Siku ya Posho, 1 Mwezi wa 11
Kutoka katika kinywa cha watoto wadogo na watoto wenye kunyonya umetokeza sifa.—Mt. 21:16.
Kama uko muzazi, usaidie watoto wako watayarishe maelezo yenye kufaa kulingana na miaka yao. Wakati fulani, mambo mazito sawa vile magumu ya ndoa ao namna ya kuwa na mwenendo safi inazungumuziwaka wakati ya funzo. Hata vile, kunaweza kuwa fungu moya ao mbili kwenye mutoto anaweza kutoa maelezo. Tena, usaidie watoto wako waelewe juu ya nini kiongozi hatawataya kila mara wakati wananyangula mikono. Kufanya vile, kunaweza kuwasaidia wasikasirike wakati kiongozi anataya wengine. (1 Ti. 6:18) Siye wote tunaweza kutayarisha maelezo yenye itamutukuza Yehova na yenye itajenga Wakristo wenzetu. (Mez. 25:11) Kama tunazungumuzia jambo yenye inatuhusu, tunapaswa kuepuka kusema mambo mingi juu yetu. ( Mez. 27:2; 2 Ko. 10:18) Kuliko kufanya vile, tutakaza akili juu ya Yehova, Neno yake, na watu wake.—Ufu. 4:11. w23.04 24-25 fu. 17-18
Siku ya Yenga, 2 Mwezi wa 11
Tusiendelee kulala usingizi kama wengine, lakini tukae macho na kulinda akili zetu.—1 Te. 5:6.
Upendo ni wa maana ili tukuwe macho na kulinda akili zetu. (Mt. 22:37-39) Kumupenda Mungu kunatusaidia tuhubiri kwa uvumilivu hata kama ile inaweza kufanya tupate magumu. (2 Ti. 1:7, 8) Tunaendelea kuhubiri kwa kutumia telefone na hata barua juu tunapenda pia wale wenye hawamutumikie Yehova. Tunatumainia kama siku moya majirani wetu watabadilika na kuanza kufanya mambo ya muzuri. (Eze. 18:27, 28) Tunapenda pia ndugu na dada zetu. Tunaonyesha ule upendo kwa “kutiana moyo na kujengana.” (1 Te. 5:11) Sawa vile maaskari wenye hawaachanake mu vita, siye pia tunatianaka moyo. Hatuwezi kukwaza ndugu na dada zetu kwa kupenda ao kurudisha ubaya kwa ubaya. (1 Te. 5:13, 15) Tunaonyesha pia kama tuko na upendo kwa kuheshimia ndugu wenye wanasimamia kutaniko.—1 Te. 5:12. w23.06 10 fu. 6; 11 fu. 10-11
Siku ya Kwanza, 3 Mwezi wa 11
Wakati [Yehova] anasema jambo fulani, je, hatalifanya?—Hes. 23:19.
Jambo moya yenye inaweza kufanya imani yetu ikuwe nguvu ni kutafakari juu ya bei ya ukombozi. Bei ya ukombozi inatuhakikishia kama ahadi za Mungu zitatimia. Wakati tunafikiria kwa uangalifu sababu yenye ilifanya Yehova atoe bei ya ukombozi na mambo yenye ile iliomba, tutaamini kabisa kama atatimiza ahadi ya kutupatia uzima wa milele mu dunia mupya. Juu ya nini tunasema vile? Bei ya ukombozi iliomba nini? Yehova alituma Mwana wake muzaliwa-pekee, mwenye alipenda sana na mwenye alikuwa rafiki yake wa karibu sana, ili azaliwe hapa ku dunia akiwa mwanadamu mukamilifu. Wakati Yesu alikuwa hapa ku dunia, alivumilia magumu ya kila aina. Kisha, aliteseka na kufa kifo ya maumivu. Yehova alilipa bei kubwa sana! Mungu wetu mwenye upendo hangeacha Mwana wake ateseke na kufa juu tu tukuwe na maisha ya muzuri kwa wakati mufupi sana. (Yoh. 3:16; 1 Pe. 1:18, 19) Juu Yehova alilipa bei kubwa vile, ile inaonyesha kama atatupatia uzima wa milele mu dunia mupya. w23.04 27 fu. 8-9