA 45

WIMBO 111 Mambo Yenye Kufanya Tukuwe na Furaha

Uendelee Kuwa na Furaha Wakati Uko Nahangaikia Mupendwa Wako

“Wale wenye kupanda mbegu kwa machozi watavuna kwa vigelegele vya shangwe.”—ZB. 126:5.

WAZO KUBWA

Namna benye kuhangaikia bapendwa yabo banaweza kuvumilia magumu yenye banapambana nayo na kuendelea kuwa na furaha.

1-2. Yehova anaona namna gani bale benye kuhangaikia bapendwa yabo? (Mezali 19:17) (Ona pia picha.)

NDUGU Jin-yeol wa Korea anasema hivi: “Tulishafanya zaidi ya miaka 32 tangu tuoane na bibi yangu. Kwa miaka tano yenye imepita, niko namuhangaikia juu iko na ugonjwa wa Parkinson wenye unafanya ikuwe nguvu kwake kujitikisa. Ninapendaka sana bibi yangu, na ninafurahia kumuhangaikia. Kila busiku, analalaka ku kitanda fulani ya bagonjwa yenye iko mu nyumba yetu. Ninalalaka pembeni yake na tunakamatana mikono.”

2 Uko nahangaikia mutu fulani mwenye unapendaka, sawa vile muzazi, bibi ao bwana yako, mutoto wako, ao rafiki? Kama ni vile, bila shaka unafurahia sana kumuhangaikia juu unamupenda. Na juu uko namuhangaikia, unaonyesha pia kama unamupenda Yehova. (1 Ti. 5:4, 8; Yak. 1:27) Lakini, inawezekana mara mingi unavumiliaka magumu yenye bengine habaonake. Wakati fulani, unaweza kuona sawa vile hakuna mwenye anaelewa magumu yenye uko nayo. Pengine unachekaka saa uko na batu, lakini saa uko weye peke unaliaka juu ya huzuni. (Zb. 6:6) Lakini, ujue kama hata kama bengine habajue magumu yenye uko napambana nayo, Yehova yeye anaijua. (Linganisha na Kutoka 3:7.) Yehova anaona machozi yako na namna uko najiima. (Zb. 56:8; 126:5) Anaona pia mambo yote yenye uko nafanya juu ya kuhangaikia mupendwa wako na anaiona kuwa ya maana. Ni sawa vile uko namukopesha Yehova na anaahidi kama atakulipa.—Soma Mezali 19:17.

Picha: Batu mbalimbali biko nahangaikia bapendwa yabo. 1. Dada iko nakulisha mama yake mwenye kuzeeka mwenye hawezi kutoka ku kitanda. 2. Dada iko nasaidia bwana yake mwenye iko mu kinga ya bilema, kuvala biato. 3. Mama anavalisha mutoto kaske ya kumulinda mbele acheze kabumbu na baba yake. 4. Ndugu anatembelea ndugu mwenye kuzeeka na anasali pamoya naye.

Uko nahangaikia mupendwa wako? (Ona fungu ya 2)


3. Inawezekana Abrahamu na Sara balipambana na magumu gani wakati balikuwa nahangaikia Tera?

3 Mu Biblia muko habari za mingi za banaume na banamuke benye balihangaikiaka bapendwa yabo. Tuone mufano wa Abrahamu na Sara. Wakati balitoka Uru, baba yabo Tera alikuwa na miaka 200 hivi. Lakini, alienda pamoya nabo. Balifanya safari ya kilometre 960 hivi kutoka Uru kuenda Harani. (Mwa. 11:31, 32) Bila shaka Abrahamu na Sara balimupenda Tera. Lakini waza kidogo: Inawezekana balikuwa nasafiri ku ngamia ao ku punda, na ile ingekuwa nguvu sana kwa Tera juu alikuwa alishazeeka. Kwa hiyo, inawezekana Abrahamu na sara balifanya mambo mingi juu ya kumuhangaikia na pengine ile ilifanya wakati fulani bachoke sana. Kwa kweli, haikukuwa mwepesi kwabo kumuhangaikia Tera, zaidi sana wakati balikuwa nasafiri. Lakini, Yehova alibapatia nguvu yenye balikuwa nayo lazima. Kwa hiyo, sawa vile tu Yehova alisaidia Abrahamu na Sara, atakusaidia na kukutia nguvu weye pia.—Zb. 55:22.

4. Tutazungumuzia nini mu hii habari?

4 Itakuwa mwepesi kwako kuendelea kuhangaikia mupendwa wako kama uko na furaha. (Mez. 15:13) Kumbuka kama unaweza kuendelea kuwa na furaha hata kama uko na magumu. (Yak. 1:2, 3) Sasa utafanya nini juu uendelee kuwa na furaha? Kitu moya yenye unaweza kufanya ni kuendelea kusali kwa Yehova na kumuomba akusaidie upate sababu za kuendelea kuwa na furaha. Mu hii habari, tutazungumuzia mambo ingine yenye mutu mwenye iko nahangaikia mupendwa wake anaweza kufanya juu aendelee kuwa na furaha. Tutazungumuzia pia mambo yenye bengine banaweza kufanya juu ya kumusaidia. Lakini tuone kwanza juu ya nini mutu mwenye iko nahangaikia mupendwa wake anapaswa kuendelea kuwa na furaha, na mambo yenye inaweza kufanya apoteze furaha yake.

JUU YA NINI INAWEZA KUWA NGUVU KUENDELEA KUWA NA FURAHA?

5. Juu ya nini mutu mwenye iko nahangaikia mupendwa wake anapaswa kuendelea kuwa na furaha?

5 Kama mutu mwenye iko nahangaikia mupendwa wake anapoteza furaha, inaweza kuwa mwepesi kwake kuchoka. (Mez. 24:10) Na wakati anachoka, itakuwa nguvu kwake kutendea mupendwa wake kwa upendo na kumusaidia sawa vile angependa kufanya. Ni mambo gani inaweza kufanya mutu mwenye iko nahangaikia mupendwa wake apoteze furaha?

6. Juu ya nini mutu mwenye iko nahangaikia mupendwa wake anaweza kuchoka sana?

6 Mutu mwenye iko nahangaikia mupendwa wake anaweza kuchoka sana. Dada mwenye jina yake Lea anasema hivi: “Hata siku yenye mambo iliendeka muzuri, mwisho wa siku ninasikiaka tu nguvu inaniisha. Wakati fulani, siwezake hata kujibia ujumbe wenye mutu ananiandikia.” Mutu mwenye iko nahangaikia mupendwa wake anakuwaka na lazima ya kupumuzika. Lakini ni nguvu kwa bamoya kupata wakati ya kupumuzika ao kulala vya kutosha. Dada mwenye jina yake Inés anasema hivi: “Inakuwaka nguvu kwangu kulala vya kutosha. Busiku ninalamukaka kisha kila saa mbili juu ya kuhangaikia mama yangu mukwe. Kwa miaka mingi, miye na bwana yangu hatuyapata hata nafasi ya kupumuzika.” Mutu mwenye iko nahangaikia mupendwa wake anaweza kukatala mualiko wa kuenda kujifurahisha pamoya na barafiki. Pia anaweza hata kukatala migao fulani mu tengenezo ya Yehova, juu inaomba akuwe pale wakati wote ili kuhangaikia mupendwa wake. Ile inaweza kufanya ajisikie kuwa peke yake na ajisikie sawa vile anabanwa na hawezi kufanya byenye anapenda.

7. Juu ya nini mutu mwenye iko nahangaikia mupendwa wake anaweza kujihukumu ao kuhuzunika?

7 Mutu mwenye iko nahangaikia mupendwa wake anaweza kujihukumu ao kusikia huzuni. Dada mwenye jina yake Jessica anasema hivi: “Ninaonaka sawa vile byenye niko nafanya habitoshe na ninajisikiaka mubaya wakati ninakamata wakati wa kupumuzika.” Batu fulani benye kuhangaikia bapendwa yabo banaweza kuona kama byenye biko nafanya ni bya kidogo, bangependa kufanya mambo mingi zaidi. Na wakati fulani banaweza kuona kama habataweza kuendelea kuhangaikia ule mutu. Na pengine wakati fulani saa balikuwa balishachoka, balisema ao kufanya jambo yenye haikufurahisha mupendwa wabo. Ile yote inaweza kufanya bajisikie mubaya sana. (Yak. 3:2) Bamoya banaweza kuhuzunika sana kuona afya ya mupendwa wabo iko naharibika zaidi na zaidi. Dada mwenye jina yake Barbara anasema hivi: “Jambo yenye inanihuzunishaka sana ni kuona vile hali ya rafiki yangu mwenye alikuwaka na nguvu, iko naharibika zaidi na zaidi kila siku.”

8. Leta mufano wenye unaonyesha namna maneno ya shukrani inagusaka moyo mutu mwenye kuhangaikia mupendwa wake.

8 Mutu mwenye iko nahangaikia mupendwa wake anaweza kuona kama bengine habana shukrani juu ya mambo yenye iko nafanya. Juu ya nini? Juu pengine bengine habazoee kumushukuru ao kumupongeza juu ya kazi ya nguvu yenye iko nafanya na juu ya mambo yenye iko najiima. Kwa hiyo tumushukuru juu ya mambo yenye iko nafanya; hata maneno ya kidogo tu inaweza kumutia moyo sana. (1 Te. 5:18) Dada mwenye jina yake Melissa anasema hivi: “Wakati fulani ninaliaka juu nishachoka sana ao kuvunjika moyo. Lakini wakati benye niko nahangaikia bananiambia, ‘Aksanti sana kwa yote yenye uko nafanya,’ ile inanitiaka moyo sana! Ile maneno inanisaidiaka nilamuke siku ya kufuata na niko na hamu ya kubahangaikia tena.” Ndugu mwenye jina yake Ahmadu anaeleza namna maneno ya shukrani inamutiaka moyo sana. Yeye na bibi yake banahangaikiaka mutoto wa ndugu yabo. Ule mutoto anaishi nabo na iko na ugonjwa wa kifafa. Ahmadu anasema hivi: “Hata kama haelewe muzuri mambo yote yenye tunafanyaka juu ya kumuhangaikia, inatugusaka sana moyo wakati anatuonyesha shukrani ao wakati anajikaza kutuandikia maneno ‘Ninabapenda.’”

NAMNA YA KUENDELEA KUWA NA FURAHA

9. Namna gani mutu mwenye iko nahangaikia mupendwa wake anaweza kuwa na kiasi?

9 Ukuwe na kiasi. (Mez. 11:2) Nguvu yetu na wakati yetu siye bote inakuwaka na mipaka. Njo maana ni muzuri na weye ujitilie mipaka juu ya mambo yenye unaweza kufanya na yenye hauwezi kufanya. Na wakati fulani inaomba kusema, “hapana,” kama unaona hautaweza kufanya jambo fulani! Ile inaonyesha kama uko na kiasi. Na kama bengine banasema kama batakusaidia, ukuwe tayari kuitika. Ndugu mwenye jina yake Jay anasema hivi: “Kila siku tunaweza tu kufanya mambo yenye uwezo wetu na wakati yetu inaturuhusu kufanya. Kama tunaelewa mipaka yetu na hatujaribu kufanya byenye binapita uwezo wetu, tutaendelea kuwa na furaha.”

10. Juu ya nini ni jambo ya maana mutu mwenye iko nahangaikia mupendwa wake akuwe na utambuzi? (Mezali 19:11)

10 Ukuwe na utambuzi. (Soma Mezali 19:11.) Kama uko na utambuzi itakuwa mwepesi kwako kubakia mwenye kutulia wakati mupendwa wako anasema ao anafanya jambo yenye haikufurahishe. Mutu mwenye iko na utambuzi anajikaza kuelewa juu ya nini mutu mwingine anatenda mu njia fulani. Ugonjwa fulani unaweza kufanya mutu afanye mambo yenye hangefanya kama hangekuwa na ule ugonjwa. (Muh. 7:7) Kwa mufano, mutu mwenye kwa kawaida anazungumuzaka kwa upendo na kutendeana kwa upole, anaweza kuwa mutu wa kubishana-bishana ao anaweza penda bengine bamufanyie byote byenye anapenda. Anaweza pia kuwa mutu wa kunungunika-nungunika, wa mihali-mihali, ao mutu mwenye hatoshekake, hata ufanye nini hafurahi. Njo maana kama uko nahangaikia mutu mwenye iko na ugonjwa fulani wa nguvu, inaweza kuwa muzuri ujikaze kuelewa muzuri ile ugonjwa. Kuelewa ugonjwa wake kutakusaidia utambue kama hakuwake vile, ni ugonjwa njo unafanya atende vile.—Mez. 14:29.

11. Mutu mwenye iko nahangaikia mupendwa wake anapaswa kupanga wakati wa kufanya mambo gani ya maana kila siku? (Zaburi 132:4, 5)

11 Panga wakati wa kutia nguvu urafiki wako pamoya na Yehova. Mara kwa mara, itaomba upange wakati wa kufanya mambo ingine ya “maana zaidi.” (Flp. 1:10) Kutia nguvu urafiki wako pamoya na Yehova ni kati ya mambo ya maana zaidi. Mufalme Daudi alitia ibada ya Yehova fasi ya kwanza mu maisha yake. (Soma Zaburi 132:4, 5.) Sawa Mufalme Daudi, ni jambo ya maana na weye upange wakati kila siku juu ya kusoma Biblia na kusali. Dada mwenye jina yake Elisha anasema hivi: “Kusali na kutafakari juu ya zaburi zenye kufariji kunanisaidiaka niendelee kuwa na furaha. Ninapendaka sana kusali, juu sala inanisaidiaka sana. Ninakuwaka nasali kwa Yehova mara mingi ku siku na iIe inanisaidiaka nibakie mwenye kutulia.”

12. Juu ya nini ni muzuri mutu mwenye iko nahangaikia mupendwa wake ajikaze kuhangaikia afya yake?

12 Ujikaze kuhangaikia afya yako. Mutu mwenye iko nahangaikia mupendwa wake anaweza kukosa wakati wa kufanya mambo yenye itamusaidia akuwe na afya ya muzuri. Kwa hiyo, hata kama hauna wakati ya mingi ni muzuri uzoee kula chakula yenye kujenga mwili na kufanya mazoezi, juu ile itakusaidia ukuwe na afya ya muzuri na uepuke mahangaiko. (Efe. 5:15, 16) Zaidi ya ile, ulale vya kutosha. (Muh. 4:6) Uchunguzi unaonyesha kama kulala kunasaidiaka ubongo wetu utumike muzuri. Habari moya ya kinganga inasema kama kulala vya kutosha kunapunguzaka mahangaiko na kunasaidiaka mutu abakie mwenye kutulia hata mu hali za nguvu. Ni muzuri pia upange wakati wa kujifurahisha. (Muh. 8:15) Dada moya mwenye anahangaikiaka mupendwa wake anasema jambo yenye inamusaidiaka aendelee kuwa na furaha. Anasema hivi: “Wakati hali ya hewa iko muzuri, ninatokaka inje na kuota kajua. Na hata mara moya ku mwezi, ninapangaka wakati wa kujifurahisha pamoya na rafiki.”

13. Juu ya nini ni muzuri kucheka? (Mezali 17:22)

13 Ukuwe nacheka. (Soma Mezali 17:22; Muh. 3:1, 4) Kucheka kunapunguzaka mahangaiko. Wakati uko nahangaikia mutu, mara mingi mambo haiendekake vile ulipanga. Lakini kama unajikaza kucheka wakati mambo haiendeke muzuri, ile mambo haitakuhuzunisha sana. Na kucheka pamoya na mutu mwenye uko nahangaikia kunaweza kutia nguvu uhusiano wenu.

14. Kuzungumuza na rafiki muzuri kunaweza kukusaidia namna gani?

14 Zungumuza na rafiki yako wa karibu. Hata kama unajikaza sana juu uendelee kuwa na furaha, wakati fulani utakuwa tu na mahangaiko. Wakati ya vile ni muzuri uzungumuze na rafiki muzuri, mwenye atakuelewa na hatafanya ujisikie mubaya. (Mez. 17:17) Umuelezee vile uko najisikia. Atakusikiliza na kukutia moyo, na pengine ile njo uko nayo lazima juu ukuwe tena na furaha.—Mez. 12:25.

15. Namna gani kuzungumuza juu ya Paradiso kunaweza kukuletea furaha?

15 Wazia maisha yenu mu Paradiso. Ujikaze kukumbuka kama kazi ya kuhangaikia mupendwa wako ni ya wakati kidogo tu, haiko ya milele; ile haiko kazi yenye Yehova alikusudia tukuwe nafanya. (2 Ko. 4:16-18) “Uzima wa kwelikweli” wenye Yehova anapenda tukuwe nao, uko mbele yetu. (1 Ti. 6:19) Kuzungumuza na mupendwa wako juu ya mambo yenye mutafanya mu paradiso kunaweza kukuletea furaha. (Isa. 33:24; 65:21) Dada mwenye jina yake Heather anasema hivi: “Mara mingi ninaambiaka benye niko nahangaikia kama karibuni tutashona pamoya, tutakimbia pamoya, tutatembeza kinga pamoya, na tutapiga chakula pamoya kwa ajili ya bapendwa betu benye batafufuliwa. Na kisha kuzungumuzia ile mambo tunamushukuru Yehova pamoya juu ya tumaini yetu.”

NAMNA BENGINE BANAWEZA KUSAIDIA

16. Tunaweza kufanya nini mu kutaniko juu ya kusaidia mutu mwenye iko nahangaikia mupendwa wake? (Ona pia picha.)

16 Usaidie mutu mwenye iko nahangaikia mupendwa wake juu apate wakati wa kufanya bingine. Ndugu na dada mu kutaniko banaweza kujitolea kupitisha wakati pamoya na mutu mwenye iko nahangaikiwa. Ile inaweza kusaidia mwenye anamuhangaikiaka apumuzike, na apate wakati wa kujihangaikia. (Gal. 6:2) Bahubiri fulani bamefanya programe juu ya kujua nani njo ataenda kusaidia kila juma. Dada mwenye kuitwa Natalya anahangaikiaka bwana yake mwenye kupooza, anasema hivi: “Ndugu fulani wa mu kutaniko yetu anakuyaka kwetu mara moya ao mara mbili ku juma juu ya kupitisha wakati pamoya na bwana yangu. Banahubiriaka pamoya, banaongeaka, na hata kuangalia mafilme pamoya. Bwana yangu anafurahiaka sana ile wakati na inanisaidiaka na miye nipate wakati wa kujihangaikia; kwa mufano ninaendaka kutembea kidogo.” Wakati fulani, unaweza kujitolea kubakia busiku pamoya na mutu mwenye iko na lazima ya kuhangaikiwa, juu mwenye anamuhangaikiaka alale vya kutosha.

Badada bawili banatembelea dada mwenye kuzeeka. Mwenye anamuchungaka anabapepea kwa furaha wakati iko naenda inje.

Unaweza kufanya nini juu ya kusaidia ndugu ao dada wa mu kutaniko yenu mwenye iko nahangaikia mupendwa wake? (Ona fungu ya 16)a


17. Wakati wa mikutano, namna gani tunaweza kusaidia mutu mwenye anahangaikiaka mupendwa wake?

17 Wakati wa mikutano, usaidie mutu mwenye iko nahangaikia mupendwa wake. Inaweza kuwa nguvu kwa mutu kufuata muzuri mafundisho ku mikutano ya kutaniko na ku mikusanyiko juu iko nahangaikia mupendwa wake wakati programe iko naendelea. Bandugu na badada mu kutaniko banaweza kujitolea kuikala pembeni ya mutu mwenye iko na lazima ya kuhangaikiwa, ikuwe wakati wa mikutano yote ao mu sehemu fulani ya mikutano. Kama ule mutu hawezi kutoka ku nyumba, ndugu ao dada anaweza kujitolea kuenda kwake juu ya kufuata pamoya naye mikutano kupitia vidéoconférence, juu mwenye anamuhangaikiaka aende ku Jumba ya Ufalme.

18. Tunaweza kufanya nini ingine kwa ajili ya bale benye kuhangaikia bapendwa yabo?

18 Pongeza mutu mwenye iko nahangaikia mupendwa wake na usali naye. Ni muzuri bazee bakuwe natembelea kwa ukawaida bale benye biko nahangaikia bapendwa yabo, juu ya kuenda kubatia moyo. (Mez. 27:23) Na siye bote mu kutaniko, hata tukuwe mu hali gani, tuzoee kupongeza benye biko nahangaikia bapendwa yabo. Tena tuombe Yehova aendelee kubapatia nguvu na kubasaidia baendelee kuwa na furaha.—2 Ko. 1:11.

19. Uko nangoya nini kwa hamu?

19 Hivi karibuni, Yehova atamaliza mambo yote yenye kutuletea maumivu na machozi. Magonjwa na kifo habitakuwa tena. (Ufu. 21:3, 4) “Kilema wa miguu ataruka-ruka kama paa.” (Isa. 35:5, 6) Matokeo ya mubaya ya buzee na maumivu ya kuhangaikia mupendwa mwenye iko mugonjwa itakuwa kati ya “mambo ya zamani [yenye] hayatakumbukwa.” (Isa. 65:17) Lakini mbele ile mambo ifike, Yehova hatatuachilia. Kama tunaendelea kumuomba atupatie nguvu, atatusaidia ‘tuvumilie kwa ukamili kwa subira na furaha.’—Kol. 1:11.

UTAJIBU NAMNA GANI?

  • Nini njo inaweza kufanya mutu mwenye iko nahangaikia mupendwa wake apoteze furaha?

  • Mutu mwenye iko nahangaikia mupendwa wake anaweza kufanya nini juu aendelee kuwa na furaha?

  • Unaweza kufanya nini juu ya kusaidia ndugu ao dada wa mu kutaniko yenu mwenye iko nahangaikia mupendwa wake?

WIMBO 155 Furaha Yetu ya Milele Inatoka kwa Yehova

a MAFASIRIO YA PICHA: Badada bawili banaenda kutembelea dada mwenye kuzeeka juu mwenye anamuhangaikiaka apate wakati wa kuenda kutembea kidogo.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2026)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine