Siku ya Posho, 8 Mwezi wa 11
Miali ya [upendo] ni moto wenye kuwaka sana, mwali wa moto wa Yah. Maji mengi hayawezi kuzima upendo, wala mito haiwezi kuufagilia mbali.—Wim. 8:6, 7.
Ile ni mafasirio ya muzuri sana ya upendo wa kweli! Na inahakikishia bibi na bwana kama wanaweza kuonyeshana upendo wa kweli. Inaomba kujikaza sana juu bibi na bwana wapendane maisha yao yote. Kwa mufano, moto unaweza kuendelea kuwaka kama mutu anaongeza kuni; kama hafanye vile, unaweza kuzimika. Vilevile, upendo kati ya bibi na bwana unaweza kuendelea kuwa nguvu maisha yao yote kama tu wako nafanya uhusiano wao ukuwe nguvu. Wakati fulani, bibi na bwana wanaweza kuona kama upendo wao uko napunguka, zaidi sana wakati wako na magumu ya kupata makuta, magumu ya afya, ao magumu ya kukomalisha watoto. Juu “mwali wa moto wa Yah” usizimike, bibi na bwana wanapaswa kuwa na uhusiano wa nguvu pamoya na Yehova. w23.05 20-21 fu. 1-3
Siku ya Yenga, 9 Mwezi wa 11
Usiogope.—Da. 10:19.
Juu tuonyeshe uhodari, tunapaswa kufanya nini? Wazazi wetu wanaweza kutuambia tukuwe na uhodari, lakini hata kama wako na uhodari, ile haimaanishe kama na siye tutakuwa tu na ile sifa. Kuwa na uhodari ni sawa vile kujifunza jambo fulani ya mupya. Jambo moya yenye inaweza kusaidia mutu akuwe na ufundi kuhusu jambo yenye iko najifunza ni kuangalia kwa uangalifu mambo yenye mwalimu wake iko nafanya na kumuiga. Vilevile, tutakuwa na uhodari, kama tunaangalia kwa uangalifu namna wengine wako naonyesha ile sifa na kuwaiga. Sawa vile Daniel, tunapaswa kujua muzuri Neno ya Mungu. Tunapaswa kufanya urafiki wa karibu sana pamoya na Yehova kwa kuongea naye kila mara na kumuambia vile tuko najisikia kabisa. Na tunapaswa kumutumainia kwa kuwa hakika kama ataendelea kutusaidia. Kama tunafanya vile, wakati imani yetu itajaribiwa tutaonyesha uhodari. Mara mingi watu wanaheshimiaka mutu mwenye kuwa na uhodari. Mutu mwenye uhodari anaweza pia kusaidia wengine wamujue Yehova. Bila shaka ni jambo ya maana kuonyesha uhodari. w23.08 2 fu. 2; 4 fu. 8-9
Siku ya Kwanza, 10 Mwezi wa 11
Muchunguze mambo yote.—1 Te. 5:21.
Neno ya Kigiriki yenye inatafsiriwa “muchunguze” ilikuwa natumiwa ili kuonyesha namna watu walikuwa napima metali sawa vile zahabu na feza ili kujua kama zilikuwa za kweli. Kwa hiyo, siye pia tunapaswa kujaribu ao kuchunguza maneno yenye tunasikia ao mambo yenye tunasoma ili kuona kama ni ya kweli ao hapana. Ile itaendelea kuwa ya maana zaidi sana kwetu kadiri taabu kubwa iko nakaribia. Kuliko kuamini kila jambo yenye watu wanasema, tunatumia uwezo wetu wa kufikiri ili kulinganisha mambo yenye tunasoma ao yenye tunasikia na mambo yenye Biblia na tengenezo ya Yehova inasema. Kama tunafanya vile, hatutapotoshwa na habari yoyote ya uongo yenye kuongozwa na pepo muchafu. (Mez. 14:15; 1 Ti. 4:1) Tunajua kama watumishi wa Mungu wataokoka taabu kubwa. Lakini, hakuna mwenye anajua mambo ya kesho. (Yak. 4:14) Hata vile, ikuwe tutakuwa tungali wazima wakati wa taabu kubwa ao kama tutakufa mbele ianze, tutapata zawabu ya uzima wa milele kama tunaendelea kuwa waaminifu. Tuendelee basi kukaza akili yetu juu ya tumaini yetu ya muzuri na tuendelee kuwa tayari kwa ajili ya siku ya Yehova! w23.06 13 fu. 15-16