Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Des. 15
“Wakati huu wa mwaka, watu ulimwenguni pote wanakumbuka kuzaliwa kwa Yesu kwa namna mbalimbali. Je, ulijua kwamba unabii wa Biblia unaonyesha uhusiano uliopo kati ya kuzaliwa kwa Yesu na amani yenye kudumu? [Acha mtu ajibu. Kisha soma Isaya 9:6, 7.] Gazeti hili linaeleza namna amani hiyo itakavyotimizwa.”
Amkeni! Des. 22
“Je, umewahi kuona kwamba watu wanatilia zaidi na zaidi mkazo juu ya sura na umbo? [Acha mtu ajibu.] Gazeti hili linazungumzia hatari fulani fulani za kuhangaikia sana uzuri. Linakazia pia thamani ya aina ya uzuri ulio wa maana zaidi.” Soma 1 Petro 3:3, 4.
Mnara wa Mlinzi Jan. 1
“Dini nyingi zinafundisha kwamba watu wanapaswa kupenda jirani zao. [Soma Mathayo 22:39.] Kwa hiyo, unafikiri kwa nini basi dini inahusika katika vita vingi na mapigano mengi katika ulimwengu? [Acha mtu ajibu.] Toleo hili la Mnara wa Mlinzi linazungumzia ulizo: Je, dini inaweza kuunganisha wanadamu?”
Amkeni! Jan. 8
“Ungewezaje kujibu ulizo hili? [Soma ulizo kwenye jalada. Kisha acha mtu ajibu.] Mali za dunia ni zenye kupungua kwa kiwango chenye kutisha. Lakini, angalia ahadi hii yenye kutia moyo. [Soma Zaburi 104:5.] Toleo hili la Amkeni! linaeleza jinsi dunia yetu inavyokaribia kurekebishwa upya kabisa.”