Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w24 Mwezi wa 10 uku. 6-11
  • Yehova “Anaponyesha Wenye Kuvunjika Moyo”

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Yehova “Anaponyesha Wenye Kuvunjika Moyo”
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2024
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • YEHOVA ANATUHAKIKISHIA KAMA TUKO BA MAANA
  • YEHOVA ANAPENDA TUKUBALI MUSAMAHA WAKE
  • YEHOVA ANATUFARIJI KUPITIA ROHO YAKE TAKATIFU
  • YEHOVA ANATUFARIJI KUPITIA NDUGU NA DADA ZETU
  • ACHA AHADI ZA YEHOVA ZIKUFARIJI
  • Hatuko Peke Yetu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
  • Kumbuka Kama Yehova Ni “Mungu Mwenye Kuishi”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2024
  • Namna ya Kupiganisha Mashaka
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2024
  • Yehova Atakusaidia Wakati wa Magumu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2024
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2024
w24 Mwezi wa 10 uku. 6-11

HABARI YA KUJIFUNZA YA 40

WIMBO 30 Baba Yangu, Mungu Wangu, na Rafiki Yangu

Yehova “Anaponyesha Wenye Kuvunjika Moyo”

“Anaponyesha wenye kuvunjika moyo; anafunga vidonda vyao.” —ZB. 147:3.

WAZO KUBWA

Mu hii habari tutaona namna Yehova anatuliza maumivu yetu ya moyo na namna tunaweza kufariji wengine.

1. Yehova anaona namna gani batumishi yake?

YEHOVA anaona nini wakati anaangalia batumishi yake ku dunia? Anajua maumivu yetu na furaha yetu. (Zb. 37:18) Wakati anaona namna tuko nafanya yetu yote juu ya kuendelea kumutumikia hata kama tuko na maumivu mu moyo, anafurahi sana! Zaidi ya ile, iko tayari kutusaidia na kutufariji.

2. Yehova anafanyia nini batu benye kuvunjika moyo, na tunaweza kufanya nini juu tupate ile musaada?

2 Zaburi 147:3 inaonyesha kama Yehova ‘anafunga vidonda’ vya wenye kuvunjika moyo. Hii andiko inamuonyesha Yehova kuwa mutu mwenye anahangaikia kwa upendo batu benye kuwa na vidonda vya moyo. Tunapaswa kufanya nini juu tupate musaada wa Yehova? Fikiria hii mufano: Munganga mwenye uzoefu anaweza kutunza muzuri mutu mwenye kuumia na kumusaidia apone. Lakini juu ule mutu apone, anapaswa kufuata kwa uangalifu mambo yenye munganga anamuambia. Mu hii habari, tutaona mambo yenye Yehova anaambia, kupitia Neno yake, bale benye biko na maumivu ya moyo na tutaona namna ya kutumikisha ile mashauri yenye upendo.

YEHOVA ANATUHAKIKISHIA KAMA TUKO BA MAANA

3. Juu ya nini batu fulani banajionaka kuwa ba bure?

3 Mu dunia yenye tunaishi hamuna upendo, na jambo ya kuhuzunisha ni kama, ile inafanya batu mingi bajisikie sawa vile habiko ba maana. Dada mwenye kuitwa Helena anasema hivi: “Mu familia yetu bazazi yetu habakutuonyesha upendo. Baba alikuwa na jeuri sana na alikuwa natuambia kila siku kama hatuko ba maana.” Sawa Helen, pengine na weye batu fulani balikutendea mubaya, balikuwa nakusema-sema mubaya ao kukufanya ujisikie kama uko mutu wa bure. Kama ni vile, inaweza kuwa nguvu kwako kuamini kama kuko mutu mwenye anaweza kukupenda na kukuhangaikia.

4. Kulingana na Zaburi 34:​18, Yehova anatuhakikishia nini?

4 Hata kama batu fulani balikutendea mubaya, ukuwe hakika kama Yehova anakupenda na anakuona kuwa wa maana. “Iko karibu na wale wenye kuvunjika moyo.” (Soma Zaburi 34:18.) Kama unajisikia kuwa mwenye “kupondwa roho,” kumbuka kama Yehova aliona mambo ya muzuri mu moyo wako na alikualika kwake. (Yoh. 6:44) Kila siku, Yehova iko tayari kukusaidia juu uko wa maana kwake.

5. Tunajifunza nini kupitia namna Yesu alitendea batu benye balikuwa naonewa?

5 Wakati tunachunguza mufano wa Yesu, tunaelewa namna Yehova anatuona. Mu utumishi wake ku dunia, Yesu alihangaikia bale benye balikuwa naonewa, na alibatendea muzuri. (Mt. 9:​9-12) Wakati mwanamuke mwenye alikuwa na ugonjwa mubaya sana aligusa nguo yake juu apone, Yesu alimufariji na alimupongeza juu ya imani yake. (Mk. 5:​25-34) Yesu anaiga kwa ukamili sifa za Baba yake. (Yoh. 14:9) Kwa hiyo, unaweza kuwa hakika kama Yehova anakuona kuwa wa maana na anaona sifa zako za muzuri, anaona imani yako, na namna unamupenda.

6. Mutu anaweza kufanya nini kama anajiona kuwa wa bure?

6 Unaweza kufanya nini kama unajiona kuwa mutu wa bure? Soma maandiko ya Biblia yenye itakuhakikishia kama Yehova anakuona kuwa wa maana, na ufikiri sana juu ya ile maandiko.b (Zb. 94:19) Kama ulishindwa kutimiza muradi fulani ao kama unavunjika moyo juu hauwezi kafanya mambo mingi sawa bengine, usijihukumu kupita kiasi. Yehova hatuombake mambo yenye inapita uwezo wetu. (Zb. 103:​13, 14) Kama mutu alikutendea mubaya zamani, usiwaze kama ni kosa yako. Kosa ni ya mutu mwenye alikutendea mubaya! Kumbuka kama kwa Yehova ni ule mwenye alitenda mubaya njo iko na kosa, haiko mwenye balitendea mubaya. (1 Pe. 3:12) Sandra, dada mwenye balitendea mubaya sana wakati alikuwa mutoto, anasema hivi: “Kila mara ninamuomba Yehova anisaidie nikuwe na mawazo muzuri juu yangu mwenyewe, na nijione namna ananiona.”

Mwanaume Mwisraeli iko na shomoro ku mukono.

Yehova Anakuona Kuwa wa Maana

Maandiko yenye kufuata itakuhakikishia kama uko wa maana kwa Yehova:

  • Zaburi 56:8. Wakati uko na huzuni, Yehova anaona machozi yako. Yehova anahangaikia sana namna uko najisikia.

  • Luka 12:​6, 7. Kama Yehova anaona ndege shomoro moya kuya ya maana sana, hauone kama weye uko wa maana zaidi kwake? Anakuhangaikia sana na anakujua muzuri juu anakupenda.

  • 1 Yohana 3:​19, 20. Ikiwa unajisikia kama hauko wa maana, kumbuka kama Yehova ‘ni mukubwa kuliko moyo wako’ na anakupenda.

7. Namna gani mambo yenye ilitufikia mu maisha zamani inaweza kutusaidia mu utumishi wetu kwa Yehova?

7 Kuwa hakika kama Yehova anaweza kukutumikisha juu ya kusaidia bengine. Amekupatia pendeleo ya kutumika pamoya naye mu kazi ya kuhubiri. (1 Ko. 3:9) Mambo yenye ilikufikia mu maisha zamani inakusaidia kujitia pa nafasi ya bengine na kuelewa muzuri namna bengine banajisikia. Unaweza kubasaidia. Helen, mwenye tulizungumuzia, alipewa musaada na sasa naye anaweza kusaidia bengine. Anasema hivi: “Miye mwenye nilikuwa najiona kuwa wa ‘bure’ Yehova amenigeuza, nimekuwa mutu mwenye anaweza kusaidia bengine.” Sasa Helen ni painia wa kawaida mwenye furaha.

YEHOVA ANAPENDA TUKUBALI MUSAMAHA WAKE

8. Isaya 1:18 inatuhakikishia nini?

8 Batumishi fulani ba Yehova banahuzunika sana juu ya makosa yenye balifanyaka zamani, ikuwe mbele ya kubatizwa ao hata kisha. Lakini ni muzuri tukumbuke kama Yehova alitutolea bei ya ukombozi juu anatupenda sana. Kwa kweli, Yehova anapenda tukubali ile zawadi. Yehova anatuhakikishia kama kisha ‘kunyoosha mambo’c pamoya naye, anasahau kabisa zambi zetu. (Soma Isaya 1:18.) Tuko wenye furaha sana juu Yehova, Baba yetu wa mbinguni mwenye upendo, anasahau zambi zetu za zamani! Lakini hawezi kusahau hata siku moya mambo ya muzuri yenye tulifanya.—Zb. 103:​9, 12; Ebr. 6:10.

9. Juu ya nini hatupaswe kukazia akili zambi zenye tulifanyaka zamani?

9 Kama unahuzunika sana juu ya mambo yenye ulifanyaka zamani, fanya yako yote juu ya kukazia akili mambo yenye uko nafanya leo, na mambo yenye utafanya mu masiku yenye kuya. Fikiria mufano ya mutume Paulo. Alihuzunika juu zamani alitesa sana Wakristo, lakini alijua kama Yehova alimusamehe. (1 Ti. 1:​12-15) Paulo aliendelea kukazia akili zambi zake za zamani? Hapana. Sawa tu vile hakuendelea kufikiria mambo yenye alifanya juu ya akuwe mufarisayo mwenye kuheshimiwa, hakuendelea kufikiria makosa yake ya zamani. (Flp. 3:​4-8, 13-15) Lakini, Paulo alifanya yake yote mu utumishi wake na alikazia akili wakati wenye kuya. Sawa Paulo, hauwezi kubadilisha mambo yenye ulifanyaka zamani. Lakini unaweza kumusifu Yehova kupitia mambo yenye unafanya leo na kufikiria mambo ya muzuri yenye Yehova atakufanyia mu wakati wenye kuya.

10. Tunaweza kufanya nini kama matendo yetu ya zamani iliumiza bengine?

10 Unaweza kujisikia mubaya juu ya matendo yako ya zamani yenye iliumiza bengine. Nini njo inaweza kukusaidia? Fanya yote yenye unaweza juu ya kutengeneza mambo, uombe musamaha na uonyeshe kupitia matendo yako kama unahuzunika. (2 Ko. 7:11) Umuombe Yehova asaidie bale benye matendo yako iliumiza. Yehova anaweza kukusaidia weye na benye uliumiza juu nyie bote muweze kuvumilia na kuwa tena na amani.

11. Mufano wa nabii Yona unaweza kutufundisha nini? (Ona pia ku jalada.)

11 Makosa yako ya zamani ikufundishe na uache Yehova akutumikishe mu njia yoyote yenye anataka. Fikiria mufano wa nabii Yona. Kuliko kuenda Ninawi vile Mungu alimuambia, Yona alikimbia na kuenda fasi ingine. Yehova alimurekebisha, na Yona alijifunza kupitia makosa yake. (Yon. 1:​1-4, 15-17; 2:​7-10) Lakini Yehova hakuacha kumutumikisha nabii wake Yona. Alimupatia nafasi ingine ya kuenda Ninawi, na Yona alitii bila kukawia. Hakuacha huzuni juu ya makosa yake ya zamani imuzuie kuitika ile mugao yenye Yehova alimupatia.—Yon. 3:​1-3.

Nabii Yona anasimama pembeni ya habari na iko naangalia mbinguni. Analobana.

Kisha nabii Yona kuokoka kutoka mu samaki kubwa, Yehova alimuambia tena aende Ninawi na atangaze ujumbe wake (Ona fungu ya 11)


YEHOVA ANATUFARIJI KUPITIA ROHO YAKE TAKATIFU

12. Namna gani Yehova anatupatia amani wakati jambo fulani ya mubaya inatufikia? (Wafilipi 4:​6, 7)

12 Kupitia roho yake takatifu, Yehova anatufariji wakati jambo fulani ya mubaya inatufikia. Tuone mambo yenye ilifikia Ron na Carol. Jambo ya kuhuzunisha ilibafikia. Mutoto wabo alijiua. Banasema hivi: “Mu maisha yetu tulishakapata magumu ya nguvu, lakini hatuyapataka magumu ya nguvu sana sawa ile. Mara mingi hatukupata usingizi usiku, kwa hiyo tulisali kwa Yehova kisha tulijisikia kuwa wenye kutulia na tulipata amani yenye kuzungumuziwa mu Wafilipi 4:​6, 7.” (Soma.) Kama uko mu magumu ya nguvu sana, unaweza kumumwangia Yehova moyo wako katika sala, unaweza kusali saa yoyote na sala zako zinaweza kuwa na urefu wenye unapenda. (Zb. 86:3; 88:1) Umuombe Yehova roho yake takatifu tena na tena. Yehova hawezi kuzarau mambo yenye unamuomba.—Lu. 11:​9-13.

13. Namna gani roho takatifu inaweza kutusaidia tuendelee kumutumikia Yehova kwa uaminifu? (Waefeso 3:16)

13 Umepata magumu ya nguvu yenye imekumaliza nguvu? Roho takatifu inaweza kukupatia nguvu ya kuendelea kumutumikia Yehova kwa uaminifu. (Soma Waefeso 3:16.) Ona mambo yenye ilifikia dada mwenye kuitwa Flora. Yeye na bwana yake balikuwa natumika pamoya mu kazi ya umisionere, kisha bwana yake akakosa uaminifu na bakavunja ndoa. Dada Flora anasema hivi: “Ile jambo yenye alinitendea iliniluma sana mupaka sikuweza kufikiria tena kitu ingine. Nilisali kwa Yehova juu anipatie roho yake takatifu ili niweze kuvumilia. Ku mwanzo niliwaza kama sitaweza, lakini Yehova alinipatia nguvu na niliweza kuvumilia.” Dada Flora anaona kama Mungu amemusaidia amutegemee zaidi na iko hakika kama atamusaidia mu magumu yake yote. Anasema tena hivi: “Maneno yenye kuwa mu Zaburi 119:32 inanigusa kabisa: ‘Nitafuata kwa bidii njia ya amri zako kwa sababu unaifanyia nafasi katika moyo wangu.’”

14. Tunaweza kufanya nini juu roho takatifu ya Mungu itusaidie?

14 Namna gani unaweza kutenda kulingana na sala yako ya kuomba roho takatifu? Fanya mambo mbalimbali yenye itasaidia roho takatifu ya Mungu ifanye kazi mu maisha yako. Mambo sawa vile kukusanyika na kuhubiri. Jaza mu akili yako mawazo ya Yehova kwa kusoma Neno yake kila siku. (Flp. 4:​8, 9) Wakati uko nasoma, tafuta habari za watu wa Mungu wenye walipambana na magumu na ufikiri sana juu ya namna Yehova aliwasaidia kuvumilia. Sandra, mwenye tulizungumuzia, alipata magumu ya mingi na yenye ilifuatana. Anasema hivi: “Habari ya Yosefu ilinigusa sana. Hata kama alipata magumu ya mingi na alitendewa bila haki, hakuacha ile iregeze urafiki wake pamoya na Yehova.”—Mwa. 39:​21-23.

YEHOVA ANATUFARIJI KUPITIA NDUGU NA DADA ZETU

15. Ni nani njo wanaweza kutufariji, na wanaweza kutusaidia namna gani? (Ona pia picha.)

15 Wakati wa magumu, ndugu na dada zetu wanaweza kuwa “chanzo cha faraja nyingi.” (Kol. 4:11) Yehova anatumia bandugu na badada juu ya kutuonyesha kama anatupenda. Banatufariji kwa kutusikiliza na kujiweka pa nafasi yetu, ao kwa kupitisha wakati pamoya na siye. Banaweza kutupatia andiko ya Biblia yenye kutia moyo ao kusali pamoya na siye.d (Ro. 15:4) Wakati fulani, banaweza kutukumbusha namna ya Yehova ya kuona mambo na ile inaweza kutusaidia tuendelee kuvumilia. Wakristo wenzetu wanaweza pia kutupatia mambo yenye tuko nayo lazima, sawa vile kututayarishia chakula wakati tuko mu magumu.

Wazee wawili wametembelea dada mu hopitali. Biblia zao ziko wazi wakati wako nazungumuza naye.

Marafiki wenye kukomala kiroho na wenye kutumainika, wanaweza kutufariji na kututegemeza sana (Ona fungu ya 15)


16. Tunaweza kufanya nini juu bengine baweze kutusaidia?

16 Juu bengine batusaidie, inaweza kuwa muzuri tubaombe musaada. Bandugu na badada yetu banatupenda sana na banapenda kutusaidia. (Mez. 17:17) Lakini pengine habajue namna tuko najisikia na mambo yenye tuko nayo lazima. (Mez. 14:10) Kama uko na mahangaiko, unaweza kuzungumuza na barafiki bazuri na kubaambia namna uko najisikia. Ubaambie mambo yenye banaweza kufanya juu ya kukusaidia. Unaweza kuzungumuza na muzee moya ao bawili benye unazoea. Badada fulani bameona kama kuzungumuza na dada mwenye kukomaa kiroho kunasaidiaka.

17. Ni mambo gani yenye inaweza kutuzuia kupata musaada wa bengine na namna gani tunaweza kuepuka ile mambo?

17 Epuka kujitenga na bengine. Juu ya maumivu yako ya moyo, wakati fulani unaweza kupenda kubakia tu weye peke. Wakati fulani, bandugu na badada banaweza kushindwa kukuelewa ao banaweza kusema maneno yenye inakuumiza. (Yak. 3:2) Usiache ile mambo ikuzuie kupata kitia moyo yenye uko nayo lazima. Muzee mwenye kuitwa Gavin, mwenye anapambana na matatizo ya kushuka moyo, anasema hivi: “Mara mingi sipendi kupitisha wakati ao kuzungumuza na bengine.” Hata vile, Gavin anajikaza kupitisha wakati na bengine, na ile inamutia moyo. Dada mwenye jina yake Amy anasema hivi: “Juu ya mambo yenye ilinifikiaka mu maisha, ni nguvu kwangu kuaminia batu. Lakini niko najifunza kupenda na kuaminia ndugu na dada zangu kama vile Yehova anafanya. Ninajua kama kufanya vile kunamufurahisha Yehova, na kunaniletea na miye furaha.”

ACHA AHADI ZA YEHOVA ZIKUFARIJI

18. Ni nini itatokea mu wakati wenye kuya, na tunaweza kufanya nini leo?

18 Tunaweza kuwa hakika kama hivi karibuni, Yehova ataponyesha maumivu yetu yote; ikuwe ya kimwili ao ya mu moyo. (Ufu. 21:​3, 4) Ile wakati, ‘hatutakumbuka’ mambo ya mubaya yenye ilitufikia. (Isa. 65:17) Sawa vile tuliona, hata sasa Yehova ‘anafunga vidonda vyetu.’ Yehova ametayarisha njia mingi za kutufariji na kutusaidia. Acha basi Yehova akufariji kupitia zile njia. Kila siku, ukuwe hakika kama ‘anakuhangaikia.’—1 Pe. 5:7.

YEHOVA ANATUSAIDIA NAMNA GANl . . .

  • tuone kama tuko wa maana?

  • tuache kuhuzunika juu ya makosa yetu ya zamani?

  • tupate faraja kutoka kwa waamini wenzetu?

WIMBO 7 Yehova Ni Nguvu Yangu

a Majina fulani imebadilishwa.

b Ona kisanduku “Yehova Anakuona Kuwa wa Maana.”

c Ili ‘kunyoosha mambo’ pamoya na Yehova, tunapaswa kuonyesha kama tumetubu kwa kumuomba Yehova atusamehe na kwa kubadilisha tabia zetu. Tukifanya zambi nzito, ni lazima tutafute pia musaada wa wazee wa kutaniko.—Yak. 5:​14, 15.

d Kwa mufano, angalia maandiko yenye inapatikana chini ya kichwa “Mahangaiko” na “Kitulizo” mu kitabu Maandiko ya Kutusaidia mu Maisha ya Kikristo.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine