Ongeza Furaha Yako Katika Kipindi cha Ukumbusho!
1. Tunaweza kufanya nini ili kuongeza furaha yetu katika Mwezi wa 3, wa 4, na wa 5?
1 Ungependa kuongeza furaha yako katika Mwezi wa 3, wa 4, na wa 5? Njia moja ya kufanya hivyo ni kuhubiri zaidi, na ikiwezekana, kuwa painia musaidizi. Namna gani kufanya hivyo kutaongeza furaha yako?
2. Namna gani kuhubiri zaidi kunaongeza furaha yetu?
2 Ongeza Furaha Yako: Yehova alipotuumba alitupa uwezo wa kufurahi na kutosheka tunapomuabudu ili kutimiza mahitaji yetu ya kiroho. (Mt. 5:3) Pia, alitaka tupate furaha inayotokana na roho ya kutoa. (Mdo 20:35) Kazi ya kuhubiri inatupa nafasi ya kumuabudu Mungu na kuwasaidia wengine. Ni wazi kwamba, kuhubiri zaidi kunaletea furaha mingi. Tena, ikiwa unahubiri sana, unaweza kuwa mwenye ufundi zaidi. Kadiri tunakuwa wenye ufundi, tunahubiri tukiwa na uhakika na bila woga. Tutakuwa na nafasi nyingi za kutoa ushahidi na kuanzisha mafunzo ya Biblia. Yote hayo yanafanya kazi ya kuhubiri iwe yenye kuleta furaha zaidi.
3. Sababu gani Mwezi wa 3 na wa 4 ni miezi inayofaa kabisa ili kuwa painia musaidizi?
3 Mwezi wa 3 na wa 4 ni miezi inayofaa kabisa kuwa painia musaidizi kwa sababu tunaweza kuchagua kuhubiri saa 30 ao 50. Pia, kuanzia Siku ya Posho tarehe 22 Mwezi wa 3, mupaka Siku ya Ukumbusho, ni kusema Siku ya Kwanza tarehe 14 Mwezi wa 4, tutafanya kampanye ya kuwaalika watu kwenye Ukumbusho. Makutaniko mengi yatakuwa na furaha zaidi kwa sababu wahubiri wengi watatumika “bega kwa bega” ili kuhubiri sehemu kubwa zaidi ya eneo wakati wa kampanye.—Sef. 3:9.
4. Unaweza kufanya nini ikiwa unataka kuwa painia musaidizi?
4 Jitayarishe Tangu Sasa: Ikiwa haujaanza kujitayarisha, chunguza programu yako na ona mabadiliko unayoweza kufanya ili kuhubiri sana katika mwezi mumoja ao zaidi. Sali kwa ajili ya hilo. (Yak. 1:5) Zungumuza na watu wa familia yako na wengine katika kutaniko kuhusu muradi huo. (Met. 15:22) Utaona kwamba hata ikiwa una matatizo ya afya ao unafanya kazi inayokuchukua wakati wote, wewe pia unaweza kupata furaha inayotokana na kazi ya upainia musaidizi.
5. Tutapata faida gani ikiwa tunahubiri zaidi katika kipindi cha Ukumbusho?
5 Yehova anataka watumishi wake wawe wenye furaha. (Zab. 32:11) Kwa kujikaza kuhubiri zaidi katika kipindi cha Ukumbusho, tutaongeza furaha yetu, na pia tutamufurahisha Baba yetu wa mbinguni.—Met. 23:24; 27:11.