Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2026)
Toka
Ingia
Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Karibu
Hii ni chombo ya kukusaidia kutafuta habari mu vichapo vya Mashahidi wa Yehova mu luga mbalimbali.
Kama unapenda kuchukua kichapo fulani, tafazali fungua jw.org.
  • Leo

Siku ya Tano, 31 Mwezi wa 10

Baba mwenyewe anawapenda ninyi, kwa sababu mumenipenda na mumeamini kwamba nilikuja nikiwa mwakilishi wa Mungu.​—Yoh. 16:27.

Yehova anapenda kuonyesha kama anakubali wale wenye anapenda. Maandiko inazungumuzia mara mbili zenye Yehova aliambia Yesu kama alikuwa Mwana wake mupendwa mwenye alikubali. (Mt. 3:17; 17:5) Unapenda kumusikia Yehova anasema kama anakukubali? Hatuwezi kusikia sauti ya Yehova, lakini anazungumuza na siye kupitia Neno yake. Tunaweza “kumusikia” Yehova anasema kuwa anatukubali wakati tunasoma maneno ya Yesu yenye kuwa mu Injili. Yesu alionyesha kwa ukamili utu wa Baba yake. Wakati tunasoma namna Yesu aliambia wafuasi wake waaminifu kama anawakubali hata kama hawakukuwa wakamilifu, tunaweza kuwazia kama ni Yehova njo iko natuambia ile maneno. (Yoh. 15:9, 15) Kama tunapata magumu, ile magumu haimaanishe kama Yehova hatukubali tena. Lakini inatupatia nafasi ya kuonyesha ni kwa kadiri gani tunamupenda na kumutumainia.​—Yak. 1:12. w24.03 28 fu. 10-11

Tuchunguze Maandiko Kila Siku—2025

Siku ya Posho, 1 Mwezi wa 11

Kutoka katika kinywa cha watoto wadogo na watoto wenye kunyonya umetokeza sifa.​—Mt. 21:16.

Kama uko muzazi, usaidie watoto wako watayarishe maelezo yenye kufaa kulingana na miaka yao. Wakati fulani, mambo mazito sawa vile magumu ya ndoa ao namna ya kuwa na mwenendo safi inazungumuziwaka wakati ya funzo. Hata vile, kunaweza kuwa fungu moya ao mbili kwenye mutoto anaweza kutoa maelezo. Tena, usaidie watoto wako waelewe juu ya nini kiongozi hatawataya kila mara wakati wananyangula mikono. Kufanya vile, kunaweza kuwasaidia wasikasirike wakati kiongozi anataya wengine. (1 Ti. 6:18) Siye wote tunaweza kutayarisha maelezo yenye itamutukuza Yehova na yenye itajenga Wakristo wenzetu. (Mez. 25:11) Kama tunazungumuzia jambo yenye inatuhusu, tunapaswa kuepuka kusema mambo mingi juu yetu. ( Mez. 27:2; 2 Ko. 10:18) Kuliko kufanya vile, tutakaza akili juu ya Yehova, Neno yake, na watu wake.​—Ufu. 4:11. w23.04 24-25 fu. 17-18

Tuchunguze Maandiko Kila Siku—2025

Siku ya Yenga, 2 Mwezi wa 11

Tusiendelee kulala usingizi kama wengine, lakini tukae macho na kulinda akili zetu.​—1 Te. 5:6.

Upendo ni wa maana ili tukuwe macho na kulinda akili zetu. (Mt. 22:37-39) Kumupenda Mungu kunatusaidia tuhubiri kwa uvumilivu hata kama ile inaweza kufanya tupate magumu. (2 Ti. 1:7, 8) Tunaendelea kuhubiri kwa kutumia telefone na hata barua juu tunapenda pia wale wenye hawamutumikie Yehova. Tunatumainia kama siku moya majirani wetu watabadilika na kuanza kufanya mambo ya muzuri. (Eze. 18:27, 28) Tunapenda pia ndugu na dada zetu. Tunaonyesha ule upendo kwa “kutiana moyo na kujengana.” (1 Te. 5:11) Sawa vile maaskari wenye hawaachanake mu vita, siye pia tunatianaka moyo. Hatuwezi kukwaza ndugu na dada zetu kwa kupenda ao kurudisha ubaya kwa ubaya. (1 Te. 5:13, 15) Tunaonyesha pia kama tuko na upendo kwa kuheshimia ndugu wenye wanasimamia kutaniko.​—1 Te. 5:12. w23.06 10 fu. 6; 11 fu. 10-11

Tuchunguze Maandiko Kila Siku—2025
Karibu
Hii ni chombo ya kukusaidia kutafuta habari mu vichapo vya Mashahidi wa Yehova mu luga mbalimbali.
Kama unapenda kuchukua kichapo fulani, tafazali fungua jw.org.
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine