Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w25 Mwezi wa 4 uku. 20-25
  • Hatuko Peke Yetu

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Hatuko Peke Yetu
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • YEHOVA ANATUONGOZA
  • YEHOVA ANATUTIMIZIA MAHITAJI YETU
  • YEHOVA ANATULINDA
  • YEHOVA ANATUFARIJI
  • SIKUZOTE YEHOVA IKO PALE JUU YETU
  • Kumbuka Kama Yehova Ni “Mungu Mwenye Kuishi”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2024
  • Yehova “Anaponyesha Wenye Kuvunjika Moyo”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2024
  • Kutoa Kutakuletea Furaha
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2024
  • Maamuzi Yenye Inaonyesha Kama Tunamutegemea Yehova
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2023
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
w25 Mwezi wa 4 uku. 20-25

HABARI YA KUJIFUNZA YA 17

WIMBO 99 Ndugu na Dada Wote

Hatuko Peke Yetu

“Nitakusaidia.”—ISA. 41:10.

WAZO KUBWA

Namna Yehova anatuhangaikia mu njia ine.

1-2. (a) Juu ya nini tunaweza kusema kama hatuko peke yetu wakati tuko na magumu? (b) Tutazungumuzia nini mu hii habari?

WAKATI tuko na magumu ya nguvu, tunaweza kujisikia sawa vile tuko peke yetu mu mutumbwi ya kidogo mu bahari kubwa yenye upepo mukali. Lakini, hatuko peke yetu. Baba yetu wa mbinguni mwenye upendo anaona magumu yetu, na anaahidi kutusaidia. Anahakikishia hivi kila mutumishi wake muaminifu: “Nitakusaidia.”—Isa. 41:10.

2 Mu hii habari tutaona namna Yehova anatusaidia (1) kwa kutuongoza, (2) kwa kutupatia mambo yenye tuko nayo lazima, (3) kwa kutulinda, na (4) kwa kutufariji. Yehova anatuhakikishia kama hata tupate magumu gani mu maisha, hatatusaabu hata kidogo. Hatatuacha hata siku moya. Kwa hiyo hatuko peke yetu.

YEHOVA ANATUONGOZA

3-4. Yehova anatuongoza namna gani? (Zaburi 48:14)

3 Soma Zaburi 48:14. Yehova anajua kama hatuwezi kujiongoza siye peke. Sasa, namna gani anaongoza waabudu wake waaminifu leo? Kwanza anatumia Biblia. (Zb. 119:105) Kupitia Neno yake yenye iliongozwa na roho yake takatifu, Yehova anatusaidia tukamate maamuzi ya muzuri na tukomalishe sifa zenye zitatusaidia tukuwe na furaha leo, na tupate uzima wa milele wakati wenye kuya.a Kwa mufano, anatushauria tusiendelee kukasirika wakati bengine banatukosea, tukuwe wanyoofu mu mambo yote, na tupende bengine kwa moyo wote. (Zb. 37:8; Ebr. 13:18; 1 Pe. 1:22) Wakati tunaonyesha zile sifa, tunakuwa bazazi bazuri, bibi ao bwana muzuri, na rafiki muzuri.

4 Zaidi ya ile, mu Biblia muko habari ya batu benye balipata magumu sawa yetu na benye balikuwa najisikia sawa siye. (1 Ko. 10:13; Yak. 5:17) Tunapata faida wakati tunasoma habari za bale batu benye baliishi kabisa na tunatumikisha mambo yenye tunajifunza. Tuzungumuzie faida mbili: Kwanza, tunaelewa kama hatuko siye peke; batu bengine pia balikuwa mu hali sawa yetu na baliweza kuvumilia. (1 Pe. 5:9) Pili, tunajifunza namna ya kupiganisha magumu.—Ro. 15:4.

5. Yehova anatumikisha nani juu ya kutuongoza mu njia ya uzima?

5 Yehova anatumia pia waabudu wenzetu juu ya kutuongoza.b Kwa mufano, baangalizi ba muzunguko banatembelea makutaniko kwa ukawaida juu ya kututia moyo. Hotuba zao zinatia imani yetu nguvu na zinatusaidia tuendelee kuwa na umoja. (Mdo. 15:40–16:5) Bazee pia banahangaikia hali ya kiroho ya kila muhubiri. (1 Pe. 5:​2, 3) Bazazi banasaidia batoto yabo bakomale kiroho. Banafanya vile kwa kubafundisha kukamata maamuzi ya muzuri na kuzoea kufanya mambo ya muzuri. (Mez. 22:6) Badada benye kukomala banasaidia badada vijana kwa kubawekea mufano muzuri, kubatolea mashauri, na kubatia moyo.—Tit. 2:​3-5.

6. Tunapaswa kufanya nini juu muongozo wa Yehova utusaidie?

6 Yehova alishafanya sehemu yake, anatutolea muongozo wenye tuko nao lazima. Namna gani tunaweza kuonyesha shukrani juu ya muongozo wenye anatutolea? Mezali 3:​5, 6 inasema hivi: “Umutegemee Yehova kwa moyo wako wote, na usitegemee uelewaji wako mwenyewe. Umutambue katika njia zako zote, naye atanyoosha mapito yako.” Wakati tunafanya vile, “atanyoosha mapito [yetu],” ni kusema, atatusaidia kuepuka magumu na kuwa na maisha ya furaha. Tuko wenye shukrani sana juu Yehova anatupenda. Na juu anatujua muzuri, anapatia kila mutu mashauri yenye iko nayo lazima!—Zb. 32:8.

YEHOVA ANATUTIMIZIA MAHITAJI YETU

7. Yehova anatusaidia kutimiza mahitaji gani? (Wafilipi 4:19)

7 Soma Wafilipi 4:19. Zaidi ya kutupatia muongozo wa kiroho, Yehova anatusaidia kupata chakula, manguo, na fasi ya kuishi. (Mt. 6:33; 2 Te. 3:12) Ni jambo ya kawaida kuhangaikia mahitaji yetu ya kimwili, lakini Yehova anatutia moyo tusihangaike sana juu ya ile mambo. (Mt. 6:25) Juu ya nini? Juu Baba yetu wa mbinguni hawezi hata kidogo kuachilia batumishi yake baaminifu wakati biko na lazima ya musaada. (Mt. 6:8; Ebr. 13:5) Tunaweza kumuamini kabisa wakati anasema kama atatupatia mambo yenye tuko nayo lazima.

8. Yehova alimufanyia nini Daudi?

8 Angalia namna Yehova alisaidia Daudi. Kwa miaka fulani, Daudi alipita mu magumu ya mingi wakati alikuwa anamukimbia Mufalme Sauli. Lakini Yehova alipatia Daudi na banaume yake mambo yenye balikuwa nayo lazima. Wakati Daudi alifikiria namna Yehova alimuhangaikia kwa miaka mingi, aliandika hivi: “Nilikuwa kijana na sasa nimezeeka, lakini sijamuona mutu yeyote mwenye haki akiwa ameachwa, wala watoto wake wakitafuta mukate.” (Zb. 37:25) Pengine na weye ulishajionea namna Yehova anapatiaka batumishi yake mambo yenye biko nayo lazima.

9. Namna gani Yehova anahangaikia batu yake wakati wa misiba? (Ona pia picha.)

9 Tena Yehova anasaidiaka batu yake mu wakati ya misiba. Kwa mufano, mu karne ya kwanza wakati mu Yerusalemu mulikuwa njala, Bakristo ba mu maeneo ingine balitumia bandugu na badada yabo misaada. (Mdo. 11:​27-30; Ro. 15:​25, 26) Leo pia batu ya Mungu banaonyesha ule ukarimu. Wakati musiba unatokea, Yehova anachochea batu yake batolee benye balipata magumu chakula, mayi, manguo, na dawa. Pia, kikundi ya wajenzi inatengeneza manyumba na Majumba ya Ufalme. Na bila kukawia batumishi ya Yehova banatia moyo na kufariji benye balipoteza bitu yabo ao benye balifisha.c

Picha: Bandugu na badada banapewa musaada wa kimwili na wa kiroho kisha musiba wa asili mu Malawi. 1. Mayi ya mingi inayala fasi ya kabambi. 2. Ndugu Gage Fleegle iko nazungumuza na ndugu na dada. 3. Bandugu biko natosha mu gari masaki ya chakula.

Namna gani Yehova anatufariji wakati wa misiba? (Ona fungu ya 9)e


10-11. Mambo yenye ilimufikia Borys inatufundisha nini?

10 Yehova anasaidiaka pia batu benye habayaanza kumuabudu. Na siye tunatafuta nafasi za kutendea muzuri benye habamutumikie Yehova. (Gal. 6:10) Kufanya vile kunatoa ushahidi wa muzuri. Fikiria mufano wa Borys, musimamizi wa masomo fulani mu Ukraine. Hata kama Borys haiko Shahidi wa Yehova, anatendeaka muzuri banafunzi Mashahidi na anaheshimia mambo yenye banaamini. Wakati Borys aliamua kukimbia vita na kuenda mu eneo ingine ya inchi yenye ilikuwa salama, bandugu balimusaidia. Kisha, Borys alihuzuria Ukumbusho wa kifo ya Yesu. Wakati Borys anakumbuka ile mambo, anasema hivi: “Mashahidi wa Yehova walinitendea muzuri na walinihangaikia. Ninawashukuru sana.”

11 Na siye tunaweza kumuiga Baba yetu mwenye rehema kwa kuonyesha upendo bale benye biko na lazima ya musaada, ikuwe banakubaliana na mambo yenye tunaamini ao hapana. (Lu. 6:​31, 36) Tunatumainia kama upendo wenye tunaonyesha batu utabachochea bakuwe banafunzi ya Kristo. (1 Pe. 2:12) Ikuwe batakubali kweli ao hapana, siye tutakuwa na furaha juu kutoa kunaleta furaha.—Mdo. 20:35.

YEHOVA ANATULINDA

12. Yehova atatolea batu yake ulinzi gani? (Zaburi 91:​1, 2, 14)

12 Soma Zaburi 91:​1, 2, 14. Leo, Yehova anaahidi kama atatulinda kiroho. Hataruhusu hata siku moya Shetani achafule ibada safi. (Yoh. 17:15) Na wakati “taabu kubwa” itaanza, tunaweza kuwa hakika kama Yehova atatimiza ahadi yake ya kulinda batu yake kiroho lakini pia kimwili.—Ufu. 7:​9, 14.

13. Namna gani Yehova analinda kila mumoya wetu?

13 Namna gani Yehova analinda kila mumoya wetu? Kupitia Maandiko, Yehova anatusaidia tujue bizuri na bibaya. (Ebr. 5:14) Wakati tunatumikisha kanuni zenye kuwa mu Neno yake, tunajilinda kiroho na kimwili. (Zb. 91:4) Zaidi ya ile, Yehova anatumia kutaniko juu ya kutulinda. (Isa. 32:​1, 2) Kupitisha wakati pamoya na batu benye banamupenda Yehova na kutii kanuni zake, kunatutia moyo na kutupatia nguvu ya kupinga mambo yenye inaweza kuharibisha hali yetu ya kiroho.—Mez. 13:20.

14. (a) Juu ya nini wakati fulani Yehova anaruhusu tupate magumu? (b) Zaburi 9:10 inatuhakikishia nini? (Ona pia maelezo ya chini.)

14 Wakati fulani Yehova alilinda batumishi yake ya zamani kimwili. Lakini, haiko kila wakati njo alifanya vile. “Matukio yenye hayatazamiwe” inaweza kutufikia. (Muh. 9:11) Pia, tangu zamani Yehova ameruhusu batu yake bateswe na hata bauawe juu ya kuonyesha kama Shetani ni muongo. (Yob. 2:​4-6; Mt. 23:34) Na leo ni vile. Hata kama Yehova hamalize magumu yetu, tunaweza kuwa hakika kama hawezi kuacha bale benye banamupenda.d—Zb. 9:10.

YEHOVA ANATUFARIJI

15. Namna gani sala, Neno ya Mungu, na Wakristo wenzetu wanatufariji? (2 Wakorinto 1:​3, 4)

15 Soma 2 Wakorinto 1:​3, 4. Wakati fulani, tunakuwaka na huzuni, na mahangaiko. Pengine uko mu hali ya nguvu yenye inafanya ujisikie kuwa peke yako. Kuko mutu mwenye anaelewa vile uko najisikia? Ndiyo, Yehova anaelewa. Yehova anajua magumu yetu, anajisikia vile tuko najisikia, lakini pia “anatufariji katika majaribu yetu yote.” Anafanya vile namna gani? Wakati tunamulilia katika sala, anatupatia “amani ya Mungu yenye kupita uelewaji wote.” (Flp. 4:​6, 7) Pia wakati tunasoma maneno ya Yehova yenye kuwa mu Biblia, tunapata faraja. Maneno ya upendo, hekima, na tumaini yenye kuwa mu Biblia inaweza kutupatia nguvu. Na ku mikutano anatufariji kupitia baamini benzetu na mafundisho ya Biblia yenye kutia moyo.

16. Mambo yenye Nathan na Priscilla balipitia inakufundisha nini?

16 Juu ya kuona namna Yehova anatufariji na kututia moyo kupitia Neno yake, ona mambo yenye ilifikia Nathan na Priscilla, benye banaishi Amerika. Miaka fulani yenye imepita, baliamua kuhamia fasi kwenye kulikuwa lazima kubwa ya bahubiri. Nathan anasema hivi: “Tulitumainia kama Yehova atabariki bidii yetu.” Lakini, kisha kufika mu mugao wabo, balipata matatizo ya afya na magumu ya kupata makuta. Ku mwisho balirudia kwabo na baliendelea kuwa na matatizo ya kupata makuta. Nathan anasema hivi: “Nilijiuliza juu ya nini Yehova hakutubariki vile tuliwazia. Nilianza hata kujiuliza ikiwa nilifanya kosa fulani.” Kisha wakati, Nathan na Priscilla balitambua kama Yehova hakubaachilia mu ile kipindi ya magumu. Nathan anasema hivi: “Mu ile kipindi ya magumu, Biblia ilikuwa sawa vile rafiki mwenye hekima mwenye alikuwa natupatia muongozo na kututia moyo. Kufikiria namna Yehova alitusaidia kuvumilia ile magumu yote kulitutayarisha kwa ajili ya magumu ya wakati wenye kuya.”

17. Namna gani dada Helga alifarijiwa? (Ona pia picha.)

17 Bandugu na badada yetu banaweza pia kutufariji. Namna gani? Fikiria mufano wa Helga, wa mu inchi ya Hongria. Kwa miaka mingi, alipata magumu yenye ilifanya akuwe na mahangaiko ya mingi na ajione kuwa wa bure. Lakini wakati anakumbuka ile kipindi, anaona kama Yehova alimufariji kupitia kutaniko. Anaandika hivi: “Sikuzote Yehova alinisaidia wakati aliona kama nguvu yangu imepunguka juu ya kazi, kuhangaikia mutoto wangu mugonjwa, na magumu ingine. Mu miaka 30 yenye imepita, Yehova amenifariji kila siku. Mara mingi ananifariji kupitia maneno ya muzuri na ya kutia moyo ya bengine. Bandugu na badada balinitumia ujumbe, karte, ao kunipongeza wakati nilikuwa na lazima kabisa ya kutiwa moyo.”

Picha: Ndugu mwenye kuzeeka iko nafarijiwa. 1. Anaangalia picha zenye batoto balimuchapia. 2. Ndugu anamutumia ujumbe. 3. Bibi na bwana banamuletea chakula. 4. Ndugu anamuita ku telefone. 5. Mutoto mwanamuke iko nachapa simba mu paradiso ya kumupatia.

Yehova anaweza kukutumikisha namna gani juu ya kufariji bengine? (Ona fungu ya 17)


18. Namna gani tunaweza kufariji bengine?

18 Tuko na pendeleo ya kuiga Mungu wetu kwa kufariji bengine. Tunaweza kufanya vile namna gani? Tunaweza kufanya vile kwa kusikiliza bengine kwa uvumilivu, kusema maneno yenye kufariji, na kubasaidia mu njia fulani. (Mez. 3:27) Tunajikaza kufariji benye kuteseka, hata benye habamutumikie Mungu. Wakati bajirani yetu biko na huzuni, banagonjwa, ao biko na mahangaiko, tunabatembelea, tunabasikiliza, na kubaambia ujumbe wenye kutia moyo wenye kuwa mu Biblia. Wakati tunamuiga Yehova, “Mungu wa faraja yote,” tunasaidia waabudu wenzetu wavumilie lakini pia tunachochea bale benye habamutumikie Yehova, bapende kujifunza juu yake.—Mt. 5:16.

SIKUZOTE YEHOVA IKO PALE JUU YETU

19. Yehova anatufanyia nini, na tunaweza kumuiga namna gani?

19 Yehova anahangaikia bote benye banamupenda. Hatuachilie wakati tuko na magumu. Sawa vile tu muzazi mwenye upendo anahangaikia mutoto wake, Yehova anahangaikia waabudu wake waaminifu. Anatuongoza, anatimiza mahitaji yetu, anatulinda, na anatufariji. Tunamuiga Baba yetu wa mbinguni mwenye upendo wakati tunategemeza na kutia bengine moyo wakati biko na magumu. Kama tunakuwa na mahangaiko ao huzuni, tukuwe hakika kama Yehova iko pamoya na siye. Yeye peke njo anatuahidi hivi: “Usiogope, kwa maana niko pamoja na wewe.” (Isa. 41:10) Kujua vile kunafanya tusiogope! Hatuko peke yetu.

NAMNA GANI YEHOVA . . .

  • anatuongoza?

  • anatimiza mahitaji yetu?

  • anatulinda na kutufariji?

WIMBO 100 Tukuwe Tayari Kukaribishana

a Ona habari “Kamata Maamuzi Yenye Inamutukuza Yehova” mu Munara wa Mulinzi wa tarehe 15, Mwezi wa 4, 2011.

b Ona fungu ya 11-14 mu habari “Endelea Kufuata Muongozo wa Yehova” mu Munara wa Mulinzi wa Mwezi wa 2, 2024.

c Unaweza kupata ku jw.org mifano ya juzi-juzi kwa kuandika “kutoa misaada” mu sehemu “tafuta.”

d Ona “Maulizo ya Wasomaji Wetu” mu Munara wa Mulinzi wa Mwezi wa 2, 2017.

e MAFASIRIO YA PICHA: Kisha musiba, ndugu wa Malawi, wako napata musaada na wako nafarijiwa.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine