Unakumbuka?
Umesoma kwa uangalifu magazeti ya Munara wa Mulinzi ya hii mwaka? Kama ni vile, pima kujibia hii maulizo:
Juu ya nini tunamupatia Yehova utukufu?
Tunamupatia Yehova utukufu juu tunamuheshimia sana na tunamupenda sana. Tena tunamupatia utukufu juu tunapenda bengine bamujue.—w25.01, uku. 3.
Kama mutu anatukosea, nini njo inaweza kutusaidia tumusamehe?
Tusifanye sawa vile hakuna kitu. Lakini pia hatupaswe kuendelea kukasirika ao kufikiria mambo yenye alitufanyia, juu ile inaweza kufanya tuendelee kuumia.—w25.02, uku. 15-16.
Mufano wa mwanafunzi Marko unaweza kusaidia namna gani ndugu vijana?
Marko aliitika kwa kupenda mugao wa kutumikia bengine. Hata kama inawezekana hali fulani ilifanya aumie na avunjike moyo, hakuacha kutumikia bengine. Alitia nguvu urafiki wake pamoya na Paulo na pamoya na Bakristo bengine benye kukomala kiroho.—w25.04, uku. 27.
Yesu alimaanisha nini wakati alisali hivi: “Nimewajulisha jina lako”? (Yoh. 17:26)
Banafunzi ya Yesu balikuwa najua jina ya Mungu. Lakini Yesu alibasaidia bajue muzuri zaidi mwenye ile jina. Alibasaidia bajue makusudi yake, kazi zake, na sifa zake.—w25.05, uku. 20-21.
Kama tuko na kiasi tutaitika nini?
Tutaitika kama kuko mambo yenye hatujue. Kwa mufano, hatujue siku na saa yenye mwisho itakuya na hatujue namna Yehova atatenda ile wakati. Tena hatujue mambo yenye inaweza kutokea kesho ao kesho yake. Na hatujue ni kwa kadiri gani Yehova anatujua.—w25.06, uku. 15-18.
Tunaweza kufanya nini juu habari fulani ao hotuba ya watu wote itusaidie?
Tunaweza kujiuliza hivi: ‘Banasema mambo gani juu ya kusaidia batu baamini hii fundisho ya Biblia? Ni mufano gani wa muzuri wenye ninaweza kutumikisha wakati niko nafundisha mutu kweli ya Biblia? Nani anaweza kufurahia hii habari?’—w25.07, uku. 19.
Namna Mungu alitendea Daudi inatufundisha nini juu ya musamaha wake?
Hata kama Daudi alifanya zambi nzito, wakati alitubu kwa moyo wote Yehova alimusamehe. (1 Fa. 9:4, 5) Wakati Mungu anasamehe hapatie mutu malipizi juu ya zambi yake ya zamani ao kumukumbusha ayo tena wakati wenye kuya.—w25.08, uku. 17.
Kama mwanafunzi wa Biblia iko na magumu ya kuelewa fundisho fulani, unaweza kufanya nini?
Kama umefasiria muzuri mwanafunzi wa Biblia kweli fulani ya Biblia lakini iko tu na magumu ya kuielewa, uipite kwanza na upange kuizungumuzia wakati ingine.—w25.09, uku. 24.
Biblia inamaanisha nini wakati inasema kama zambi iko na “nguvu za udanganyifu”? (Ebr. 3:13)
Zambi inaweza kutuchochea tufanye mambo ya mubaya. Inaweza pia kutudanganya na kutufanya tukuwe na mashaka. Kwa mufano inaweza kutufanya tushakie kama Mungu anatupenda.—w25.10, uku. 16.
Ni mambo gani tatu yenye inaweza kutusaidia tusali kwa moyo wote?
(1) Tunaweza kufikiria sifa za Yehova. (2) Tunaweza kufikiria mambo yenye iko natuhangaisha na kuizungumuzia mu sala, kwa mufano kama tuko na lazima ya kusamehe mutu fulani. (3) Tunaweza kufanya sala za murefu. Ile itatusaidia kuambia Yehova mambo yenye kuwa ndani kabisa ya moyo wetu.—w25.10, uku. 19-20.
Tunaweza kufanya nini juu ya kusaidia benye kuzeeka?
Tunaweza kubatembelea ao kubaita ku telefone. Tunaweza kubasindikiza ku hopitale ao tunaweza kufanya nabo aina mbalimbali ya mahubiri.—w25.11, uku. 6-7.
Ni mambo gani inaweza kufanya siku yenu ya ndoa imuletee Yehova utukufu?
Mufuate sheria za serikali. Siku ya ndoa munapaswa kuhakikisha kama mambo yote na pia fete inapitikana mu njia yenye kuheshimika na yenye inaonyesha tunda ya roho ya Mungu. Muvale na kujipamba kwa kiasi na muepuke desturi zenye hazipatane na Maandiko. Muzungumuzie waziwazi mambo yenye itapitikana siku ya ndoa yenu.—w25.12, uku. 21-24.