Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
MNARA WA MLINZI Des. 15
“Wakati huu wa mwaka, wengi wanafikiria kuzaliwa kwa Yesu. Je, ulijua kwamba kuna mambo ya thamani tunayoweza kujifunza kutokana na simulizi la Biblia la kuzaliwa kwake? [Acha mtu ajibu. Kisha onyesha ukurasa wa 5, na soma 2 Timotheo 3:16.] Toleo hili la Mnara wa Mlinzi linazungumzia mengine kati ya mambo hayo.”
Amkeni! Des. 22
“Je, unafikiri kwamba wazazi wana sababu ya kuhangaikia jinsi viburudisho vya leo vyenye jeuri vinavyokuwa na uvutano juu ya watoto wao? [Acha mtu ajibu.] Wazazi wengi hutumia andiko hili la Biblia kuwa mwongozo. [Soma Zaburi 11:5.] Toleo hili la Amkeni! linasaidia familia kuchunguza hatari zinazotokana na michezo ya kompyuta.”
MNARA WA MLINZI Jan. 1
“Watu wanapopoteza mpendwa katika kifo au wanapogonjwa, mara nyingi wanajiuliza, ‘Kwa nini Mungu anaruhusu jambo hili?’ Labda umejiuliza ulizo hilohilo. Biblia inaonyesha kwamba Mungu anawaonea huruma wale wanaoteseka. [Soma Isaya 63:9a.] Gazeti hili linaeleza kwa nini tunaweza kuwa hakika kwamba Mungu atamaliza kuteseka.”
Amkeni! Jan. 8
“Je, unafikiri kwamba serikali inapaswa kuzuia uhuru wa usemi? [Acha mtu ajibu.] Namna gani ikiwa usemi unahusu kuzungumza na wengine kuhusu dini, kama tunavyosoma hapa? [Soma Matendo 28:30, 31.] Hivi karibuni, ulizo hilo lililetwa mbele ya Mahakama Makuu ya Shirikisho la Amerika. Unaalikwa kusoma kuhusu jambo hilo katika toleo hili la Amkeni!”