Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 9/15 uku. 2
  • Tuige Imani Yao

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Tuige Imani Yao
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2015
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Barua ya Baraza Lenye Kuongoza
    Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
  • “Kutoa Ushahidi Kamili” Kuhusu Ufalme wa Mungu
    Huduma Yetu ya Ufalme—2011
  • Namna Maandiko Inatupatia Nguvu ya Kuvumilia Magumu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2021
  • Maulizo ya Kujikumbusha ya Sehemu ya 2
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2015
km 9/15 uku. 2

Tuige Imani Yao

1. Kuanzia juma la tarehe 19 Mwezi wa 10, tutajifunza kitabu gani katika Funzo la Biblia la Kutaniko?

1 Kuanzia juma la tarehe 19 Mwezi wa 10, 2015, tutajifunza kitabu Tuige Imani Yao katika Funzo la Biblia la Kutaniko. Kitabu hiki kinazungumuzia wanaume na wanawake 14 wenye kutajwa katika Biblia wenye walionyesha imani. Kinaeleza habari yao kwa njia yenye kutufanya tujisikie kama tuko na watu hao waaminifu, na kinatusaidia kuona kwamba haiko watu wa kuwazia tu, lakini ni watu wa kweli kabisa wenye walipambana na magumu wakati walimutumikia Yehova. Kitabu hiki kinatoa somo mbalimbali ili kutusaidia tuone namna ya kutumikisha mambo hayo katika maisha yetu ya leo.—Ebr. 6:12.

2. Eleza mambo fulani yenye kuwa katika kitabu Tuige Imani Yao.

2 Mambo Fulani Yenye Kuwa Katika Kitabu Hiki: Kitabu hiki kina karte na muchoro wenye kutuonyesha namna matukio yalifuatana ili kutusaidia tujue kama mutu mwenye kutajwa aliishi wapi na wakati gani. Tena, kila sura iko na sehemu yenye kichwa “Mambo ya Kukumbuka . . . ,” ili kutusaidia tufikiri sana juu ya habari hiyo na kutumikisha mambo yenye tumejifunza katika sura hiyo. Pia, kitabu hiki kina picha za kupendeza, maelezo madogo-madogo, na michoro mingine yenye kutusaidia tuelewe muzuri zaidi habari.

3. Ni nini itatusaidia kupata faida wakati tutajifunza kitabu Tuige Imani Yao?

3 Nini Itatusaidia Kupata Faida Wakati wa Funzo: Kwenye mwanzo wa kitabu hiki kuna Barua ya Baraza Lenye Kuongoza yenye kututia moyo kwa maneno haya: “Tumia akili yako, uwe kama mwenye kuona na kusikia, kugusa na kunusa mambo unayosoma. Ujisikie kama watu wanaozungumuziwa katika Biblia walivyojisikia.” Kutumia akili yetu hakumaanishe kuwaza mambo yenye haiko katika habari hiyo, lakini kunamaanisha kufikiri sana juu ya mambo yenye habari hiyo yenye kuongozwa na roho inasema na kujitia pa nafasi ya watu wenye kutajwa. Kufanya hivyo kunaomba kuwa na wakati na kufikiri sana. (Neh. 8:8) Kama funzo linaanza katikati ya sura, kiongozi atarudilia mawazo makubwa ya funzo la juma lenye lilipita kwa segonde 30 ao kwa dakika moja. Kama katika sehemu ya kujifunza hakuna sehemu “Mambo ya Kukumbuka . . . ,” kiongozi anaweza kumalizia kwa kuuliza ulizo moja ao mbili

4. Sababu gani ni lazima kujifunza kitabu Tuige Imani Yao?

4 Tunaishi katika ulimwengu wenye unatafuta kila siku kuregeza imani yetu katika njia mbalimbali. Kitabu hiki—na sehemu za Munara wa Mulinzi zenye kitabu hiki kinategemea—ni zawadi kutoka kwa Yehova ili kutia imani yetu nguvu. (Yak. 1:17) Kwa hiyo, ili tupate faida, sisi wote tujikaze sana kuhuzuria kila Funzo la Biblia la Kutaniko na kutoa maelezo wakati wa funzo!

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine