Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2026)
Toka
Ingia
Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Karibu
Hii ni chombo ya kukusaidia kutafuta habari mu vichapo vya Mashahidi wa Yehova mu luga mbalimbali.
Kama unapenda kuchukua kichapo fulani, tafazali fungua jw.org.
  • Leo

Siku ya Yenga, 9 Mwezi wa 11

Usiogope.​—Da. 10:19.

Juu tuonyeshe uhodari, tunapaswa kufanya nini? Wazazi wetu wanaweza kutuambia tukuwe na uhodari, lakini hata kama wako na uhodari, ile haimaanishe kama na siye tutakuwa tu na ile sifa. Kuwa na uhodari ni sawa vile kujifunza jambo fulani ya mupya. Jambo moya yenye inaweza kusaidia mutu akuwe na ufundi kuhusu jambo yenye iko najifunza ni kuangalia kwa uangalifu mambo yenye mwalimu wake iko nafanya na kumuiga. Vilevile, tutakuwa na uhodari, kama tunaangalia kwa uangalifu namna wengine wako naonyesha ile sifa na kuwaiga. Sawa vile Daniel, tunapaswa kujua muzuri Neno ya Mungu. Tunapaswa kufanya urafiki wa karibu sana pamoya na Yehova kwa kuongea naye kila mara na kumuambia vile tuko najisikia kabisa. Na tunapaswa kumutumainia kwa kuwa hakika kama ataendelea kutusaidia. Kama tunafanya vile, wakati imani yetu itajaribiwa tutaonyesha uhodari. Mara mingi watu wanaheshimiaka mutu mwenye kuwa na uhodari. Mutu mwenye uhodari anaweza pia kusaidia wengine wamujue Yehova. Bila shaka ni jambo ya maana kuonyesha uhodari. w23.08 2 fu. 2; 4 fu. 8-9

Tuchunguze Maandiko Kila Siku—2025

Siku ya Kwanza, 10 Mwezi wa 11

Muchunguze mambo yote.​—1 Te. 5:21.

Neno ya Kigiriki yenye inatafsiriwa “muchunguze” ilikuwa natumiwa ili kuonyesha namna watu walikuwa napima metali sawa vile zahabu na feza ili kujua kama zilikuwa za kweli. Kwa hiyo, siye pia tunapaswa kujaribu ao kuchunguza maneno yenye tunasikia ao mambo yenye tunasoma ili kuona kama ni ya kweli ao hapana. Ile itaendelea kuwa ya maana zaidi sana kwetu kadiri taabu kubwa iko nakaribia. Kuliko kuamini kila jambo yenye watu wanasema, tunatumia uwezo wetu wa kufikiri ili kulinganisha mambo yenye tunasoma ao yenye tunasikia na mambo yenye Biblia na tengenezo ya Yehova inasema. Kama tunafanya vile, hatutapotoshwa na habari yoyote ya uongo yenye kuongozwa na pepo muchafu. (Mez. 14:15; 1 Ti. 4:1) Tunajua kama watumishi wa Mungu wataokoka taabu kubwa. Lakini, hakuna mwenye anajua mambo ya kesho. (Yak. 4:14) Hata vile, ikuwe tutakuwa tungali wazima wakati wa taabu kubwa ao kama tutakufa mbele ianze, tutapata zawabu ya uzima wa milele kama tunaendelea kuwa waaminifu. Tuendelee basi kukaza akili yetu juu ya tumaini yetu ya muzuri na tuendelee kuwa tayari kwa ajili ya siku ya Yehova! w23.06 13 fu. 15-16

Tuchunguze Maandiko Kila Siku—2025

Siku ya Pili, 11 Mwezi wa 11

[Anafunulia] watumishi wake manabii jambo lake la siri.​—Amo. 3:7.

Hatujue namna maunabii fulani yenye kuwa mu Biblia itatimia. (Da. 12: 8, 9) Lakini, kushindwa kuelewa kabisa namna unabii fulani utatimia, haimaanishe kama ule unabii hautatimia. Bila shaka, tunaweza kuwa hakika kama kwa wakati wenye kufaa kabisa Yehova atatusaidia kuelewa mambo yenye tunapaswa kujua, sawa vile alifanyaka zamani. Mataifa itafanya tangazo ya “amani na usalama.” (1 Te. 5:3) Kisha, serikali za ulimwengu zitashambulia dini ya uongo na kuiharibu. (Ufu. 17:16, 17) Na kisha watashambulia watu wa Mungu. (Eze. 38:18, 19) Ile matukio itaongoza moja kwa moja ku vita ya mwisho ya Armagedoni. (Ufu. 16:14, 16) Tuko hakika kama ile mambo itatokea hivi karibuni. Mbele itokee, tuendelee basi kumushukuru Baba yetu wa mbinguni mwenye upendo kwa kuchunguza kwa uangalifu maunabii yenye kuwa mu Biblia na kwa kusaidia wengine wafanye pia vile. w23.08 13 fu. 19-20

Tuchunguze Maandiko Kila Siku—2025
Karibu
Hii ni chombo ya kukusaidia kutafuta habari mu vichapo vya Mashahidi wa Yehova mu luga mbalimbali.
Kama unapenda kuchukua kichapo fulani, tafazali fungua jw.org.
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine