Chukua Mipango Tangu Sasa ili Kushiriki Zaidi Katika Mahubiri
1. Kwa nini kipindi cha Ukumbusho ni wakati muzuri sana kwetu, na kipindi hicho kinatutolea nafasi ya kuonyesha nini?
1 Kila mwaka, kipindi cha Ukumbusho ni wakati muzuri kabisa kwetu ili ‘kumusifu sana Yehova.’ (Zab. 109:30) Je, utashiriki zaidi katika mahubiri mwezi wa 3 ili kuonyesha shukrani yako kwa Mungu aliyechukua mipango ili zabihu ya ukombozi itolewe? Sasa huu ndio wakati wa kuchukua mipango ili ushiriki zaidi katika mahubiri.—Met. 21:5.
2. Ulijisikia namna gani ilipotangazwa kwamba mupango ulichukuliwa ili painia musaidizi ahubiri saa 30 katika mwezi wa 4 wa mwaka uliopita, na ndugu na dada wengine walijisikia namna gani?
2 Panga Kuwa Painia Musaidizi: Mwaka uliopita ndugu na dada katika makutaniko yote walifurahi sana waliposikia kwamba inawezekana kuwa painia musaidizi katika mwezi wa 4 kwa sababu saa zinazoombwa kwa mapainia wasaidizi zilipunguzwa kipindi hicho. Ndugu mumoja aliandika hivi: “Ningali kwenye masomo ya sekondari, kwa hiyo niliona kwamba siwezi kuwa painia wa kawaida. Lakini nitajaza ombi la painia musaidizi ili nihubiri saa 30 lakini nitajikaza kuhubiri saa 50 katika mwezi wa 4.” Dada mumoja anayefanya kazi ya kimwili kwa saa nyingi alisema hivi: “Saa 30 tu, hilo ni rahisi sana!” Wakati mupango huo ulitangazwa, ndugu mumoja mwenye umri wa miaka 80 hivi, aliyekuwa painia hapo zamani, alisema hivi: “Huu ndio wakati niliokuwa nikingojea! Yehova alijua kwamba kazi ya upainia ndio iliyokuwa kipindi bora katika maisha yangu!” Wengine ambao hawakuweza kufanya upainia walijiwekea miradi ya kuongeza saa wanazopitisha kwa kawaida katika mahubiri.
3. Ni sababu gani zinazotuchochea ili tupange tena kuwa mapainia wasaidizi katika mwezi wa 3, wa 4, na wa 5?
3 Mwezi wa 3 utakuwa mwezi unaofaa kabisa ili kuwa painia musaidizi kwa kuwa tutakuwa tena na pendeleo la kuwa mapainia wasaidizi katika mwezi huo, tunaweza kuamua kuhubiri saa 30 tu ao saa 50. Pia, kuanzia Siku ya Posho, tarehe 17 mwezi wa 3, tutaanza kampanye ya pekee ili kualika watu waje kuhuzuria pamoja nasi Ukumbusho utakaofanywa tarehe 5 mwezi wa 4. Ndugu na dada wengi watafurahia kushiriki zaidi katika mahubiri mwezi wa 4 na wa 5; miezi hiyo saa zinazoombwa kwa mapainia wasaidizi ni 50.
4. Tunaweza kufanya nini ili tuhubiri zaidi katika kipindi cha Ukumbusho, na kwa hiyo tutakuwa na nafasi ya kufanya nini?
4 Wakati wa Ibada yenu ya Familia ya mangaribi, munaweza kuzungumuzia namna kila mumoja katika familia anaweza kushiriki zaidi katika mahubiri katika kipindi hicho cha Ukumbusho. (Met. 15:22) Umuombe Yehova abariki jitihada zako. (1 Yoh. 3:22) Hakika, ukishiriki zaidi katika mahubiri kipindi hicho, utakuwa na nafasi ya kumusifu Yehova sana na pia utakuwa na furaha zaidi.—2 Kor. 9:6.