Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 9/97 uku. 6
  • Tumtegemee Yehova ili ‘Kufululiza Kukuza’

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Tumtegemee Yehova ili ‘Kufululiza Kukuza’
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Namna ya Kutumia Broshua Habari Njema Inayotoka kwa Mungu!
    Huduma Yetu ya Ufalme—2013
  • Tumwige Yehova Kwa Kuhangaikia Kwelikweli Wengine
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Utoaji Uliopendekezwa kwa Ajili ya Utumishi wa Shambani
    Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Tuanzishe Mafunzo ya Biblia Katika Broshua Anataka
    Huduma Yetu ya Ufalme—1999
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1997
km 9/97 uku. 6

Tumtegemee Yehova ili ‘Kufululiza Kukuza’

 1 “[Nilipata] kwa mara ya kwanza shangwe ya kushiriki katika kuunda kutaniko lipya. Hilo liliomba miaka miwili ya kazi yenye bidii, sala na kutumaini katika Yehova, ‘yeye afululizaye kukuza.’” w80 15/4 26 Hivyo ndivyo alivyosema painia mmoja mwenye bidii aliyejifunza umuhimu wa kumtegemea Yehova ili ‘kufululiza kukuza.’ (1 Kor. 3:5-9) Tunapowatafuta watu wanaopendezwa na maulizo ya kiroho, sisi pia tunahitaji tegemeo la Mungu ikiwa tunataka kwamba huduma yetu izae matunda.​—Mit. 3:5, 6.

2 Ni Jambo la Lazima Kulima: Ili kwamba mbegu za ukweli zikomae, inafaa kuzilima. Kumuona tena mtu siku moja au mbili kisha ziara ya kwanza mara nyingi kunazaa matokeo mazuri. Tuwe wenye shauku na urafiki. Tumtie msikilizaji wetu katika hali ya starehe. Tusiwe sisi wenyewe tu ndio wenye kusema. Tumtolee nafasi ya kufahamiana nasi na tuonyeshe kwamba tunapendezwa naye kibinafsi.

 3 Mwezi wote wa Septemba, tutaendelea kama vile mnamo Agosti kutolea broshua mbalimbali. Lakini itatupasa pia kuwaona tena watu walioonyesha kupendezwa au waliokubali broshua. Jinsi gani? Kwa kufanya ziara za kurudia na kwa kutolea mafunzo ya Biblia. (Mt. 28:​19, 20) Kwa hiyo, tutaweza kutumia broshua Anataka na kujisaidia na madokezo manne yafuatayo.

 4 Ikiwa tunazungumza na mtu anayejiuliza ulimwengu unakwenda wapi, tungeweza kurudilia mazungumzo hivi:

◼ “Una wasiwasi bila shaka kama mimi juu ya kuanguka kwa adili ya watu. Tunasikia mambo ya hatari juu ya jeuri ya nyumbani, ninapenda kusema juu ya watoto, wazazi au wenzi wa ndoa wanaonyanyaswa kwa kutendewa vibaya. Kwa upande mwingine, wengi wanaona kuwa jambo la kawaida kusema uongo au kuiba ili kutosheleza tamaa zao. Kulingana nawe, je! yale watu wanayofanyia maisha yao ni yenye maana kwa Mungu? [Tuache mtu ajibu.] Mungu alimwekea mwanadamu kanuni fulani, na kanuni hizo si ngumu kuheshimu.” Tusome 1 Yohana 5:3. Kisha tutolee broshua Anataka na tuifungue kwenye somo 10. Tuvutie uangalifu juu ya mazoea yanayoandikwa katika italiki mwanzoni mwa mafungu 2 mpaka 6, na tumuulize mtu ni zoea gani, machoni pake, linaloumiza zaidi watu. Tusome fungu linalohusika na andiko moja au mawili, kulingana na hali. Tumalize kwa kusoma fungu 7 na tuagane kwa mazungumzo mengine wakati ujao.

 5 Kwa wale wanaohangaikia maisha yao ya familia, tungeweza kusema:

◼ “Kwa maoni yako, je! ni jambo la akili kumtegemea Muumba ili mtu afanikiwe kujenga maisha yake ya familia?” Tuache mtu ajibu. Tufungue broshua Anataka kwenye somo 8 na tufasirie kwamba ina kanuni zinazotokana na Biblia kwa kila mshiriki wa familia. Tuonyeshe jinsi ya kutumia broshua hiyo, kwa kuiambatanisha na Biblia, ili kupatia ndani faida zote. Tufuate maagizo yanayopatikana kwenye ukurasa 2. Tuchukue mipango ili kurudi tena kumaliza somo au, ikiwa somo lilichunguzwa kikamilifu, ili kujifunza somo lingine ambalo mtu alichagua.

 6 Angalia namna ya moja kwa moja ya kutolea funzo la Biblia. Inahusu kuonyesha broshua “Anataka” na kusema:

◼ “Broshua hii ni funzo linalochunguza kwa ujumla mafundisho ya msingi ya Biblia. Kwa kila ukurasa utakuta majibu kwa maulizo yanayowasumbua watu tangu karne nyingi. Kwa mfano: Kusudi la Mungu ni nini kuhusu dunia?” Tujielekeze kwenye somo 5 na tusome maulizo ya mwanzoni. Tumuulize mtu ni ulizo gani linalompendeza zaidi na tusome fungu au mafungu yanayolingana, na pia maandiko yanayopatana. Tumfasirie kwamba anaweza pia kupata kwa vyepesi majibu yenye kutosheleza kwa maulizo mengine. Tumpendekezee kurudi tena ili kuchunguza ulizo lingine.

 7  Tutapendelea labda u­fu­ndi huu ulio mwepesi zaidi ili kuanzisha funzo la Biblia:

◼ “Je! unajua kwamba katika dakika chache tu unaweza kupata jibu kwa ulizo la maana sana la Biblia? Kwa mfano . . . ” Tutaje ulizo moja linalopatikana mwanzoni mwa mojawapo ya masomo ya broshua na kwamba, kulingana nasi, mtu huyo anajiuliza. Ili kupata mawazo ya maulizo, tuone mafungu 15 na 16 ya nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Aprili 1997 yenye kichwa cha habari “Tujipe Ujasiri ili Kufanya Ziara za Kurudia.”

 8 Kushinda kwa shangwe mwito wa kufanya ziara za kurudia na mafunzo ya Biblia ni mojawapo ya utendaji mbalimbali wa “wafanyakazi wenzi” wa Mungu. (1 Kor. 3:​9, TUM) Tujikaze hivyo kukomaza kupendezwa, kisha tumtegemee Mungu ili ‘kukuza.’ Kwa kufanya hivyo, tutapata uradhi wa kwelikweli, ule ambao utendaji mwingine wowote hauwezi kutoa.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine