Jinsi Gani Kutendea Familia Yetu?
1 Wengi wetu tunayo familia ambayo haipatikani katika ukweli. Tungependa kuwaona watu hao ambao ni wapendwa wetu wanajiunga nasi kwenye njia ya uzima! Hangaiko letu kuhusu wakati wao ujao ni kubwa ikiwa inahusu washiriki wa nyumba yetu. Inakuwa labda miaka kwamba tunajaribu kuwachochea kwenye ukweli, lakini hatungepaswa kukata kauli kwamba hali ni isiyo kuwa na tumaini.
2 Hata ikiwa kwamba Yesu alikuwa akihubiri, “ndugu zake walikuwa hawadhihirishi imani katika yeye.” (Yn. 7:5, TUM) Wakati fulani, washiriki wa familia yake walifikiri kwamba alirukwa na akili. (Mk. 3:21) Ingawaje hivyo, Yesu hakuwaona kama watu wenye kupotea. Ndugu zake walifikia kuukubali ukweli. (Mdo. 1:14) Ndugu yake mdogo Yakobo alikuja kuwa nguzo ya kutaniko la Kikristo. (Gal. 1:18, 19; 2:9) Ikiwa tunataka kupata shangwe ya kuona washiriki wa familia yetu wanaukubali ukweli, tusiache kujaribu kuwagusa na habari njema ya Ufalme.
3 Tuwe Wenye Kuburudisha, si Wenye Kusumbua: Watu ambao Yesu alikuwa akiwahubiri walikuwa wakihisi wenye kuburudishwa, si kukasirishwa. (Mt. 11:28, 29) Hakuwa akiwasumbua na mafundisho ambayo hawangepaswa kuelewa. Ikiwa tunataka kuwaburudisha washiriki wa familia yetu na maji ya ukweli, tuwanyweshe na bilauri moja ya maji wakati mmoja, si ndoo ya maji yenye kujaa! Mwangalizi mmoja msafiri alisema: “Wale wanaopata matokeo bora kabisa kwa washiriki wa familia zao ni wale wanaoamsha udadisi (uchunguzaji) wao kwa kutoa ushuhuda kwa mambo madogo madogo.” Kwa namna hiyo, inawezekana hata labda kwamba watu wapinzani wanafikia kuuliza maulizo na kwamba, hatimaye wawe na hamu ya ukweli.—1 Pt 2:2; ona pia 1 Wakorintho 3:1, 2.
4 Wakristo wengi wenye kuoa walitoa ushuhuda wenye matokeo kwa wenzi wao kwa kuacha kichapo fulani wazi kwenye ukurasa unaoweza kuwapendeza. Dada mmoja aliyekuwa akifanya hivyo alijifunza hata na watoto wake kwa jinsi mume wake aweze kuwasikia, akitoa mafasirio ambayo yangeweza kuwa yenye manufaa kwake. Wakati mwingine, alikuwa akimuuliza: “Leo, nimejifunza jambo hili na lile wakati wa funzo langu. Wewe unawazaje?” Hatimaye, mumewe alikubali ukweli.
5 Tuwe Wenye Heshima, si Wasiovumilia: Mhubiri mmoja wa kike alisema kwamba “hata washiriki wa familia wana haki ya kushikilia maoni yao.” Tunapaswa hivyo kuonyesha heshima wakati wanapotoa mawazo yao au kwamba wanatuomba kimakusudi kutokuwazungumzia ukweli. (Muh. 3:7; 1 Pt. 3:15) Huku tukiwaonyesha uvumilivu, upendo, tukijua kuwasikiliza vizuri, tunaweza kuwa haraka kuchukua nafasi za kutoa ushuhuda stadi. Linaweza kuwa jambo lenye manufaa kuonyesha uvumilivu, kama inavyoonyeshwa na kisa cha Mkristo mmoja ambaye, muda wa miaka 20, alistahimili kwa uvumilivu kutendewa vibaya na mke wake ambaye hakuwa akishiriki imani zake. Kwa kuwa alianza kubadilika, alisema: “Ninamshukuru Yehova kama nini kwamba alinisaidia kukuza tunda la roho, ustahimilivu, kwa sababu sasa naweza kuona tokeo: Mke wangu ameanza kutembea katika kijia cha uhai!”
6 Jinsi gani kutendea familia yako? Inawezekana kwamba, kwa msaada wa mwenendo wako mzuri wa Kikristo na kwa sala zako kwa faida yao, “unawavuta kwa Yehova.”—1 Pt. 3:1, 2, nota.