Siku ya Tatu, 29 Mwezi wa 10
Acha nimusifu Yehova; Acha kila kitu chenye kuwa ndani yangu kisifu jina lake takatifu.—Zb. 103:1.
Watu waaminifu wanamupenda Mungu, na ile inawachochea wasifu jina yake kwa moyo wote. Mufalme Daudi alielewa kama kusifu jina ya Mungu ni kumusifu Mungu mwenyewe. Jina ya Mungu, Yehova, inamaanisha mambo mingi, inatukumbusha sifa zake za muzuri, na matendo yake ya ajabu. Daudi aliona jina ya Baba yake kuwa takatifu na aliisifu. Alipenda kufanya vile kwa “kila kitu chenye kuwa ndani” yake, ni kusema, kwa moyo wote. Kuhusu kumusifu Yehova, Walawi njo walikuwa ku mustari wa mbele. Kwa unyenyekevu, walikubali kama maneno yao haingeweza kusifu jina ya Yehova kwa ukamili vile inastahili. (Ne. 9:5) Bila shaka, ile sifa yenye kutoka ku moyo na yenye kufanywa kwa unyenyekevu, ilifurahisha moyo wa Yehova. w24.02 9 fu. 6
Siku ya Ine, 30 Mwezi wa 10
Kwa kadiri tumefanya maendeleo, tuendelee kutembea kwa utaratibu katika mwendo uleule.—Flp. 3:16.
Kama haufikie muradi wenye haupatane na uwezo wako, usiwaze kama Yehova ataona kuwa unashindwa. (2 Ko. 8:12) Ujifunze mambo fulani kupitia kizuizi yenye unakutana nayo.Usisahau miradi yenye ulishakafikia. Biblia inasema kama “Mungu hana ukosefu wa haki ili asahau kazi yenu.” (Ebr. 6:10) Na weye usisahau miradi yenye ulishakafikia, sawa vile kukomalisha urafiki wako pamoya na Yehova, kuambia wengine juu yake, ao kubatizwa. Sawa vile tu ulijikazaka kufikia miradi yako ya kiroho zamani, unaweza pia kujikaza kufikia miradi yako ya sasa.Kwa musaada wa Yehova, unaweza kuwa na furaha ya kufikia muradi wako Kila mara ujikaze kuona namna Yehova iko nakusaidia, na ile itafanya ukuwe na furaha wakati uko najikaza kufikia miradi yako. (2 Ko. 4:7) Kama hauvunjike moyo, utapata baraka mingi hata zaidi.—Gal. 6:9. w23.05 31 fu. 16-18
Siku ya Tano, 31 Mwezi wa 10
Baba mwenyewe anawapenda ninyi, kwa sababu mumenipenda na mumeamini kwamba nilikuja nikiwa mwakilishi wa Mungu.—Yoh. 16:27.
Yehova anapenda kuonyesha kama anakubali wale wenye anapenda. Maandiko inazungumuzia mara mbili zenye Yehova aliambia Yesu kama alikuwa Mwana wake mupendwa mwenye alikubali. (Mt. 3:17; 17:5) Unapenda kumusikia Yehova anasema kama anakukubali? Hatuwezi kusikia sauti ya Yehova, lakini anazungumuza na siye kupitia Neno yake. Tunaweza “kumusikia” Yehova anasema kuwa anatukubali wakati tunasoma maneno ya Yesu yenye kuwa mu Injili. Yesu alionyesha kwa ukamili utu wa Baba yake. Wakati tunasoma namna Yesu aliambia wafuasi wake waaminifu kama anawakubali hata kama hawakukuwa wakamilifu, tunaweza kuwazia kama ni Yehova njo iko natuambia ile maneno. (Yoh. 15:9, 15) Kama tunapata magumu, ile magumu haimaanishe kama Yehova hatukubali tena. Lakini inatupatia nafasi ya kuonyesha ni kwa kadiri gani tunamupenda na kumutumainia.—Yak. 1:12. w24.03 28 fu. 10-11