Siku ya Posho, 11 Mwezi wa 10
Muende, watu wangu, muingie katika vyumba vyenu vya ndani.—Isa. 26:20.
‘Vyumba vya ndani’ vinaweza kumaanisha makutaniko. Wakati wa taabu kubwa, tutapata ulinzi wenye Yehova anatuahidi kama tunaendelea kuungana na waamini wenzetu. Njo maana, kwa sasa, tunapaswa kujikaza sana kuvumilia ndugu na dada zetu lakini pia kuwapenda. Ile njo inaweza kufanya tuokoke! “Ile siku kubwa ya Yehova” itakuwa kipindi ya nguvu sana kwa wanadamu wote. (Sef. 1:14, 15) Watu wa Yehova watakuwa pia na magumu. Lakini, kama tunajitayarisha sasa, tutakuwa wenye kutulia na tutasaidia wengine. Tutavumilia magumu yote yenye tutakutana nayo. Wakati ndugu na dada zetu wanateseka, tutafanya yote yenye tunaweza ili kuwasaidia kwa kuwaonyesha huruma na kuwatolea musaada wenye wako nayo lazima. Na kama tunajifunza kupenda ndugu na dada zetu leo, tutaendelea kuwapenda hata wakati wenye kuya. Na ku mwisho, Yehova atatubariki kwa kutupatia uzima wa milele ku dunia kwenye misiba yote na taabu yote itakuwa ilishasahauliwa.—Isa. 65:17. w23.07 7 fu. 16-17
Siku ya Yenga, 12 Mwezi wa 10
[Yehova] atawafanya kuwa imara, atawatia nguvu, atawafanya ninyi musitikisike.—1 Pe. 5:10.
Mara mingi wakati Neno ya Mungu inazungumuzia watu waaminifu wa zamani, inasema kama walikuwa wenye nguvu. Lakini wakati fulani hata wenye nguvu zaidi kati yao, hawakujisikia kuwa na nguvu. Kwa mufano, wakati fulani Mufalme Daudi alijisikia kuwa “imara kama mulima,” lakini wakati mwingine “aliogopa sana.” (Zb. 30:7) Hata kama Samsoni alikuwa na nguvu mingi sana wakati alikuwa naongozwa na roho ya Mungu, alisema kama bila nguvu yenye kutoka kwa Mungu “atakuwa muzaifu na kuwa kama wanadamu wengine wote.” (Amu. 14:5, 6; 16:17) Wale wanaume waaminifu walikuwa wenye nguvu kwa sababu tu Yehova aliwapatia nguvu. Mutume Paulo alikubali kama alikuwa na lazima ya nguvu kutoka kwa Yehova. (2 Ko. 12:9, 10) Alipambana na magumu ya afya. (Gal. 4:13, 14) Wakati fulani, ilikuwa nguvu kwake kufanya mambo ya muzuri. (Ro. 7:18, 19) Na wakati ingine alikuwa na mahangaiko na hakujua ni nini itamufikia. (2 Ko. 1:8, 9) Hata vile, wakati Paulo alikuwa muzaifu, njo wakati alikuwa mwenye nguvu. Namna gani? Yehova alimupatia Paulo nguvu yenye alikuwa nayo lazima. Alimutia nguvu. w23.10 12 fu. 1-2
Siku ya Kwanza, 13 Mwezi wa 10
Yehova anaona ndani ya moyo.—1 Sa. 16:7.
Ikiwa wakati fulani tunajiona kuwa watu wa bure, tukumbuke kama ni Yehova njo alituvuta kwake. (Yoh. 6:44) Anaona jambo fulani ya muzuri ndani yetu, jambo fulani yenye pengine siye wenyewe hatuone, na anajua moyo wetu. (2 Ny. 6:30) Kwa hiyo tunaweza kumuamini wakati anasema kama tuko wa maana. (1 Yo. 3:19, 20) Mbele ya kujifunza kweli, wamoja kati yetu walifanya mambo yenye pengine wanaendelea kuhuzunikia mupaka leo. (1 Pe. 4:3) Hata Wakristo waaminifu wanapiganisha muelekeo wa kufanya zambi. Moyo wako uko nakuhukumu? Kama ni vile, usivunjike moyo. Ujue kama hata watumishi fulani wa Yehova walijisikia vile. Kwa mufano, mutume Paulo alijiona kuwa wa bure wakati alifikiria uzaifu wake. (Ro. 7:24) Kwa kweli, Paulo alikuwa ametubu zambi zake na kubatizwa. Lakini, aliendelea kujiona kuwa “mudogo zaidi kati ya mitume” na mutenda-zambi “wa kwanza kabisa.”—1 Ko. 15:9; 1 Ti. 1:15. w24.03 27 fu. 5-6