Vijana, Miradi Yenu Ya Kiroho Ni Gani?
1 Yehova anajua kwa kadiri gani kazi yenye kupendeza na miradi inayoweza kufikiwa inachangia kwa furaha. (Ona Mwanzo 1:28; 2:15, 19) Katika siku zetu, anakabidhi watumishi wake kazi ya kuhubiri na kufundisha. Tunao pia mradi wa juu wa kufikia uhai udumuo milele katika Paradiso. Kwa kungoja, tunapaswa kujiwekea miradi ya kiroho yenye kuendelea ikiwa tunataka kutumia vizuri nguvu zetu na mali zetu.—1 Kor. 9:26.
2 Miradi Yenye Kusawazika kwa Vijana: Vijana wangepaswa kuwa na miradi ya kitheokrasi inayopatana na uwezo wao mbalimbali wa kibinafsi. (1 Tim. 4:15) Watoto wadogo walifikia mradi wa kujifunza majina ya vitabu vyote vya Biblia hata kabla ya kujua kusoma. Kwa msaada wa funzo la familia, watoto wanajifunza kutayarisha mikutano katika kusudi la kuweza kutoa majibu yanayofikiriwa vizuri na kujiandikisha kwenye Shule ya Huduma ya Kitheokrasi. Kwa kushindikiza wazazi wao katika mahubiri, wanajifunza kushiriki katika kazi ya ushuhuda na wanafanya maendeleo kwa ajili ya kuwa wahubiri wasiobatizwa. Ni vizuri kwamba wazazi wazungumze kikawaida na watoto wao juu ya mradi wa kujitoa wakfu na wa ubatizo.
3 Ikiwa wewe ni tineja, ni miradi gani ya kiroho unayojiwekea? ‘Mkumbuke Muumba wako Mkuu’ kwa kukaza kikiki uangalifu wako juu ya miradi iliyo hakika ya lazima katika maisha. (Muh. 12:1; Zab. 71:17) Kwa nini kutokuwa painia msaidizi wakati wa mapumziko ya shule? Je! umekwisha kufikiria kuanzisha huduma ya wakati wote kwa kuwa painia wa kawaida? Ungesema nini juu ya kujifunza lugha ya kigeni ili kuweza, baadaye, kutegemeza kikundi au kutaniko la lugha ya kigeni, katika eneo lenu au mahali pengine? Kati ya akina ndugu na dada wanaotumikia kwa sasa Betheli au walio waangalizi wasafiri au wamishonari, wengi walijiwekea mradi wa utumishi wa wakati wote walipokuwa bado shuleni. Kwa nini kutofanya vivyo hivyo?
4 Ninyi mlio katika umri mdogo, jikazeni kuiga mfano wa Yesu. Katika umri wa miaka 12, tayari alikuwa akizungumza kikawaida maswala ya kiroho. (Lk. 2:42-49, 52) Kwa kujiwekea miradi mizuri ambayo itawasukuma kuwa na funzo la kibinafsi, kusoma kila siku Biblia na kutafuta ushirika wa Wakristo wakomavu wakati wa mikutano na mahubiri, mtapata mazoezi yatakayowasaidia kufundisha wengine juu ya Ufalme wa Mungu, kama alivyofanya Yesu.