Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • ijwbq habari 79
  • Ufalme wa Mungu Uko mu Moyo Wako?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Ufalme wa Mungu Uko mu Moyo Wako?
  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Jibu ya Biblia
  • Je, Ufalme wa Mungu Ni Hali ya Moyoni Tu?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Ufalme Wa Mungu
    Amuka!—2013
  • Kweli Kuhusu Ufalme wa Mungu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2020
  • Ufalme wa Mungu Ni Nini?
    Mungu Anataka Nini Kwetu?
Ona Habari Zaidi
Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
ijwbq habari 79
Muchoro wa mwili wa mwanadamu, hakuna serikali halisi yenye inaweza kuwa ndani yake

Ufalme wa Mungu Uko mu Moyo Wako?

Jibu ya Biblia

Hapana, Ufalme wa Mungu hauko mu moyo wa Wakristo.a Biblia inaonyesha kwenye Ufalme wa Mungu uko wakati inauita kuwa “ufalme wa mbinguni.” (Matayo 4:17, La Sainte Bible en swahili de la R.D.Congo) Ona namna Biblia inaonyesha kama Ufalme wa Mungu ni serikali ao guvernema yenye iko natawala ikiwa mbinguni.

  • Ufalme wa Mungu uko na watawala, watu wenye utatawala, sheria, na kusudi. Kusudi yake ni kutimiza mapenzi ya Mungu mbinguni na ku dunia.​—Matayo 6:10; Ufunuo 5:10.

  • Ufalme wa Mungu utatawala “vikundi vya watu, mataifa, na vikundi vya luga” vya mu dunia yote. (Danieli 7:13, 14) Mamlaka ya Ufalme wa Mungu haitoke kwa watu, lakini inatoka kwa Mungu.​—Zaburi 2:4-6; Isaya 9:7.

  • Yesu aliambia mitume wake waaminifu kama watakuwa pamoya naye mu Ufalme wa mbinguni ili ‘wakae kwenye viti vya ufalme.’​—Luka 22:28, 30.

  • Ufalme wa Mungu uko na maadui, na utawaharibu.​—Zaburi 2:1, 2, 8, 9; 110:1, 2; 1 Wakorinto 15:25, 26.

Biblia haifundishe kama Ufalme wa Mungu unatawala ndani ya moyo wa mutu. Lakini, inafundisha kama “neno la Ufalme” ao “habari njema ya Ufalme” inaweza kugusa mioyo yetu na inapaswa kufanya vile.​—Matayo 13:19; 24:14.

Maneno “ufalme wa Mungu umo ndani yenu,” maana yake nini?

Watu fulani wanashindwa kuelewa fasi kwenye Ufalme wa Mungu uko juu ya namna tafsiri fulani za Biblia zinatafsiri Luka 17:21. Kwa mufano, tafsiri Union Version inatafsiri ile andiko hivi: “Ufalme wa Mungu umo ndani yenu.” Juu tuelewe muzuri ile andiko, tunapaswa kufikiria ni watu gani Yesu aliambia ile maneno.

Viongozi fulani wa dini wenye walikuwa namupinga Yesu

Ufalme wa Mungu haukukuwa ndani ya mioyo ya watu wabaya na wenye walikuwa napenda kumuua Yesu

Yesu alikuwa nazungumuza na Wafarisayo, viongozi wa dini wenye walikuwa namupinga na wenye walikuwa natafuta kumuua. (Matayo 12:14; Luka 17:20) Unawaza kabisa Ufalme wa Mungu ulikuwa mu mioyo ya wale watu wabaya? Yesu aliwaambia hivi: “Mumejaa unafiki na uvunjaji wa sheria.”​—Matayo 23:27, 28.

Tafsiri zingine zinatafsiri muzuri maneno ya Yesu mu Luka 17:21: “Ufalme wa Mungu uko kati yenu.” (Italiki ni zetu; Habari Njema) “Ufalme wa Mungu uko katikati yenu.” (Tafsiri ya Ulimwengu Mupya) Ufalme wa Mungu ulikuwa “kati” ao “katikati ya” Wafarisayo, juu Yesu, mwenye angekuwa Mufalme wa Ufalme wa Mungu alikuwa katikati yao.​—Luka 1:32, 33.

a Dini za mingi za Kikristo zinafundishaka kama Ufalme wa Mungu uko mu moyo wa mutu. Kwa mufano, mu Amerika, Kanisa ya Kibatisti ya Kusini ilisema kama Ufalme wa Mungu ni sehemu ya “utawala wa Mungu mu moyo na mu maisha ya mutu.” Vilevile, mu kitabu Jesus of Nazareth, Papa Benedikto wa 16, alisema kama “Ufalme wa Mungu unakuya wakati tuko na moyo mutiifu.”

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2026)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine