Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w25 Mwezi wa 6 uku. 14-19
  • Itika Kama Kuko Mambo Yenye Haujue

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Itika Kama Kuko Mambo Yenye Haujue
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • HATUJUE WAKATI MWISHO ITAFIKA
  • HATUJUE NAMNA YEHOVA ANAWEZA KUTENDA
  • HATUJUE BYA KESHO
  • HATUWEZI KUELEWA MUZURI NI KWA KADIRI GANI YEHOVA ANATUJUA
  • Utafute Majibu ya hii Maulizo
    Programu ya Mukusanyiko wa Muzunguko wa 2025-2026 Pamoja na Mwangalizi wa Muzunguko
  • Maamuzi Yenye Inaonyesha Kama Tunamutegemea Yehova
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2023
  • Kumbuka Kama Yehova Ni “Mungu Mwenye Kuishi”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2024
  • Utafute Majibu ya hii Maulizo:
    Programu ya Mukusanyiko wa Muzunguko wa 2025-2026 Pamoja na Mujumbe wa Tawi
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
w25 Mwezi wa 6 uku. 14-19

HABARI YA KUJIFUNZA YA 26

WIMBO 123 Tutii Mupango wa Kiteokrasi

Itika Kama Kuko Mambo Yenye Haujue

“Hatuwezi kumuelewa kabisa Mweza-Yote.”—YOB. 37:23.

WAZO KUBWA

Hata kama kuko mambo yenye hatujue, tunaweza kuvumilia magumu kama tunakazia akili mambo yenye tunajua, na kama tunamutumainia Yehova.

1. Yehova alituumba na uwezo gani, na juu ya nini?

YEHOVA alituumba mu njia ya ajabu. Alitupatia uwezo wa kufikiri, wa kujifunza mambo ya mupya, na wa kuelewa mambo yenye tunajifunza na kuitumikisha. Juu ya nini alituumba vile? Juu anapenda ‘tupate ujuzi juu yake,’ na tutumie ule ujuzi juu ya kukamata maamuzi ya muzuri wakati tuko namutumikia.—Mez. 2:1-5; Ro. 12:1.

2. (a) Tuko na mipaka gani? (Yobu 37:23, 24) (Ona pia picha) (b) Tunapata faida gani wakati tunaitika kama kuko mambo yenye hatujue?

2 Ni kweli Yehova alituumba na uwezo wa kujifunza, lakini tuko na mipaka; kuko tu mambo yenye hatujue. (Soma Yobu 37:23, 24.) Mufano wa Yobu unatusaidia kuelewa ile jambo. Yehova alimuuliza maulizo ya mingi yenye ilimusaidia aelewe kama kuko mambo mingi yenye hakujua. Ile ilimusaidia ajinyenyekeze na abadilishe mawazo yake. (Yob. 42:3-6) Na siye tunapata faida wakati tunaitika kama kuko mambo yenye hatujue. Kuitika kama kuko mambo yenye hatujue kunafanya tutumainie kama Yehova atatujulisha mambo yenye ni lazima kabisa tujue juu tuweze kukamata maamuzi ya hekima.—Mez. 2:6.

Mwangaza inatoka mu mawingu na kumuangazia Yobu wakati Yehova iko nazungumuza naye. Elihu na bafariji tatu ba bongo biko pembeni na biko naangalia.

Kama Yobu, na siye tutapata faida ikiwa tunakubali kama kuko mambo yenye hatujue (Ona fungu ya 2)


3. Tutazungumuzia nini mu hii habari?

3 Mu hii habari tutaona mambo fulani yenye hatujue, na mahangaiko yenye tunaweza kuwa nayo juu hatujue ile mambo. Tena, tutaona juu ya nini ni jambo ya muzuri vile kuko mambo yenye hatujue. Kuzungumuzia ile mambo itatusaidia tukuwe hakika kama Yehova, “Ule mwenye kuwa mukamilifu katika ujuzi,” anatuambiaka mambo yenye ni lazima kabisa tujue.—Yob. 37:16.

HATUJUE WAKATI MWISHO ITAFIKA

4. Kulingana na Matayo 24:36, hatujue nini?

4 Soma Matayo 24:36. Hatujue wakati mwisho itafika. Hata Yesu naye wakati alikuwa ku dunia hakujua “siku ile na saa ile.”a Aliambia mitume wake kama Yehova njo iko na haki ya kuamua wakati wenye matukio fulani itatokea. (Mdo. 1:6, 7) Yehova alishapanga wakati wenye mwisho itafika. Lakini siye hatujue ile siku wala ile saa.

5. Kukosa kujua siku yenye mwisho itafika, inaweza kuwa na matokeo gani juu yetu?

5 Sawa vile maneno ya Yesu inaonyesha, hatujue tutaendelea kuchunga mupaka wakati gani mbele mwisho ifike. Ile inaweza kufanya tuchoke kuchunga ao tuvunjike moyo, zaidi sana kama tulishangoya siku ya Yehova kwa miaka mingi. Pia inaweza kuwa nguvu kuvumilia wakati batu ya familia ao batu bengine banatucheka juu mwisho haiyafika. (2 Pe. 3:3, 4) Tunaweza kuwaza kama ikiwa tungejua siku yenye mwisho itafika, ingekuwa mwepesi zaidi kuichunga na kuvumilia wakati bengine banatucheka.

6. Juu ya nini ni muzuri vile hatujue siku yenye mwisho itafika?

6 Kusema kweli, ni muzuri vile Yehova hatuambie siku yenye mwisho itafika. Juu ya nini? Kwa kufanya vile anatupatia nafasi ya kuonyesha kama tunamutumikia juu tunamupenda na tunamutumainia. Tungekuwa najua ile siku, ingekuwa sawa vile tuko namutumikia juu tu tunajua kama siku yake iko karibu. Njo maana kuliko kukazia akili wakati wenye ile siku na ile saa itafika, ni muzuri kukazia akili mambo yenye itafanyika kisha ile siku. Kufanya vile kutatusaidia tuendelee kumukaribia Yehova na kumutumainia. Kutatusaidia pia tuendelee kufanya yetu yote juu ya kumufurahisha.—2 Pe. 3:11, 12.

7. Tunajua nini?

7 Ni muzuri tukazie akili mambo yenye tunajua. Tunajua nini? Tunajua kama siku za mwisho zilianza mu 1914. Maunabii ya Biblia njo inatusaidia tujue kama siku za mwisho zilianza ile mwaka. Zaidi ya ile, Biblia ilitabiri mambo mbalimbali yenye ilianza kutokea ile mwaka. Ile yote inatuhakikishia kama “siku kubwa ya Yehova iko karibu.” (Sef. 1:14) Tunajua pia kazi yenye Yehova anapenda tufanye. Anapenda tuhubirie batu mingi sana “habari njema ya Ufalme.” (Mt. 24:14) Ile habari njema iko nahubiriwa mu maeneo 240 hivi na mu luga zaidi ya 1000. Haiko lazima tujue siku na saa yenye mwisho itafika juu tuhubiri habari njema kwa bidii.

HATUJUE NAMNA YEHOVA ANAWEZA KUTENDA

8. Maneno “kazi ya Mungu wa kweli” inamaanisha nini? (Muhubiri 11:5)

8 Haiko kila mara njo tunajuaka “kazi ya Mungu wa kweli.” (Soma Muhubiri 11:5.) “Kazi ya Mungu wa kweli” ni mambo yenye Yehova anafanya itokee, ao mambo yenye anaruhusu itokee juu ya kutimiza mapenzi yake. Hatuwezi kujua juu ya nini kabisa Yehova anaruhusu jambo fulani itokee ao kujua mambo yenye atafanya juu ya kutusaidia. (Zb. 37:5) Hatuwezi kujua kabisa ile mambo, sawa vile tu hatujue namna mutoto anakomalaka mu tumbo; hata banasayansi habayaelewa muzuri-muzuri namna mutoto anakomalaka mu tumbo.

9. Kukosa kujua namna Yehova atatusaidia kunaweza kuwa na matokeo gani juu yetu?

9 Juu hatujue namna Yehova anaweza kutusaidia, tunaweza kusita kukamata maamuzi fulani. Kwa mufano, tunaweza kusita kuacha mambo fulani yenye tunapendaka juu tuweze kufanya mambo mingi zaidi mu kazi ya kuhubiri ao kuhamia kwenye kuko lazima kubwa ya wahubiri. Ao tuko napenda kufikia muradi fulani, lakini hatuifikie. Ao tena tuko nahubiri sana, lakini hatupate matokeo ya muzuri. Ao pengine tuko napata magumu mingi mu mugao fulani wa kiteokrasi. Ile mambo inaweza kufanya tuwaze kama Yehova hatukubali tena.

10. Kukosa kujua vile Yehova atatenda kunatusaidia kukomalisha sifa gani?

10 Ni muzuri vile hatujue namna Yehova atatenda juu ile inatusaidia tukomalishe sifa za maana sawa vile unyenyekevu na kiasi. Tunaelewa kama mawazo ya Yehova na njia zake ziko yulu sana kupita zetu. (Isa. 55:8, 9) Tunajifunza kumutegemea Yehova zaidi na kuwa hakika kama, kwa musaada wake mambo itakuwa muzuri. Na wakati tunapata matokeo ya muzuri mu kazi ya kuhubiri ao mu kazi ingine ya kiteokrasi, tunamupatia Yehova utukufu. (Zb. 127:1; 1 Ko. 3:7) Kama mambo haipitikane vile tuliwazia, tunapaswa kukumbuka kama Yehova iko naona. (Isa. 26:12) Siye tufanye yenye tunaweza na tuendelee kutumainia kama Yehova atafanya yenye inabakia. Hata kama Yehova hatatufanyia miujiza sawa vile alikuwaka nafanya zamani, tuko hakika kama atatupatia muongozo wenye tuko nao lazima.—Mdo. 16:6-10.

11. Tunajua mambo gani ya maana?

11 Fikiria mambo yenye tunajua. Tunajua kama Yehova anakuwaka na upendo, haki, na hekima. Tunajua kama anafurahia sana mambo yenye tunamufanyia na mambo yenye tunafanyia baabudu benzetu. Pia tunajua kama sikuzote Yehova anabariki bale benye banaendelea kuwa bashikamanifu kwake.—Ebr. 11:6.

HATUJUE BYA KESHO

12. Yakobo 4:13, 14 inatufundisha nini?

12 Soma Yakobo 4:13, 14. Kusema tu kweli, hatujue vile maisha yetu itakuwa kesho. Mu hii dunia, “wakati na matukio yenye hayatazamiwe” inaweza kutufikia. (Muh. 9:11) Njo maana hatuwezi kujua kama mipango yetu itatimia ao kama tungali naishi juu tuweze kuitimiza.

13. Kukosa kujua bya kesho kunaweza kuwa na matokeo gani juu yetu?

13 Kukosa kujua vile mambo itakuwa kesho kunaweza kutuletea mahangaiko. Juu ya nini? Juu tunaweza kuanza kuogopa mambo yenye inaweza kutokea, na ile inaweza kutupotezea furaha. Mambo ya mubaya inaweza kutufikia kwa kushitukia, ao maisha yetu inaweza kubadilika bila kutazamia. Ile inaweza kufanya tukuwe na huzuni na kutuletea mahangaiko. Ao tena, wakati mambo yenye tulikuwa natazamia haifike, tunaweza kuvunjika moyo.—Mez. 13:12.

14. Tunapaswa kufanya nini juu tukuwe na furaha? (Ona pia picha.)

14 Hata nini itokee mu maisha yetu, wakati tunavumilia magumu tunaonyesha kama tunamutumikia Baba yetu wa mbinguni juu tunamupenda. Biblia inatusaidia kuelewa kama haiko kila magumu njo Yehova atatuepusha nayo, na kama Yehova hapangake mbele ya wakati mambo yenye itatupata mu maisha. Anajua kama juu tukuwe na furaha haiko lazima tujue mbele ya wakati mambo yenye itatupata kesho ao kesho yake. Lakini anajua kama juu tukuwe na furaha tunapaswa kufuata muongozo wake na kumutii. (Yer. 10:23) Wakati tunatafuta muongozo wa Yehova mbele ya kukamata maamuzi, ni sawa vile tuko nasema: “Kama Yehova anapenda, tutaishi na kufanya hiki ao kile.”—Yak. 4:15.

Picha: 1. Baba na mutoto yake banatia bitu mu sakoshi. Banatia mu sakoshi Biblia na bintu bingine bya lazima. 2. Ule baba, bibi yake na mutoto biko mu hema wakati mvula iko nanyesha. Mu hii hali ya nguvu banatumikisha bitu bienye balitia mu sakoshi.

Kutafuta muongozo wa Yehova na kumutii kunatulinda (Ona fungu ya 14-15)b


15. Tunajua nini juu ya wakati wenye kuya?

15 Ni kweli hatujue byenye binaweza kutufikia kesho. Lakini tunajua kama Yehova ameahidi kutupatia uzima wa milele, bamoya mbinguni na bengine ku dunia. Tunajua kama hawezi kusema bongo, na hakuna kitu yenye inaweza kumuzuia kutimiza ahadi zake zote. (Tit. 1:2) Yeye tu njo anaweza ‘kutabiri matokeo tangu mwanzo na tangu zamani sana mambo yenye bado hayajafanywa.’ Mambo yenye alitabiri zamani ilitimia. Na mambo yenye alishatabiri juu ya masiku yenye iko nakuya, nayo itatimia. (Isa. 46:10) Tuko hakika kama hakuna kitu yenye inaweza kumufanya aache kutupenda. (Ro. 8:35-39) Atatupatia hekima, atatufariji, na atatupatia nguvu yenye tuko nayo lazima juu tuvumilie magumu yote yenye tutakutana nayo. Tukuwe hakika kama Yehova atatusaidia na atatubariki.—Yer. 17:7, 8. 

HATUWEZI KUELEWA MUZURI NI KWA KADIRI GANI YEHOVA ANATUJUA

16. Sawa vile Zaburi 139:1-6 inasema, Yehova anajua nini juu yetu, na ile inafanya ujisikie namna gani?

16 Soma Zaburi 139:1-6. Muumbaji wetu anatujua muzuri sana. Anajua juu ya nini tuko vile tuko, juu ya nini tunajisikiaka vile tunajisikiaka, na juu ya nini tunawazaka vile tunawazaka. Anatuhangaikiaka kila wakati. Anajua byenye tunasema, na byenye tulipenda kumaanisha. Anajua mambo yenye tunafanya na juu ya nini tunaifanya. Mufalme Daudi alisema kama Yehova iko tayari kutusaidia sikuzote na iko na uwezo wa kufanya vile. Inagusa moyo sana kujua kama Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa wa ulimwengu wote, Mungu Mweza-Yote, Muumbaji wa mbingu na dunia, anatuhangaikia sana vile. Daudi alisema hivi: “Ujuzi wa namna hiyo unapita uelewaji wangu. Uko mwingi sana, siwezi kuuelewa.”—Zb. 139:6, maelezo ya chini.

17. Juu ya nini inaweza kuwa nguvu kuitika kama Yehova anatujua muzuri?

17 Mambo sawa vile desturi yetu, mambo yenye tulikuwa naamini mbele tujue kweli, ao hata namna tuliishi mu familia yetu inaweza kufanya ikuwe nguvu kwetu kuona kama Yehova ni Baba mwenye upendo, mwenye anatuhangaikia. Ao tunaweza kuwaza kama juu zamani tulifanyaka makosa makubwa, Yehova hatapenda kutujua na kama iko mbali na siye. Daudi naye aliwazaka vile wakati fulani. (Zb. 38:18, 21) Tena mutu mwenye iko najikaza kubadilisha maisha yake juu aishi kulingana na kanuni za Yehova, anaweza kujiuliza hivi: ‘Kama Mungu ananielewa muzuri, juu ya nini anapenda nibadilishe maisha yangu na najua muzuri kama hivi njo ninakuwaka?’

18. Tunapata faida gani wakati tunaitika kama Yehova anatujua muzuri kupita vile tunajijua? (Ona pia picha.)

18 Tunaweza kujifunza kuitika kama Yehova anatujua muzuri kupita vile tunajijua, na kama anaona bizuri byenye biko mu siye byenye siye hatuwezi kuona. Ni kweli Yehova anaonaka uzaifu wetu na anaelewa juu ya nini tuko vile. Lakini anajua kama tunaweza kubadilika, na kwa upendo anatusaidia kufanya mabadiliko. Yehova anajua kama tunaweza kuwa batu bazuri kabisa. (Ro. 7:15) Kujua vile kunatuchochea tuendelee kumutumikia kwa uaminifu na kwa furaha.

Picha: 1. Ndugu mwenye kuvunjika moyo iko naangalia ku dirisha wakati inje kuko giza na mvula. 2. Mu Paradiso ule ndugu iko natembea mu njia pamoya na barafiki yake na biko nafurahia mazingira.

Yehova anatusaidia tukuwe hakika kabisa kama ahadi zake juu ya dunia mupya zitatimia. Ile inaweza kutusaidia tuendelee kuvumilia hata kama hatujue bya kesho (Ona fungu ya 18-19)c


19. Ni mambo gani tunajua kabisa juu ya Yehova?

19 Tunajua kama Yehova ni upendo. Hatuna hata shaka moya juu ya ile jambo. (1 Yo. 4:8) Tunajua kama anatuomba tufuate kanuni zake juu anatupenda na anapenda tukuwe na maisha ya muzuri. Tunajua kama Yehova anapenda tupate uzima wa milele. Na juu ile iwezekane alitupatia bei ya ukombozi. Bei ya ukombozi inatuhakikishia kama tunaweza kumutumikia Yehova kwa uaminifu hata kama hatukamilike. (Ro. 7:24, 25) Pia tunajua kama “Mungu ni mukubwa kuliko mioyo yetu na anajua mambo yote.” (1 Yo. 3:19, 20) Yehova anaona kila kitu juu yetu na anatutumainia, anajua kama tunaweza kufanya mapenzi yake.

20. Ni nini itatusaidia tusihangaike sana juu ya mambo yenye hatujue?

20 Yehova hatufichake mambo yenye tuko na lazima ya kujua. Wakati tunakubali ile kweli, tunaepuka kuhangaikia sana mambo yenye hatujue na tunakazia akili mambo ya maana zaidi. Na wakati tunafanya vile, tunaonyesha kama tunamutumainia kabisa, “Ule Mwenye kuwa mukamilifu katika ujuzi.” (Yob. 36:4) Ni kweli kama leo kuko mambo yenye hatujue, lakini tunajua kama Yehova ataendelea kutufundisha milele mambo mingi ya mupya, na tutaendelea kujifunza mambo mingi juu ya Mungu wetu Mukubwa.—Muh. 3:11.

TUMEJIFUNZA NINI?

  • Juu ya nini ni muzuri vile hatujue siku mwisho itafika?

  • Juu ya nini haiko lazima tujue bya kesho juu tukuwe na furaha?

  • Juu ya nini ni muzuri tuelewe kama Yehova anatujua muzuri sana?

WIMBO 104 Baba, Unipatie Roho Yako Takatifu

a Juu Yesu njo ataongoza vita ya kuharibu ulimwengu wa Shetani, ni wazi kama sasa anajua siku Armagedoni itafika na wakati wenye ‘atakamilisha ushindi wake.’—Ufu. 6:2; 19:11-16.

b MAFASIRIO YA PICHA : Baba na mutoto yake banatia bitu mu sakoshi juu familia yabo ikuwe tayari kama kunatokea hali fulani yenye inaomba kutenda kwa haraka.

c MAFASIRIO YA PICHA : Ndugu mwenye iko na magumu iko nafikiria furaha yenye atakuwa nayo mu dunia mupya.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2026)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine