Siku ya Posho, 18 Mwezi wa 10
Muendelee kuomba, na mutapewa; muendelee kutafuta, na mutapata; muendelee kupiga hodi, na watawafungulia.—Lu. 11:9.
Uko na lazima ya kuwa na uvumilivu zaidi? Kama ni vile, muombe Yehova akusaidie. Uvumilivu ni sehemu ya tunda ya roho. (Gal. 5:22, 23) Tunapaswa kumuomba Yehova atupatie roho yake takatifu na kumuomba atusaidie tukomalishe tunda ya ile roho. Kama tunajikuta mu hali yenye inatuomba tuonyeshe uvumilivu, tunapaswa “kuendelea kumuomba” Yehova roho takatifu ili tuonyeshe uvumilivu. (Lu. 11:13) Tunapaswa pia kumuomba atusaidie tuone mambo vile yeye anaiona. Na kisha kusali, tunapaswa kufanya yetu yote juu tuendelee kuwa wavumilivu kila siku. Kama tunaendelea kumuomba Yehova atusaidie tukuwe na uvumilivu na kama tunaendelea kufanya yetu yote juu ya kuonyesha ile sifa, atatusaidia tukuwe na uvumilivu zaidi hata kama hatukukuwaka na ile sifa zamani. Kutafakari juu ya mifano yenye kuwa mu Biblia kunaweza pia kusaidia. Mu Biblia muko mifano mingi ya watu wenye walikuwa na uvumilivu. Kama tunatafakari juu ya ile mifano, tunaweza kujifunza njia mbalimbali za kuonyesha uvumilivu. w23.08 22 fu. 10-11
Siku ya Yenga, 19 Mwezi wa 10
Mushushe nyavu zenu, muvue samaki.—Lu. 5:4.
Yesu alimuhakikishia mutume Petro kama Yehova atamuhangaikia. Yesu mwenye alikuwa amefufuliwa, alisaidia Petro na mitume wengine kukamata tena samaki kwa njia ya muujiza. (Yoh. 21:4-6) Bila shaka ule muujiza ulimuhakikishia Petro kama ni mwepesi kwa Yehova kumutolea vitu vya kimwili vyenye alikuwa navyo lazima. Pengine Petro alikumbuka namna Yesu alisemaka kama Yehova atatimiza mahitaji ya wale wenye “kutafuta kwanza Ufalme.” (Mt. 6:33) lle ilifanya Petro atie kazi ya kuhubiri pa nafasi ya kwanza, hapana kazi ya kuvua samaki. Kisha pale alitoa ushahidi kwa uhodari siku ya Pentekoste ya mwaka wa 33 K.K.Y., na akasaidia maelfu ya watu wakubali habari njema. (Mdo. 2:14, 37-41) Na kisha alisaidia Wasamaria na Watu wa Mataifa wakubali Kristo. (Mdo. 8:14-17; 10:44-48) Ni wazi kama Yehova alitumia Petro ili kuleta watu wa namna zote mu kutaniko. w23.09 20 fu. 1; 23 fu. 11
Siku ya Kwanza, 20 Mwezi wa 10
Kama hamunijulishe ndoto hiyo, pamoja na maana yake, mutakatwa vipande-vipande.—Da. 2:5.
Miaka mbili hivi kisha Wababiloni kuharibu Yerusalemu. Nebukadneza, Mufalme wa Babiloni alilota ndoto yenye ilimuogopesha kuhusu sanamu kubwa sana. Alisema kama ataua wanaume wote wenye hekima, kutia ndani Danieli kama wanashindwa kumuambia ndoto yake na kama wanashindwa kuifasiria. (Da. 2:3-5) Danieli alipaswa kutenda haraka, juu kama hangefanya vile, watu wengi wangekufa. Njo maana “aliingia na kumuomba mufalme amupatie wakati ili amufasirie mufalme maana yake.” (Da. 2:16) Ile ilionyesha kama Danieli alikuwa na uhodari na imani. Juu ya nini tunasema vile? Juu mu Biblia hamuna andiko yenye inaonyesha kama Danieli alikuwaka nafasiria ndoto zamani. Aliomba marafiki wake “wasali ili wapate rehema kutoka kwa Mungu wa mbinguni juu ya siri hiyo.” (Da. 2:18) Yehova alijibia sala zao. Kwa musaada wa Mungu, Danieli alifasiria ndoto ya Nebukadneza. Kwa kufanya vile, aliokoa uzima wake na wa marafiki wake. w23.08 3 fu. 4