Siku ya Tano, 10 Mwezi wa 10
Kumuogopa Yehova ndio mwanzo wa hekima.—Mez. 9:10.
Mukristo anapaswa kufanya nini kama anaona picha ya pornografia bila kutazamia? Anapaswa kuacha kuiagalia palepale. Jambo yenye inaweza kutusaidia kufanya vile ni kukumbuka kama urafiki wetu pamoya na Yehova njo jambo ya maana sana. Vilevile, hata picha fulani zenye zinaweza kuonekana sawa vile hazifanane picha za pornografia, zinaweza kulamusha tamaa ya kufanya uasherati. Juu ya nini tunapaswa kuziepuka? Juu hatupendi hata kidogo kufanya uzinifu mu moyo wetu. (Mt. 5:28, 29) David, muzee wa mu Tailandi anasema hivi: “Najiulizaka hivi: ‘Hata kama hizi picha hazifanane picha za pornografia, Yehova atafurahi kama naendelea kuziangalia?’ Kujiuliza vile kunanisaidiaka nitende kwa hekima.” Kuogopa kufanya jambo yoyote yenye itamuhuzunisha Yehova kutatusaidia tutende kwa hekima. Kumuogopa Mungu njo “mwanzo” ao musingi “wa hekima.” w23.06 23 fu. 12-13
Siku ya Posho, 11 Mwezi wa 10
Muende, watu wangu, muingie katika vyumba vyenu vya ndani.—Isa. 26:20.
‘Vyumba vya ndani’ vinaweza kumaanisha makutaniko. Wakati wa taabu kubwa, tutapata ulinzi wenye Yehova anatuahidi kama tunaendelea kuungana na waamini wenzetu. Njo maana, kwa sasa, tunapaswa kujikaza sana kuvumilia ndugu na dada zetu lakini pia kuwapenda. Ile njo inaweza kufanya tuokoke! “Ile siku kubwa ya Yehova” itakuwa kipindi ya nguvu sana kwa wanadamu wote. (Sef. 1:14, 15) Watu wa Yehova watakuwa pia na magumu. Lakini, kama tunajitayarisha sasa, tutakuwa wenye kutulia na tutasaidia wengine. Tutavumilia magumu yote yenye tutakutana nayo. Wakati ndugu na dada zetu wanateseka, tutafanya yote yenye tunaweza ili kuwasaidia kwa kuwaonyesha huruma na kuwatolea musaada wenye wako nayo lazima. Na kama tunajifunza kupenda ndugu na dada zetu leo, tutaendelea kuwapenda hata wakati wenye kuya. Na ku mwisho, Yehova atatubariki kwa kutupatia uzima wa milele ku dunia kwenye misiba yote na taabu yote itakuwa ilishasahauliwa.—Isa. 65:17. w23.07 7 fu. 16-17
Siku ya Yenga, 12 Mwezi wa 10
[Yehova] atawafanya kuwa imara, atawatia nguvu, atawafanya ninyi musitikisike.—1 Pe. 5:10.
Mara mingi wakati Neno ya Mungu inazungumuzia watu waaminifu wa zamani, inasema kama walikuwa wenye nguvu. Lakini wakati fulani hata wenye nguvu zaidi kati yao, hawakujisikia kuwa na nguvu. Kwa mufano, wakati fulani Mufalme Daudi alijisikia kuwa “imara kama mulima,” lakini wakati mwingine “aliogopa sana.” (Zb. 30:7) Hata kama Samsoni alikuwa na nguvu mingi sana wakati alikuwa naongozwa na roho ya Mungu, alisema kama bila nguvu yenye kutoka kwa Mungu “atakuwa muzaifu na kuwa kama wanadamu wengine wote.” (Amu. 14:5, 6; 16:17) Wale wanaume waaminifu walikuwa wenye nguvu kwa sababu tu Yehova aliwapatia nguvu. Mutume Paulo alikubali kama alikuwa na lazima ya nguvu kutoka kwa Yehova. (2 Ko. 12:9, 10) Alipambana na magumu ya afya. (Gal. 4:13, 14) Wakati fulani, ilikuwa nguvu kwake kufanya mambo ya muzuri. (Ro. 7:18, 19) Na wakati ingine alikuwa na mahangaiko na hakujua ni nini itamufikia. (2 Ko. 1:8, 9) Hata vile, wakati Paulo alikuwa muzaifu, njo wakati alikuwa mwenye nguvu. Namna gani? Yehova alimupatia Paulo nguvu yenye alikuwa nayo lazima. Alimutia nguvu. w23.10 12 fu. 1-2