Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w25 Mwezi wa 9 uku. 20-25
  • Benye Biko na “Muelekeo Wenye Kufaa” Bataitika Kweli

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Benye Biko na “Muelekeo Wenye Kufaa” Bataitika Kweli
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • WAKATI BATU BANAPENDEZWA
  • WAKATI UNAANZA KUJIFUNZA BIBLIA NA MUTU
  • WAKATI MUTU ANAANZA KUKUSANYIKA NA SIYE
  • Maamuzi Yenye Inaonyesha Kama Tunamutegemea Yehova
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2023
  • Namna ya Kufurahia Zaidi Mahubiri
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2024
  • Itika Kama Kuko Mambo Yenye Haujue
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
  • Kukaribia Bandugu na Badada Yetu Ni Jambo ya Muzuri Kwetu!
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
w25 Mwezi wa 9 uku. 20-25

HABARI YA KUJIFUNZA YA 39

WIMBO 54 “Hii Ndiyo Njia”

Benye Biko na “Muelekeo Wenye Kufaa” Bataitika Kweli

“Wote wenye walikuwa na muelekeo wenye kufaa kwa ajili ya uzima wa milele wakakuwa waamini.”—MDO. 13:48.

WAZO KUBWA

Kujua wakati wa kuanzisha funzo ya Biblia na kualika batu ku mikutano yetu.

1. Batu banatenda namna gani wakati banasikia habari njema? (Matendo 13:​47, 48; 16:​14, 15)

MU KARNE ya kwanza, batu mingi balikubali kweli wakati tu baliisikia. (Soma Matendo 13:​47, 48; 16:​14, 15.) Leo pia, batu fulani banafurahi wakati tu banasikia habari njema kwa mara ya kwanza. Hata benye ku mwanzo habakupendezwa na ujumbe wetu, kisha wakati banaweza kufungula moyo wao na kukubali kweli. Tunapaswa kufanya nini wakati tunapata batu benye kuwa na “muelekeo wenye kufaa” mu mahubiri?

2. Ni mu njia gani kazi yetu ya kufanya banafunzi iko sawa vile kazi ya mulimaji?

2 Tunaweza kufananisha kazi yetu ya kuhubiri na kazi ya mulimaji. Kama mu shamba yake muko byenye binakomala, anabivuna kwanza, lakini anaendelea kuhangaikia byenye habiyakomala. Na siye, wakati tunapata mutu mwenye anaitika habari njema, tunamusaidia bila kukawia akuwe mwanafunzi wa Kristo. Lakini, tunaendelea pia kusaidia bale benye habayakuwa tayari kujifunza baelewe juu ya nini ni jambo ya maana bajifunze Biblia. (Yoh. 4:​35, 36) Inaomba utambuzi juu tujue nani njo iko tayari kuanza kujifunza na nani njo inaomba kusaidia zaidi. Tuone sasa mambo yenye tunaweza kufanya wakati tunazungumuza kwa mara ya kwanza na batu benye banapendezwa. Tutaona pia namna tutabasaidia bafanye maendeleo.

WAKATI BATU BANAPENDEZWA

3. Tunaweza kufanya nini wakati tunakutana na mutu mwenye anapendezwa? (1 Wakorinto 9:26)

3 Mu mahubiri wakati tunakutana na mutu mwenye anapendezwa, tunapenda kumusaidia bila kukawia juu aingie mu barabara yenye inaongoza ku uzima. Tusijizuie kuanzisha naye funzo ya Biblia na kumualika ku mikutano mara tu ya kwanza yenye tunazungumuza naye.—Soma 1 Wakorinto 9:26.

4. Leta mufano wa mutu mwenye alikuwa tayari kujifunza Biblia palepale.

4 Tuanzishe funzo. Batu fulani benye tunakutana mu mahubiri banakuwaka tayari kuanza kujifunza palepale. Kwa mufano, mu Kanada, siku moya mwanamuke fulani kijana alikaribia prezantware na akakamata broshua Furahia Maisha Milele! Ilikuwa siku ya ine. Dada mwenye alikuwa ku prezantware alimuambia kama anaweza kuanza kujifunza Biblia bila kulipa kwa kutumia ile broshua. Ule kijana mwanamuke alipendezwa na akapatia ule dada nimero yake ya telefone. Ileile siku, ule mwanamuke aliandikia ule dada na kumuuliza ni wakati gani njo bataanza kujifunza. Ule dada alimuambia kama banaweza anza mwisho wa juma, kisha ule kijana mwanamuke akasema: “Halafu kesho? Niko na wakati.” Balianza kujifunza Siku ya Tano. Na ileile juma, ule mwanamuke alifika kwa mara ya kwanza ku mikutano yetu ya mwisho wa juma na akafanya maendeleo ya haraka.

5. Namna gani tunaweza kuonyesha utambuzi wakati tunataka kuanzisha funzo ya Biblia? (Ona pia picha.)

5 Kusema kweli, haiko kila mutu njo ataitika kutusikiliza palepale sawa vile ule mwanamuke. Kuko benye biko na lazima ya wakati zaidi. Pengine itaomba kwanza kuzungumuzia habari yenye inafurahisha mutu. Tusiwaze kama ule mutu hataitikaka kujifunza, tuendelee tu kumuhangaikia, na pengine kisha wakati kidogo anaweza kuitika kuanza kujifunza. Tunaweza kusema nini wakati tunapenda kuanzisha funzo ya Biblia na mutu? Tuone vile bahubiri fulani benye biko na ufundi ya kuanzisha mafunzo ya Biblia balijibia ile ulizo.

Picha: 1. Bandugu bawili biko nazungumuza na mwanaume mwenye kukomala inje ya nyumba yake. 2. Badada bawili banatolea mwanamuke moya broshua “Furahia Maisha Milele!” banasimama inje ku mulango yake. Ule mwanamuke anabeba mutoto wake mudogo na mutoto wake mwingine anasimama pembeni yake.

Tunaweza kusema nini juu ya kusaidia batu benye niko ku hizi picha bafurahie kujifunza Biblia? (Ona fungu ya 5)a


6. Tunaweza kusema nini juu mutu aone kama kujifunza Biblia kutamusaidia?

6 Bahubiri na bapainia benye baliulizwa maulizo kuhusu kuanzisha mafunzo ya Biblia balisema kama, mu maeneo fulani wakati tuko nazungumuzia funzo ya Biblia, ni muzuri kuepuka kutumia maneno sawa vile “funzo ya Biblia,” ao “kukufundisha.” Aseme ni muzuri zaidi kutumikisha maneno sawa vile “maongezi,” “mazungumuzo,” ao “kujua Biblia.” Juu mutu apende kuzungumuza na siye siku ingine, tunaweza kutumia maneno sawa vile, “Inashangaza kuona vile Biblia inajibia maulizo ya maana yenye batu banajiulizaka,” ao “Biblia haizungumuzie tu mambo ya dini, inaweza kutusaidia mu maisha ya kila siku.” Unaweza kuongezea hivi: “Haiombe hata wakati mingi; unaweza kujifunza kitu fulani ya maana mu dakika 10 ao 15 tu.” Tunaweza kusema vile bila kuambia musikilizaji kama tutakuwa namurudilia “kila juma,” juu asiwaze kama analazimika kuzungumuza na siye kila wakati.

7. Ni wakati gani njo batu fulani banaelewa kama bamepata kweli? (1 Wakorinto 14:​23-25)

7 Ubaalike ku mikutano. Inaonekana kama wakati wa Paulo, batu fulani balielewa kama bamepata kweli wakati balifika ku mikutano ya Kikristo. (Soma 1 Wakorinto 14:​23-25.) Na leo ni vile. Mara mingi bapya banafanyaka maendeleo haraka wakati banaanza kukusanyika. Ni wakati gani njo tunapaswa kualika mutu ku mikutano? Mu kitabu Furahia Maisha Milele! ni mu somo ya 10 njo mwanafunzi anaalikwa ku mikutano. Lakini haiko lazima ungoye mufike mu ile somo juu umualike. Wakati uko nazungumuza naye mara tu ya kwanza, unaweza kumualika ku mukutano wa mwisho wa juma. Umuambie tungo ya hotuba ao jambo fulani yenye itazungumuziwa mu funzo ya Munara wa Mulinzi.

8. Tunaweza kuambia mutu nini kuhusu mikutano yetu wakati tunamualika? (Isaya 54:13)

8 Wakati tunaalika mutu mwenye kupendezwa, tumufasirie kama mambo yenye tunafanyaka ku mikutano yetu iko tofauti na mambo yenye makanisa ingine inafanyaka. Wakati mwanafunzi fulani wa Biblia alijionea funzo ya Munara wa Mulinzi mara ya kwanza, aliuliza hivi dada mwenye alikuwa najifunza naye Biblia: “Mwenye iko naongoza anajua jina ya kila mutu?” Ule dada alimuambia kama siye bote tunajikazaka kujua majina ya batu ya mu kutaniko yetu, sawa vile tu tunajuaka majina ya batu ya mu familia yetu. Ule mwanafunzi aliona kama ile ilikuwa tofauti na mu kanisa yake, habajuanake hata majina. Zaidi ya ile, tufasirie mwanafunzi juu ya nini tunakusanyikaka. (Soma Isaya 54:13.) Tunakusanyika juu ya kumuabudu Yehova, kujifunza juu yake, na kutiana moyo. (Ebr. 2:12; 10:​24, 25) Njo maana mikutano yetu inapangwa muzuri juu tuweze kujifunza, na hakukuwake madesturi-desturi. (1 Ko. 14:40) Majumba yetu ya Ufalme haikuwake na bya mingimingi, na inajengwa mu namna yenye inafanya ikuwe mwepesi kwetu kujifunza. Tena, ku mikutano yetu hatuchochee batu baunge mukono upande fulani mu mambo ya politike; na hatufanyake mabishano juu ya kutetea mawazo yetu ya kipekee. Inaweza kuwa muzuri kuonyesha mwanafunzi mbele ya wakati video, Kwa Kawaida Tunafanya Nini Kwenye Jumba la Ufalme? Ile itamusaidia ajue mbele ya wakati mambo yenye itapitikana ku mukutano.

9-10. Wakati tunaalika mutu ku mikutano tunaweza kumuambia nini juu asiogope kufika? (Ona pia picha.)

9 Batu fulani banasita kuya ku mikutano yetu juu banaogopa kama tutabaambia bakuwe Mashahidi wa Yehova. Hakikishia mutu kama akikuya, halazimike kusema ao kufanya jambo fulani, anaweza tu kuya kusikiliza na basi. Tunakaribisha mafamilia, hata benye biko na batoto badogo-dogo. Ku mikutano yetu hakuna mafundisho ya batoto tu. Bazazi na batoto banaikala pamoya na banajifunza pamoya. Ile inasaidia bazazi bajue kama batoto yabo biko salama, na bajue byenye batoto yabo biko nafundishwa. (Kum. 31:12) Hatulombake sadaka na hatupitishake kitunga ya kutia ndani makuta. Lakini, tunafuata hii amri ya Yesu: “Mulipokea bure, mutoe bure.” (Mt. 10:8) Unaweza pia kuambia mutu kama haiko lazima akuye navala manguo ya bei. Mungu anaangaliaka njo moyo.—1 Sa. 16:7.

10 Kama mutu anafika ku mikutano, ufanye ajisikie kuwa anakaribishwa sana. Ambia bazee fulani na bandugu na dada bamusalimie. Kama anaona banamukaribisha muzuri, atapenda kuya tena siku ingine. Kama hana Biblia, musome pamoya mu Biblia yako, na umusaidie afuatane na musemaji na ajue kwenye tuko mu funzo ya Munara wa Mulinzi.

Mwanamuke mwenye tuliona ku picha ya kutangulia anafurahia namna bandugu na dada banamukaribisha kwa furaha ku Jumba ya Ufalme. Anabeba mutoto wake mudogo na mutoto wake mwingine iko nazungumuza na mutoto mwingine.

Kama mutu anaanza kukusanyika bila kukawia, atafanya pia maendeleo bila kukawia (Ona fungu ya 9-10)


WAKATI UNAANZA KUJIFUNZA BIBLIA NA MUTU

11. Namna gani unaweza kuonyesha kama unaheshimia programe na wakati ya musikilizaji wako?

11 Unapaswa kukumbuka nini wakati unaanza kujifunza Biblia na mutu? Uheshimie programe yake na wakati yake. Kwa mufano, kama mulisikilizana mutaanza kujifunza saa fulani, ufike ile saa hata kama kwenye unaishi batu habafikake kwa wakati. Tena, siku ya kwanza ya funzo, ni muzuri musijifunze wakati murefu. Bahubiri fulani benye uzoefu banasema kama ni muzuri kumaliza mbio, hata kama mutu anapenda muendelee. Na usiseme mingi. Acha musikilizaji aseme mawazo yake.—Mez. 10:19.

12. Tunapaswa kufanya nini wakati tunaanza kujifunza Biblia na mutu?

12 Wakati tu tunaanza kujifunza na mutu, tunapaswa kumusaidia amujue Yehova na Yesu na abapende. Tunaweza kufanya vile kwa kumufundisha mambo yenye iko mu Biblia, hapana mawazo yetu. (Mdo. 10:​25, 26) Wakati mutume Paulo alikuwa nafundisha, mara mingi alikuwa nazungumuzia Yesu, mwenye Yehova alituma juu atusaidie kumujua na kumupenda. (1 Ko. 2:​1, 2) Tena Paulo alionyesha wazi kama ni jambo ya maana kusaidia banafunzi ba mupya bakomalishe sifa za muzuri, zenye Biblia inafananisha na zahabu, feza, na majiwe ingine ya bei. (1 Ko. 3:​11-15) Kati ya zile sifa kuko imani, hekima, utambuzi na kumuogopa Mungu. (Zb. 19:​9, 10; Mez. 3:​13-15; 1 Pe. 1:7) Umuige Paulo kwa kusaidia banafunzi yako bakuwe na imani yenye nguvu na bakuwe na urafiki wa karibu pamoya na Baba yabo wa mbinguni mwenye upendo.—2 Ko. 1:24.

13. Namna gani tunaweza kuonyesha uvumilivu na kuonyesha kama tunaelewa mutu mwenye tuko najifunza naye? (2 Wakorinto 10:​4, 5) (Ona pia picha.)

13 Iga namna ya Yesu ya kufundisha kwa kujikaza kuwa muvumilivu na kwa kujikaza kuelewa mutu. Uepuke kumuuliza maulizo yenye itafanya asikie haya. Tena, kama haiko mwepesi kwake kuelewa wazo fulani, inaweza kuwa muzuri kuitambuka kwanza na kuizungumuzia wakati ingine. Kama mwanafunzi hayakuwa tayari kuitika fundisho fulani ya Biblia tusimukaze, tumuachie wakati juu kweli itie mizizi mu moyo wake. (Yoh. 16:12; Kol. 2:​6, 7) Biblia inasema kama mafundisho ya bongo iko sawa vile “mambo yenye yametia mizizi kabisa” yenye tunapaswa “kupindua.” (Soma 2 Wakorinto 10:​4, 5) Inaweza kuwa nguvu kwa mwanafunzi kuachana na mambo yenye anaamini tangu zamani, njo maana tunapaswa kwanza kumusaidia akuwe na urafiki wa karibu pamoya na Yehova, kama tunafanya vile itakuwa mwepesi kwake kuachana na mafundisho yenye ilishatia mizizi mu moyo wake.—Zb. 91:9.

Ule mwanaume mwenye kukomala wa ku picha ya kutangulia iko najifunza kitabu “Furahia Maisha Milele!” pamoya na bandugu bawili. Ku kabati yenye iko pembeni yabo kuko mapete ya mu jeshi.

Acha wakati ipite juu kweli za Biblia zitie mizizi mu moyo (Ona fungu ya 13)


WAKATI MUTU ANAANZA KUKUSANYIKA NA SIYE

14. Namna gani tunapaswa kutendea mutu mwenye anaanza kukusanyika na siye?

14 Yehova anapenda tutendee muzuri mutu mwenye anaanza kukusanyika, ikuwe ni wa desturi gani, ni maskini ao tajiri, ao ikuwe anatoka wapi. (Yak. 2:​1-4, 9) Wakati mutu anaanza kukusanyika na siye, namna gani tunaweza kuonyesha kama tunamupenda?

15-16. Tunaweza kufanya nini juu ya kusaidia batu benye banafika ku mikutano yetu bajisikie muzuri?

15 Batu fulani banakuyaka ku mikutano yetu juu tu banapenda kuona namna mikutano yetu inafanyikaka, ao pengine mutu mwenye anaishi fasi ingine alibatia moyo bafike ku mikutano yetu. Njo maana kama unaona mutu wa mupya ku mikutano, uende uzungumuze naye. Umukaribishe lakini usipitishe mipaka. Umuombe aikale na weye. Kama hana Biblia ao kitabu yenye muko natumikisha ku mukutano, umuombe afuate na weye ao umupatie yake. Na kama kuko mambo ingine yenye unaweza fanya juu ajisikie muzuri, uifanye. Kwa mufano, mwanaume fulani mwenye alifika ku mikutano yetu, aliambia ndugu moya mwenye alimukaribisha kama hakukuwa najisikia muzuri juu yeye hakukuwa navala namna tunavalaka ku mikutano. Ule ndugu alimusaidia asijihangaishe na akamuambia kama siye Mashahidi wa Yehova tuko tu sawa batu bengine. Ule mwanaume alifanya maendeleo na akabatizwa, na angali nakumbuka maneno ya ule ndugu. Sawa vile tunaona, ni muzuri kuhangaikia mutu wa mupya mwenye anafika ku mikutano yetu, lakini tufanye angalisho: Wakati tuko naongea naye mbele ao kisha mikutano, tusijiingize mu mambo yake ya kipekee.—1 Pe. 4:15.

16 Kuko jambo ingine yenye tunaweza kufanya juu ya kusaidia batu benye banafika ku mikutano yetu bajisikie muzuri. Kama mu mazungumuzo yetu, mu majibu yetu, ao mu kipindi yenye tutafanya tutazungumuzia batu benye habiko Mashahidi, tufanye vile kwa heshima. Tuepuke kubachambua-chambua ao kutumia maneno yenye inaweza kubakwaza. (Tit. 2:8; 3:2) Kwa mufano, tunaepuka kusema mubaya juu ya mambo yenye banaamini. (2 Ko. 6:3) Bandugu benye banatoaka hotuba banapaswa kuwa baangalifu sana juu ya ile. Ni muzuri pia bakuwe banafasiria maneno yenye batu benye habiko Mashahidi banaweza kuwa na magumu ya kuelewa.

17. Kusudi yetu ni nini wakati tunapata batu benye kuwa na “muelekeo wenye kufaa” mu mahubiri?

17 Vile masiku iko napita, njo vile kazi yetu ya kufanya banafunzi iko nakuwa ya haraka. Tuko naendelea kutafuta batu benye kuwa na “muelekeo wenye kufaa kwa ajili ya uzima wa milele.” (Mdo. 13:48) Na wakati tunabapata, tusijizuie kuanzisha funzo ya Biblia ao kubaalika ku mikutano yetu. Kama tunafanya vile, tutabasaidia baanze kutembea mu “barabara yenye kuongoza kwenye uzima.”—Mt. 7:14.

UTAJIBU NAMNA GANI?

  • Namna gani tunaweza kusaidia batu benye kuwa na “muelekeo wenye kufaa” wakati tunazungumuza nabo mara ya kwanza?

  • Tunaweza kufanya nini juu ya kusaidia mutu wakati tu tunaanza kujifunza naye?

  • Tunaweza kufanya nini juu ya kusaidia bale benye banafika ku mikutano yetu bajisikie muzuri?

WIMBO 64 Kufanya Kazi ya Mavuno kwa Furaha

a MAFASIRIO YA PICHA : Bandugu bawili biko nazungumuza na mwanaume mwenye alikuwaka askari zamani mwenye iko napumuzika mbele ya kwake. Badada bawili biko nahubiria kwa kifupi mama mwenye iko na mambo mingi ya kufanya.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine