Siku ya Yenga, 26 Mwezi wa 10
Mungu anapinga wenye majivuno, lakini anapatia wanyenyekevu fazili zenye hazistahiliwe.—Yak. 4:6.
Biblia inazungumuzia mifano mingi ya wanamuke wa pekee wenye walimupenda na kumutumikia Yehova. Kama vile andiko yetu ya musingi inaonyesha, walikuwa “na kiasi katika tabia zao, na waaminifu katika mambo yote.”(1 Ti. 3:11) Zaidi ya ile, dada vijana wanaweza kupata mu kutaniko yao dada Wakristo wenye kukomaa kiroho wenye kuwa mifano mizuri ya kuiga. Dada vijana, hamuone kama itakua muzuri mutafute mu kutaniko yenu dada fulani wenye kukomaa kiroho wenye munaweza kuiga? Mutambue sifa zao za muzuri, kisha muone namna munaweza pia kuzionyesha. Moya kati ya sifa za maana ili kuwa Mukristo mwenye kukomaa kiroho ni unyenyekevu. Kama dada iko munyenyekevu, atakuwa na uhusiano muzuri pamoya na Yehova na pamoya na wengine. Kwa mufano, mwanamuke mwenye anamupenda Yehova anategemeza kwa unyenyekevu mupango wa ukichwa wenye Baba yake wa mbinguni aliweka. (1 Ko. 11:3) Kuko mambo yenye anaweza kufanya juu ya kuonyesha kama anategemeza ule mupango wa ukichwa mu kutaniko, na mambo ingine yenye anaweza kufanya juu ya kuonyesha kama anategemeza ule mupango mu familia. w23.12 18-19 fu. 3-5
Siku ya Kwanza, 27 Mwezi wa 10
Bwana wanapaswa kupenda bibi zao kama miili yao wenyewe.—Efe. 5:28.
Yehova anatazamia kwamba bwana amupende bibi yake na ahangaikie mahitaji yake ya kiroho, ya kimwili, na akuwe rafiki muzuri kwake. Kuwa na uwezo wa kufikiri, kuheshimia wanamuke, na kuwa mwenye kutegemeka, zitakusaidia kuwa bwana muzuri. Kisha kuoa, munaweza kuwa na watoto. Mufano wa Yehova unaweza kukufundisha nini kuhusu kuwa baba muzuri? (Efe. 6:4) Yehova aliambia waziwazi Yesu, mwana wake, kama anamupenda na anamukubali. (Mt. 3:17) Kama unakuwa baba, uhakikishie watoto wako kwa ukawaida kama unawapenda. Ukuwe na zoea ya kuwapongeza juu ya mambo ya muzuri yenye wanafanya. Baba wenye wanamuiga Yehova wanasaidia watoto wao wakuwe Wakristo wenye kukomaa kiroho. Unaweza kujitayarisha sasa kwa ajili ya ile daraka kwa kupenda na kuhangaikia watu wa familia yako na wa mu kutaniko, na kwa kujifunza kuwaonyesha kama unawapenda na kama unawaona kuwa wa maana.—Yoh. 15:9. w23.12 28-29 fu. 17-18
Siku ya Pili, 28 Mwezi wa 10
[Yehova] ndiye anafanya nyakati zako kuwa imara.—Isa. 33:6.
Siye watumishi waaminifu wa Yehova tunapambana na magumu yenye watu wote wanapataka. Tunaweza pia kupambana na upinzani ao mateso kutoka kwa wale wenye wanachukia watu wa Mungu. Hata kama Yehova hazuie ile magumu isitupate, anatuahidi kama atatusaidia. (Isa. 41:10) Kwa musaada wake tunaweza kuendelea kuwa na furaha, kukamata maamuzi ya muzuri, na kuendelea kuwa washikamanifu, hata mu hali za nguvu sana. Yehova anaahidi kutupatia jambo yenye Biblia inaita “amani ya Mungu.” (Flp. 4:6, 7) Ile amani ni utulivu wa akili na wa moyo wenye mutu anakuwaka nao kwa sababu ya uhusiano muzuri wenye iko nao pamoja naye. Ile amani “inapita uelewaji wote”; inapita jambo yoyote yenye tunaweza kuwazia. Ulishakasikia utulivu wa ajabu kisha kusali kwa Yehova? Ile yenye ulisikiaka njo “amani ya Mungu.” w24.01 20 fu. 2; 21 fu. 4