Siku ya Posho, 25 Mwezi wa 10
Shafani akaanza kukisoma mbele ya mufalme.—2 Ny. 34:18.
Wakati Mufalme Yosia alikuwa na miaka 26 alianza kutengeneza hekalu. Wakati ile kazi ilikuwa inafanywa, “kitabu cha Sheria ya Yehova yenye ilipewa kupitia Musa” kilipatikana. Kisha kusikia maneno yenye ilikuwa imeandikwa mu ile kitabu, mufalme alichochewa kutenda kupatana na ile maneno. (2 Ny. 34:14, 19-21) Na weye ungependa kuwa nasoma Biblia kila siku? Kama uko najikaza kufanya vile, usomaji wako uko naendelea muzuri? Unaandikaka maandiko yenye inaweza kukusaidia? Wakati Yosia alikuwa na miaka karibu 39 alifanya kosa yenye ilifanya apoteze uzima wake. Alijitumainia kuliko kutafuta muongozo wa Yehova. (2 Ny. 35:20-25) Tunajifunza nini? Ikuwe tuko na miaka ngapi, ao tumejifunza Biblia kwa muda gani, tunapaswa kuendelea kumutafuta Yehova, ni kusema, tunapaswa kusali kwa ukawaida, kutafuta muongozo wake, kujifunza Neno yake, na kutafuta mashauri ya Wakristo wenye kukomaa kiroho. Kama tunafanya vile, inawezekana tusifanye makosa makubwa-makubwa na tukuwe na furaha zaidi.—Yak. 1:25. w23.09 12 fu. 15-16
Siku ya Yenga, 26 Mwezi wa 10
Mungu anapinga wenye majivuno, lakini anapatia wanyenyekevu fazili zenye hazistahiliwe.—Yak. 4:6.
Biblia inazungumuzia mifano mingi ya wanamuke wa pekee wenye walimupenda na kumutumikia Yehova. Kama vile andiko yetu ya musingi inaonyesha, walikuwa “na kiasi katika tabia zao, na waaminifu katika mambo yote.”(1 Ti. 3:11) Zaidi ya ile, dada vijana wanaweza kupata mu kutaniko yao dada Wakristo wenye kukomaa kiroho wenye kuwa mifano mizuri ya kuiga. Dada vijana, hamuone kama itakua muzuri mutafute mu kutaniko yenu dada fulani wenye kukomaa kiroho wenye munaweza kuiga? Mutambue sifa zao za muzuri, kisha muone namna munaweza pia kuzionyesha. Moya kati ya sifa za maana ili kuwa Mukristo mwenye kukomaa kiroho ni unyenyekevu. Kama dada iko munyenyekevu, atakuwa na uhusiano muzuri pamoya na Yehova na pamoya na wengine. Kwa mufano, mwanamuke mwenye anamupenda Yehova anategemeza kwa unyenyekevu mupango wa ukichwa wenye Baba yake wa mbinguni aliweka. (1 Ko. 11:3) Kuko mambo yenye anaweza kufanya juu ya kuonyesha kama anategemeza ule mupango wa ukichwa mu kutaniko, na mambo ingine yenye anaweza kufanya juu ya kuonyesha kama anategemeza ule mupango mu familia. w23.12 18-19 fu. 3-5
Siku ya Kwanza, 27 Mwezi wa 10
Bwana wanapaswa kupenda bibi zao kama miili yao wenyewe.—Efe. 5:28.
Yehova anatazamia kwamba bwana amupende bibi yake na ahangaikie mahitaji yake ya kiroho, ya kimwili, na akuwe rafiki muzuri kwake. Kuwa na uwezo wa kufikiri, kuheshimia wanamuke, na kuwa mwenye kutegemeka, zitakusaidia kuwa bwana muzuri. Kisha kuoa, munaweza kuwa na watoto. Mufano wa Yehova unaweza kukufundisha nini kuhusu kuwa baba muzuri? (Efe. 6:4) Yehova aliambia waziwazi Yesu, mwana wake, kama anamupenda na anamukubali. (Mt. 3:17) Kama unakuwa baba, uhakikishie watoto wako kwa ukawaida kama unawapenda. Ukuwe na zoea ya kuwapongeza juu ya mambo ya muzuri yenye wanafanya. Baba wenye wanamuiga Yehova wanasaidia watoto wao wakuwe Wakristo wenye kukomaa kiroho. Unaweza kujitayarisha sasa kwa ajili ya ile daraka kwa kupenda na kuhangaikia watu wa familia yako na wa mu kutaniko, na kwa kujifunza kuwaonyesha kama unawapenda na kama unawaona kuwa wa maana.—Yoh. 15:9. w23.12 28-29 fu. 17-18