Siku ya Ine, 23 Mwezi wa 10
“Mukuwe na mizizi na kufanywa imara juu ya ule musingi.”—Efe. 3: 17.
Siye Wakristo hatutosheke tu na mafundisho ya musingi ya Biblia. Kwa musaada wa roho takatifu ya Mungu tunapenda sana kujifunza “hata mambo mazito ya Mungu.” (1 Ko. 2:9, 10) Juu ya nini usijiwekee programu ya kujifunza habari zenye zitakusaidia umukaribie Yehova zaidi? Kwa mufano, unaweza kuchunguza namna alionyesha upendo watumishi wake wa zamani na namna ile inaonyesha kama anakupenda na weye. Unaweza kuchunguza mipango yenye Yehova aliweka kwa ajili ya ibada mu Israeli na kuona namna inalingana na vile Yehova anapenda Wakristo wamuabudu leo. Ao pengine unaweza kujifunza kwa undani maunabii yenye Yesu alitimiza mu maisha na utumishi wake hapa ku dunia. Tutafurahi sana kama tunajifunza zile habari kwa kutumia Index ao Musaada wa Kutafuta Habari kwa Ajili ya Mashahidi wa Yehova. Kujifunza Biblia kwa undani kunaweza kukusaidia kutia nguvu imani yako, na kukusaidia “upate ujuzi juu ya Mungu.”—Mez. 2:4, 5. w23.10 18-19 fu. 3-5
Siku ya Tano, 24 Mwezi wa 10
Zaidi ya mambo yote, mukuwe na upendo mwingi ninyi kwa ninyi, kwa sababu upendo unafunika zambi nyingi.—1 Pe. 4:8.
Neno yenye mutume Neno “mwingi” yenye Petro alitumia inamaanisha neno kwa neno “kupanuka.” Sehemu ya pili ya ile andiko inaonyesha matokeo ya upendo mwingi: unafunika zambi za ndugu zetu. Ni sawa vile upendo ulikuwa nguo yenye inaweza kupanuka yenye tunakamata na mikono mbili na tunaanza kuikokota na inapanuka mupaka inafunika hapana zambi moya ao mbili, lakini “zambi nyingi.” ‘Kufunika’ ni namna ingine ya kusema kusamehe. Sawa tu vile nguo inaweza kufunika kasoro, upendo unaweza kufunika uzaifu na makosa ya wengine. Upendo wetu unapaswa kuwa nguvu sana juu tuweze kusamehe makosa ya waamini wenzetu, hata kama wakati fulani ile inaomba kujikaza sana. (Kol. 3:13) Wakati tunasamehe wengine tunaonyesha kama upendo wetu uko nguvu na kama tunapenda kumufurahisha Yehova. w23.11 11-12 fu. 13-15
Siku ya Posho, 25 Mwezi wa 10
Shafani akaanza kukisoma mbele ya mufalme.—2 Ny. 34:18.
Wakati Mufalme Yosia alikuwa na miaka 26 alianza kutengeneza hekalu. Wakati ile kazi ilikuwa inafanywa, “kitabu cha Sheria ya Yehova yenye ilipewa kupitia Musa” kilipatikana. Kisha kusikia maneno yenye ilikuwa imeandikwa mu ile kitabu, mufalme alichochewa kutenda kupatana na ile maneno. (2 Ny. 34:14, 19-21) Na weye ungependa kuwa nasoma Biblia kila siku? Kama uko najikaza kufanya vile, usomaji wako uko naendelea muzuri? Unaandikaka maandiko yenye inaweza kukusaidia? Wakati Yosia alikuwa na miaka karibu 39 alifanya kosa yenye ilifanya apoteze uzima wake. Alijitumainia kuliko kutafuta muongozo wa Yehova. (2 Ny. 35:20-25) Tunajifunza nini? Ikuwe tuko na miaka ngapi, ao tumejifunza Biblia kwa muda gani, tunapaswa kuendelea kumutafuta Yehova, ni kusema, tunapaswa kusali kwa ukawaida, kutafuta muongozo wake, kujifunza Neno yake, na kutafuta mashauri ya Wakristo wenye kukomaa kiroho. Kama tunafanya vile, inawezekana tusifanye makosa makubwa-makubwa na tukuwe na furaha zaidi.—Yak. 1:25. w23.09 12 fu. 15-16