MUENDELEE KUKESHA!
Biblia Inasema Nini Juu ya Kuabudu Sanamu?
Kulingana na shirika ya habari Catholic News Service, wakati ya misa yenye ilifanywa tarehe 25, Mwezi wa 3, 2022 ku kanisa ya Saint-Pierre, Papa François alisimama mbele ya sanamu ya Maria “na amefunga macho na kuinamisha kichwa, na iko nasali kimya-kimya.” “Alimulilia Maria” alete amani. Habari fulani mu gazeti Vatican News iliongezea kama “Papa alisali ili kutia wanadamu wote mu moyo safi wa Maria, zaidi sana wakaaji wa Urusi na Ukraine.”
Unawaza nini? Inafaa kabisa kusali mbele ya sanamu ao kuzitumia juu ya kumuabudu Mungu? Fikiria maandiko yenye kufuata:
“Haupaswe kujifanyia sanamu ya kuchongwa wala umbo ya kitu fulani chenye kuwa juu mbinguni wala chenye kuwa hapa chini juu ya dunia wala chenye kuwa ndani ya maji chini ya dunia. Haupaswe kuviinamia wala kushawishiwa kuvitumikia, kwa sababu mimi, Yehova Mungu wako, ni Mungu mwenye anataka watu washikamane na yeye tu.”—Kutoka 20:4, 5.a
“Sanamu zao ni feza na zahabu, kazi ya mikono ya mwanadamu. Ziko na kinywa, lakini haziwezi kusema; ziko na macho, lakini haziwezi kuona; ziko na masikio, lakini haziwezi kusikia; ziko na pua, lakini haziwezi kunusa; ziko na mikono, lakini haziwezi kugusa; ziko na miguu, lakini haziwezi kutembea; hazitoe sauti yoyote kwa koo yao. Watu wenye kuzitengeneza watakuwa kama vile sanamu hizo, na wale wote wenye kuzitegemea.”—Zaburi 115:4-8.
“Mimi ni Yehova. Hilo ndilo jina langu; sitachangia utukufu wangu na mutu yeyote, wala sipatie sanamu za kuchongwa sifa yangu.”—Isaya 42:8, maelezo ya chini.
“Mukimbie ibada ya sanamu.”—1 Wakorinto 10:14.
“Mujiepushe na sanamu.”—1 Yohana 5:21.
Juu ya kujua mambo mingi zaidi kuhusu mambo yenye Biblia inasema juu ya kutumia sanamu mu ibada, soma habari “Mawazo ya Biblia—Sanamu” ao uangalie video Mungu Anapendaka Tutumie Sanamu Wakati Tuko Tunamuabudu?
Unaweza pia kufurahia mambo yenye Biblia inasema juu ya habari zenye kufuata:
Kwenye tulitosha picha: Vincenzo Pinto/AFP via Getty Images
a Yehova njo jina ya pekee ya Mungu. (Zaburi 83:18) Ona habari “Yehova Ni Nani?”