Benye Kuzeeka, Muko ba Maana Sana mu Kutaniko
“Ninashangalaka sana wakati ninafikiria mambo yenye nilikuwa na uwezo wa kufanya wakati nilikuwa kijana. Lakini leo nilishazeeka na siwezi kufanya mambo mingi sawa zamani.”—Connie, mwenye iko na miaka 83.
Pengine na weye hauwezi kufanya mambo mingi sawa zamani juu ya buzee. Hata kama ulishamutumikia Yehova kwa uaminifu kwa miaka mingi, unaweza kuvunjika moyo juu hali yako haikuruhusu tena kufanya mambo mingi. Kwa mufano unaweza kuanza kulinganisha mambo yenye uko nafanya leo na yenye ulikuwaka nafanya zamani. Kama ni vile unaweza kufanya nini juu uendelee kuwa na furaha?
Yehova Anakuomba Ufanye Nini?
Ujiulize hivi, ‘Yehova ananiomba nifanye nini?’ Maneno yenye kuwa mu Kumbukumbu la Torati 6:5, inaweza kukufariji. Ile andiko inasema hivi: “Unapaswa kumupenda Yehova Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa nafsi yako yote na kwa nguvu zako zote.”
Ile andiko inaonyesha kama Yehova anakuomba umutumikie kwa moyo wako wote, kwa nafsi yako yote, na kwa nguvu zako zote. Ile inaweza kukusaidia uepuke kujilinganisha na bengine, ao kulinganisha mambo yenye unaweza kufanya leo na mambo yenye ulikuwaka na uwezo wa kufanya zamani.
Waza kidogo: Wakati ulikuwa kijana, ulikuwa namutumikia Yehova namna gani? Inawezekana ulikuwa namutumikia kwa uwezo wako wote kulingana na hali yako ya ile wakati. Hata vile ungali namutumikia Yehova kwa uwezo wako wote kulingana na hali yako ya leo. Kama unaelewa ile, utaona kama uko namutumikia Yehova sawa tu zamani. Ulikuwa namutumikia kwa uwezo wako wote zamani na uko unafanya vile leo.
Ulimutumikia Yehova kwa uwezo wako wote wakati ulikuwa kijana, na uko namutumikia kwa uwezo wako wote mu buzee
UNAWEZA KUSAIDIA SANA BENGINE
Jambo ingine yenye inaweza kukusaidia ni hii: Kuliko tu kufikiria mambo yenye hauwezi tena kufanya, fikiria nafasi zenye uko nazo za kusaidia bengine. Juu uko Mukristo mwenye kuzeeka, kuko mambo yenye unaweza kufanya leo yenye haungeweza kufanya wakati ulikuwa kijana. Kwa mufano unaweza kufanya mambo yenye kufuata:
Kuelezea bengine mambo yenye umejifunza mu maisha. Fikiria maneno ya batu benye kufuata benye kuzungumuziwa mu Biblia:
Mufalme Daudi: “Nilikuwa kijana na sasa nimezeeka, lakini sijamuona mutu yeyote mwenye haki akiwa ameachwa, wala watoto wake wakitafuta mukate.”—Zb. 37:25.
Yoshua: “Sasa muangalie! Ninakaribia kufa, na munajua muzuri kwa moyo wenu wote na kwa nafsi yenu yote kwamba hakuna hata neno moja lenye halikutimia kati ya ahadi zote za muzuri zenye Yehova Mungu wenu aliwaahidi. Yote yametimia kwa ajili yenu. Hakuna hata neno moja kati ya maneno hayo lenye halikutimia.”—Yos. 23:14.
Pengine na weye umesema maneno ya vile. Maneno ya Daudi na Yoshua inahusu mambo yenye balijionea mu maisha. Ile maneno ilikuwa na buzito juu ni mambo yenye balijionea na kusikia kwa miaka mingi.
Kama na weye umemutumikia Yehova kwa miaka mingi, unaweza kuelezea bengine baraka za Yehova zenye umejionea. Unakumbuka wakati wenye ulijionea namna Yehova alisaidia batu yake mu njia ya pekee? Kama ni vile, ujisikie huru kuelezea bengine! Ile inaweza kubasaidia, pengine umejionea namna kufanya vile kunasaidia bengine. Kwa hiyo, wakati bengine banasikia vile umemutumikia Yehova kwa uaminifu kwa miaka mingi ile inaweza kubatia moyo.—Ro. 1:11, 12.
Jambo ingine yenye unaweza kufanya juu ya kutia bengine moyo ni kuenda ku mikutano ku Jumba ya Ufalme, kama hali yako inaruhusu. Kama unafanya vile, utapata faida na pia Bakristo benzako. Connie, mwenye tulishataya, anasema hivi: “Kuenda ku mikutano ku Jumba ya Ufalme kunanisaidia nisivunjike moyo. Ku Jumba ya Ufalme bandugu na dada bananionyeshaka upendo ya mingi. Ile inanisaidiaka nisivunjike moyo. Ninajikazaka kuonyesha shukrani yangu kwa kubapatia zawadi za kidogo-kidogo. Na ninajikazaka kufanya mambo ya kiroho pamoya na bandugu na badada.”
YEHOVA ANAFURAHIA MAMBO YOTE YENYE UKO UNAMUFANYIA
Mu Biblia muko mifano ya batu ba mingi benye habakuweza kufanya mambo mingi sababu ya hali yabo, lakini Yehova alibapenda. Fikiria mufano wa Simeoni Mwisraeli mwenye kuzeeka mwenye aliishi mu kipindi yenye Yesu alizaliwa. Wakati Simeoni alikuwa naenda ku hekalu, pengine aliona vijana wako nafanya kazi mbalimbali za maana ku hekalu na pengine alijiona kama haiko tena wa maana juu hangeweza kumutumikia Yehova sawa vile wale vijana. Lakini Yehova alikuwa na mawazo tofauti. Alimuona Simeoni kuwa “mwenye haki na mwenye kumuogopa Mungu” na alimubariki kwa kumupatia pendeleo ya kumuona mutoto Yesu. Na hata Yehova alimutumikisha juu ya kutoa unabii juu ya Masiya mwenye angekuya! (Lu. 2:25-35) Wakati Yehova aliangalia Simeoni hakuona tu mwanaume mwenye hana nguvu tena juu ya buzee, lakini aliona mwanaume mwenye imani yenye nguvu, “na roho takatifu ilikuwa juu yake.”
Yehova alimubariki Simeoni kwa kumupatia pendeleo ya kuona mutoto Yesu na kutabiri kama Yesu njo angekuwa Masiya
Na weye unaweza kuwa hakika kama Yehova anaona vile uko unamutumikia kwa uaminifu hata kama kuko mambo yenye hauwezi tena kufanya. Kwa Yehova, zabihu “inakubaliwa zaidi kulingana na kile chenye mutu iko nacho, haiko kulingana na kile chenye mutu hana.”—2 Ko. 8:12.
Kwa hiyo, kazia akili mambo yenye unaweza kufanya. Kwa mufano fikiria aina mbalimbali ya mahubiri yenye unaweza kufanya, hata kama ni kwa wakati kidogo tu. Pia, unaweza kutia moyo bandugu na badada yako kwa kubaita ku telefone ao kubaandikia maneno fulani yenye kutia moyo. Matendo ya kidogo-kidogo yenye upendo inaweza kugusa sana bandugu na badada, zaidi sana kama inatoka kwa mutu mwenye amemutumikia Yehova kwa miaka mingi.
Ndugu na dada benye kuzeeka, hata kama mwili yenu haibaruhusu tena kufanya mambo fulani, Yehova anaweza kuendelea kubatumikisha juu ya kufanya mambo ya mingi. Ona mufano wa dada fulani wa mu Afrika ya Mashariki wenye kuwa mu kisanduku “Alisaidia Kuokoa Uzima wa Mutu.”
Kumbuka kama imani yako na uaminifu wako wa miaka mingi unaweza kutia moyo bengine. Uko mufano muzuri wa uvumilivu, na unaweza kuwa hakika kama ‘Mungu hana ukosefu wa haki ili asahau kazi yako na upendo wenye ulionyesha kwa ajili ya jina lake kwa kutumikia na kuendelea kutumikia watakatifu.’—Ebr. 6:10.
ENDELEA KUWA NA MAMBO MINGI YA KUFANYA
Uchunguzi unaonyesha kama batu mingi benye kuzeeka benye banajitoa sana juu ya kusaidia bengine banakuwaka na afya ya muzuri zaidi kimwili na kiakili, na banakuwaka naishi wakati murefu.
Kusema kweli, kufanya mambo ya muzuri hakutamaliza matokeo ya buzee. Ni Ufalme wa Mungu tu njo utamaliza hali yetu ya kutokamilika, ni kusema hakutakuwa tena kuzeeka wala kufa.—Ro. 5:12.
Lakini, mambo yenye uko unafanya hata leo juu ya kumutumikia Yehova, sawa vile kusaidia bengine bafikie kumujua, inakusaidia ukuwe na tumaini yenye nguvu, na inaweza hata kuwa na matokeo ya muzuri juu ya afya yako. Ndugu na dada benye kuzeeka, tunapenda mujue kama Yehova anaona byenye muko namufanyia kuwa bya maana sana, na kama mufano wenu wa imani unatia moyo sana kutaniko.