Siku ya Yenga, 19 Mwezi wa 10
Mushushe nyavu zenu, muvue samaki.—Lu. 5:4.
Yesu alimuhakikishia mutume Petro kama Yehova atamuhangaikia. Yesu mwenye alikuwa amefufuliwa, alisaidia Petro na mitume wengine kukamata tena samaki kwa njia ya muujiza. (Yoh. 21:4-6) Bila shaka ule muujiza ulimuhakikishia Petro kama ni mwepesi kwa Yehova kumutolea vitu vya kimwili vyenye alikuwa navyo lazima. Pengine Petro alikumbuka namna Yesu alisemaka kama Yehova atatimiza mahitaji ya wale wenye “kutafuta kwanza Ufalme.” (Mt. 6:33) lle ilifanya Petro atie kazi ya kuhubiri pa nafasi ya kwanza, hapana kazi ya kuvua samaki. Kisha pale alitoa ushahidi kwa uhodari siku ya Pentekoste ya mwaka wa 33 K.K.Y., na akasaidia maelfu ya watu wakubali habari njema. (Mdo. 2:14, 37-41) Na kisha alisaidia Wasamaria na Watu wa Mataifa wakubali Kristo. (Mdo. 8:14-17; 10:44-48) Ni wazi kama Yehova alitumia Petro ili kuleta watu wa namna zote mu kutaniko. w23.09 20 fu. 1; 23 fu. 11
Siku ya Kwanza, 20 Mwezi wa 10
Kama hamunijulishe ndoto hiyo, pamoja na maana yake, mutakatwa vipande-vipande.—Da. 2:5.
Miaka mbili hivi kisha Wababiloni kuharibu Yerusalemu. Nebukadneza, Mufalme wa Babiloni alilota ndoto yenye ilimuogopesha kuhusu sanamu kubwa sana. Alisema kama ataua wanaume wote wenye hekima, kutia ndani Danieli kama wanashindwa kumuambia ndoto yake na kama wanashindwa kuifasiria. (Da. 2:3-5) Danieli alipaswa kutenda haraka, juu kama hangefanya vile, watu wengi wangekufa. Njo maana “aliingia na kumuomba mufalme amupatie wakati ili amufasirie mufalme maana yake.” (Da. 2:16) Ile ilionyesha kama Danieli alikuwa na uhodari na imani. Juu ya nini tunasema vile? Juu mu Biblia hamuna andiko yenye inaonyesha kama Danieli alikuwaka nafasiria ndoto zamani. Aliomba marafiki wake “wasali ili wapate rehema kutoka kwa Mungu wa mbinguni juu ya siri hiyo.” (Da. 2:18) Yehova alijibia sala zao. Kwa musaada wa Mungu, Danieli alifasiria ndoto ya Nebukadneza. Kwa kufanya vile, aliokoa uzima wake na wa marafiki wake. w23.08 3 fu. 4
Siku ya Pili, 21 Mwezi wa 10
Ule mwenye atavumilia mupaka mwisho ataokolewa.—Mt. 24:13.
Fikiria faida za kuwa na uvumilivu. Kama tuko na uvumilivu, tutakuwa na furaha zaidi na tutatulia zaidi. Kama tuko na uvumilivu, tunaweza kuwa na afya ya muzuri kimwili na kiakili. Kama tunavumilia wengine, tutakuwa na uhusiano wa muzuri zaidi pamoya nao. Kutaniko yetu itakuwa na umoja zaidi. Kama hatukasirike haraka wakati mutu fulani anatuchokoza, ile itafanya hali isiharibike zaidi. (Zb. 37:8, maelezo ya chini; Mez. 14:29) Lakini, zaidi ya yote, tutamuiga Baba yetu wa mbinguni na tutamukaribia hata zaidi. Uvumilivu ni sifa ya muzuri kabisa yenye inatuleteaka siye wote faida! Kusema kweli, haiko mwepesi kila mara kuwa na uvumilivu, lakini kwa musaada wa Yehova, tunaweza kuendelea kuonyesha ile sifa. Na vile tuko naendelea kungoya kwa uvumilivu dunia mupya, tuko hakika kama “jicho la Yehova linalinda wale wenye kumuogopa, wale wenye kungojea upendo wake mushikamanifu.” (Zb. 33:18) Tuazimie basi kuendelea kuvaa uvumilivu. w23.08 22 fu. 7; 25 fu. 16-17