Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2026)
Toka
Ingia
Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Karibu
Hii ni chombo ya kukusaidia kutafuta habari mu vichapo vya Mashahidi wa Yehova mu luga mbalimbali.
Kama unapenda kuchukua kichapo fulani, tafazali fungua jw.org.
Matangazo
Luga mupya yenye kupatikana: Betsileo
  • Leo

Siku ya Pili, 28 Mwezi wa 10

[Yehova] ndiye anafanya nyakati zako kuwa imara.​—Isa. 33:6.

Siye watumishi waaminifu wa Yehova tunapambana na magumu yenye watu wote wanapataka. Tunaweza pia kupambana na upinzani ao mateso kutoka kwa wale wenye wanachukia watu wa Mungu. Hata kama Yehova hazuie ile magumu isitupate, anatuahidi kama atatusaidia. (Isa. 41:10) Kwa musaada wake tunaweza kuendelea kuwa na furaha, kukamata maamuzi ya muzuri, na kuendelea kuwa washikamanifu, hata mu hali za nguvu sana. Yehova anaahidi kutupatia jambo yenye Biblia inaita “amani ya Mungu.” (Flp. 4:6, 7) Ile amani ni utulivu wa akili na wa moyo wenye mutu anakuwaka nao kwa sababu ya uhusiano muzuri wenye iko nao pamoja naye. Ile amani “inapita uelewaji wote”; inapita jambo yoyote yenye tunaweza kuwazia. Ulishakasikia utulivu wa ajabu kisha kusali kwa Yehova? Ile yenye ulisikiaka njo “amani ya Mungu.” w24.01 20 fu. 2; 21 fu. 4

Tuchunguze Maandiko Kila Siku—2025

Siku ya Tatu, 29 Mwezi wa 10

Acha nimusifu Yehova; Acha kila kitu chenye kuwa ndani yangu kisifu jina lake takatifu.​—Zb. 103:1.

Watu waaminifu wanamupenda Mungu, na ile inawachochea wasifu jina yake kwa moyo wote. Mufalme Daudi alielewa kama kusifu jina ya Mungu ni kumusifu Mungu mwenyewe. Jina ya Mungu, Yehova, inamaanisha mambo mingi, inatukumbusha sifa zake za muzuri, na matendo yake ya ajabu. Daudi aliona jina ya Baba yake kuwa takatifu na aliisifu. Alipenda kufanya vile kwa “kila kitu chenye kuwa ndani” yake, ni kusema, kwa moyo wote. Kuhusu kumusifu Yehova, Walawi njo walikuwa ku mustari wa mbele. Kwa unyenyekevu, walikubali kama maneno yao haingeweza kusifu jina ya Yehova kwa ukamili vile inastahili. (Ne. 9:5) Bila shaka, ile sifa yenye kutoka ku moyo na yenye kufanywa kwa unyenyekevu, ilifurahisha moyo wa Yehova. w24.02 9 fu. 6

Tuchunguze Maandiko Kila Siku—2025

Siku ya Ine, 30 Mwezi wa 10

Kwa kadiri tumefanya maendeleo, tuendelee kutembea kwa utaratibu katika mwendo uleule.​—Flp. 3:16.

Kama haufikie muradi wenye haupatane na uwezo wako, usiwaze kama Yehova ataona kuwa unashindwa. (2 Ko. 8:12) Ujifunze mambo fulani kupitia kizuizi yenye unakutana nayo.Usisahau miradi yenye ulishakafikia. Biblia inasema kama “Mungu hana ukosefu wa haki ili asahau kazi yenu.” (Ebr. 6:10) Na weye usisahau miradi yenye ulishakafikia, sawa vile kukomalisha urafiki wako pamoya na Yehova, kuambia wengine juu yake, ao kubatizwa. Sawa vile tu ulijikazaka kufikia miradi yako ya kiroho zamani, unaweza pia kujikaza kufikia miradi yako ya sasa.Kwa musaada wa Yehova, unaweza kuwa na furaha ya kufikia muradi wako Kila mara ujikaze kuona namna Yehova iko nakusaidia, na ile itafanya ukuwe na furaha wakati uko najikaza kufikia miradi yako. (2 Ko. 4:7) Kama hauvunjike moyo, utapata baraka mingi hata zaidi.​—Gal. 6:9. w23.05 31 fu. 16-18

Tuchunguze Maandiko Kila Siku—2025
Karibu
Hii ni chombo ya kukusaidia kutafuta habari mu vichapo vya Mashahidi wa Yehova mu luga mbalimbali.
Kama unapenda kuchukua kichapo fulani, tafazali fungua jw.org.
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine