Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • wp22 na. 1 uku. 6-7
  • 1 | Usikuwe na Ubaguzi

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • 1 | Usikuwe na Ubaguzi
  • Munara wa Mulinzi Unatangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti ya Watu Wote)—2022
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Fundisho ya Biblia:
  • Ile Iko na Maana Gani?
  • Mambo Yenye Unaweza Kufanya:
  • 3 | Utoshe Mawazo ya Chuki mu Akili Yako
    Munara wa Mulinzi Unatangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti ya Watu Wote)—2022
  • Namna ya Kuachana na Chuki
    Munara wa Mulinzi Unatangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti ya Watu Wote)—2022
  • Yehova “Hana Ubaguzi”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Juu ya Nini Chuki Iko Naendelea?
    Munara wa Mulinzi Unatangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti ya Watu Wote)—2022
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unatangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti ya Watu Wote)—2022
wp22 na. 1 uku. 6-7
Mwanaume mweusi iko na picha ya muzungu mwenye sura ya kicheko, na mwanamume muzungu iko na picha ya mweusi mwenye iko na sura ya kicheko. Kule nyuma kuko picha ya watu wenye kukasirika.

NAMNA YA KUACHANA NA CHUKI

1 | Usikuwe Na Ubaguzi

Fundisho ya Biblia:

“Mungu hana ubaguzi, lakini katika kila taifa [kila] mutu mwenye anamuogopa na kufanya mambo yenye kuwa sawa anakubaliwa naye.”​—MATENDO 10:34, 35.

Ile Iko na Maana Gani?

Juu ya kuamua kama tuko watu wazuri ao watu wabaya, Yehovaa Mungu haangaliake inchi yetu, rangi yetu ya ngozi, ao desturi yetu. Jambo yenye anaangaliaka ni moyo wetu. Kusema kweli, “mwanadamu bure anaona kile chenye kinaonekana kwa macho, lakini Yehova anaona ndani ya moyo.”​—1 Samweli 16:7.

Mambo Yenye Unaweza Kufanya:

Hata kama hatuwezi kusoma mu mioyo ya watu, tunaweza kujikaza kumuiga Mungu kwa kuepuka kubagua wengine. Epuka kuwa na mawazo fulani juu ya mutu juu tu ni wa inchi fulani, wa rangi fulani ya ngozi, ao wa desturi fulani. Ukiona kama uko na mawazo ya mubaya juu ya watu fulani, pengine juu tu ni wa rangi ingine ya ngozi ao wa inchi ingine, umuombe Mungu akusaidie utoshe ile mawazo mu akili yako. (Zaburi 139:23, 24) Ukimuomba Yehova kwa moyo wote akusaidie uepuke ubaguzi, ukuwe hakika kama atasikiliza sala yako na atakusaidia.​—1 Petro 3:12.

a Yehova ni jina ya pekee ya Mungu.​—Zaburi 83:18.

“Nilikuwa siyaikalaka kwa amani pamoya na muzungu. Sasa nilikuwa mu familia ya kweli ya ndugu na dada wa mu dunia yote.”​—TITUS

Habari ya Kweli​—TITUS

Aliachana na Chuki

Titus.

Titus alikuwaka mu kikundi ya watu wenye jeuri, wenye walichukia sana sheria zenye zilichochea ubaguzi wa rangi ya ngozi. Anasema hivi: “Tulikuwa naenda fasi mbalimbali za mu muji kwenye watu weusi hawakuruhusiwa kufika, sawa vile ku hoteli na fasi za kukunywia pombe, juu tu ya kuanzisha ugomvi.” Titus anasema kama chuki njo ilikuwa namuchochea atende vile. Anasema tena hivi: “Kila mara wakati nilikuwa nabishana na mutu, ikuwe mwanamuke ao mwanaume, miye njo nilikuwa wa kwanza kumupiga.”

Titus alianza kubadilika wakati alianza kujifunza Biblia pamoya na Mashahidi wa Yehova. Mambo yenye alikuwa nasoma mu Biblia ilimusaidia sana. Jambo yenye ilimugusa sana ni ahadi ya Mungu kuhusu mambo yenye atafanya mu siku zenye ziko nakuya. Mungu anasema kama mu siku zenye ziko nakuya “kifo hakitakuwa tena, wala maombolezo wala kilio wala maumivu havitakuwa tena.”​—Ufunuo 21:3, 4.

Ku mwanzo, haikukuwa mwepesi kwa Titus kuacha kuchukia wengine. Anasema hivi: “Ilikuwa nguvu sana kubadilisha mawazo na matendo yangu.” Lakini mambo yenye alijifunza mu Matendo 10:34, 35 ilimusaidia sana. Ile andiko inaonyesha kama Mungu hana ubaguzi.

Ile ilimusaidia namna gani? Titus anasema hivi: “Nilisadiki kabisa kama dini ya Mashahidi wa Yehova njo ya kweli, wakati nilijionea wazi namna wanapendana bila kuangalia kama huyu ni muzungu, ao ni mweusi, ao ni wa rangi gani ya ngozi. Hata mbele nikuwe Shahidi wa Yehova, Mukristo moya muzungu alinialika kwake ili nikule chakula pamoya naye. Nilikuwa siyaikalaka kwa amani pamoya na muzungu. Lakini, ile siku nilienda kwake na nikakula pamoya naye. Kwangu, ile ilikuwa ndoto kabisa. Sasa nilikuwa mu familia ya kweli ya ndugu na dada wa mu dunia yote.”

Ukipenda kujua mambo mingi juu ya Titus, soma Munara wa Mulinzi wa tarehe 1 Mwezi wa 8, 2009, ukurasa wa 28-29.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine