Siku ya Tatu, 22 Mwezi wa 10
Imani yenyewe bila matendo imekufa.—Yak. 2:17.
Yakobo alionyesha kama mutu anaweza kusema kama iko na imani; lakini, je, matendo yake inaonyesha imani kabisa? (Yak. 2:1-5, 9) Yakobo anazungumuzia pia mutu mwenye anaona ‘ndugu ao dada anakosa nguo ao chakula’ lakini hamutolee musaada wenye iko nao lazima. Hata kama ule mutu anasema kama iko na imani, ile imani haionekane kupitia matendo; kwa hiyo, ile imani ni ya bure. (Yak. 2:14-16) Yakobo alizungumuzia Rahabu kuwa mufano muzuri wa kuonyesha imani kupitia matendo. (Yak. 2:25, 26) Rahabu alisikia habari kuhusu Yehova na akaamini kama ni Yehova njo alikuwa anategemeza Waisraeli. (Yos. 2:9-11) Alionyesha imani yake kupitia matendo. Alilinda wapelelezi wawili Waisraeli wakati uzima wao ulikuwa mu hatari. Ile ilikuwa na matokeo gani? Ule mwanamuke, mwenye hakamilike na mwenye hakukuwa Muisraeli, alionwa kuwa mwenye haki sawa vile tu Abrahamu. Mufano wake unaonyesha ulazima wa kuwa na imani yenye inaonekana kupitia matendo. w23.12 5-6 fu. 12-13
Siku ya Ine, 23 Mwezi wa 10
“Mukuwe na mizizi na kufanywa imara juu ya ule musingi.”—Efe. 3: 17.
Siye Wakristo hatutosheke tu na mafundisho ya musingi ya Biblia. Kwa musaada wa roho takatifu ya Mungu tunapenda sana kujifunza “hata mambo mazito ya Mungu.” (1 Ko. 2:9, 10) Juu ya nini usijiwekee programu ya kujifunza habari zenye zitakusaidia umukaribie Yehova zaidi? Kwa mufano, unaweza kuchunguza namna alionyesha upendo watumishi wake wa zamani na namna ile inaonyesha kama anakupenda na weye. Unaweza kuchunguza mipango yenye Yehova aliweka kwa ajili ya ibada mu Israeli na kuona namna inalingana na vile Yehova anapenda Wakristo wamuabudu leo. Ao pengine unaweza kujifunza kwa undani maunabii yenye Yesu alitimiza mu maisha na utumishi wake hapa ku dunia. Tutafurahi sana kama tunajifunza zile habari kwa kutumia Index ao Musaada wa Kutafuta Habari kwa Ajili ya Mashahidi wa Yehova. Kujifunza Biblia kwa undani kunaweza kukusaidia kutia nguvu imani yako, na kukusaidia “upate ujuzi juu ya Mungu.”—Mez. 2:4, 5. w23.10 18-19 fu. 3-5
Siku ya Tano, 24 Mwezi wa 10
Zaidi ya mambo yote, mukuwe na upendo mwingi ninyi kwa ninyi, kwa sababu upendo unafunika zambi nyingi.—1 Pe. 4:8.
Neno yenye mutume Neno “mwingi” yenye Petro alitumia inamaanisha neno kwa neno “kupanuka.” Sehemu ya pili ya ile andiko inaonyesha matokeo ya upendo mwingi: unafunika zambi za ndugu zetu. Ni sawa vile upendo ulikuwa nguo yenye inaweza kupanuka yenye tunakamata na mikono mbili na tunaanza kuikokota na inapanuka mupaka inafunika hapana zambi moya ao mbili, lakini “zambi nyingi.” ‘Kufunika’ ni namna ingine ya kusema kusamehe. Sawa tu vile nguo inaweza kufunika kasoro, upendo unaweza kufunika uzaifu na makosa ya wengine. Upendo wetu unapaswa kuwa nguvu sana juu tuweze kusamehe makosa ya waamini wenzetu, hata kama wakati fulani ile inaomba kujikaza sana. (Kol. 3:13) Wakati tunasamehe wengine tunaonyesha kama upendo wetu uko nguvu na kama tunapenda kumufurahisha Yehova. w23.11 11-12 fu. 13-15