Siku ya Kwanza, 3 Mwezi wa 11
Wakati [Yehova] anasema jambo fulani, je, hatalifanya?—Hes. 23:19.
Jambo moya yenye inaweza kufanya imani yetu ikuwe nguvu ni kutafakari juu ya bei ya ukombozi. Bei ya ukombozi inatuhakikishia kama ahadi za Mungu zitatimia. Wakati tunafikiria kwa uangalifu sababu yenye ilifanya Yehova atoe bei ya ukombozi na mambo yenye ile iliomba, tutaamini kabisa kama atatimiza ahadi ya kutupatia uzima wa milele mu dunia mupya. Juu ya nini tunasema vile? Bei ya ukombozi iliomba nini? Yehova alituma Mwana wake muzaliwa-pekee, mwenye alipenda sana na mwenye alikuwa rafiki yake wa karibu sana, ili azaliwe hapa ku dunia akiwa mwanadamu mukamilifu. Wakati Yesu alikuwa hapa ku dunia, alivumilia magumu ya kila aina. Kisha, aliteseka na kufa kifo ya maumivu. Yehova alilipa bei kubwa sana! Mungu wetu mwenye upendo hangeacha Mwana wake ateseke na kufa juu tu tukuwe na maisha ya muzuri kwa wakati mufupi sana. (Yoh. 3:16; 1 Pe. 1:18, 19) Juu Yehova alilipa bei kubwa vile, ile inaonyesha kama atatupatia uzima wa milele mu dunia mupya. w23.04 27 fu. 8-9
Siku ya Pili, 4 Mwezi wa 11
Ee Kifo, uko wapi uwezo wako wa kuumiza?—Ho. 13:14.
Yehova anapenda kabisa kufufua wafu? Bila shaka anapenda. Alipatia waandikaji wengi wa Biblia roho yake takatifu ili waandike ahadi yake ya kufufua wafu wakati yenye kuya. (Isa. 26:19; Ufu. 20:11-13) Kila mara, Yehova anatimizaka ahadi zote zenye anatoaka. (Yos. 23:14) Kusema kweli, anapenda kabisa kufufua wafu. Fikiria maneno yenye Yobu alisema. Alikuwa hakika kuwa hata kama anakufa Yehova angetamani kumufufua. (Yob. 14:14, 15, maelezo ya chini.) Yehova hayabadilika. Anatamani kufufua waabudu wake wenye walishakufa. Anapenda sana kuwafufua na kuwapatia afya ya muzuri na maisha yenye furaha. Tuseme nini juu ya mamiliare ya watu wenye hawakupata nafasi ya kujifunza kweli juu ya Yehova mbele wakufe? Yehova Mungu wetu wa upendo anapenda kuwafufua pia. (Mdo. 24:15) Anapenda kuwapatia nafasi ya kuwa marafiki wake na kuishi milele ku dunia.—Yoh. 3:16. w23.04 9 fu. 5-6
Siku ya Tatu, 5 Mwezi wa 11
Kwa musaada wa Mungu tutapata nguvu.—Zb. 108:13.
Namna gani unaweza kutia nguvu tumaini yako? Kwa mufano, kama uko na tumaini ya kuishi milele ku dunia, usome na utafakari maandiko ya Biblia yenye kufasiria namna Paradiso itakuwa. (Isa. 25:8; 32:16-18) Fikiria namna maisha itakuwa mu dunia mupya. Ujiwazie uko pale. Kama tunaendelea kukazia akili tumaini ya dunia mupya yenye tuko nayo, magumu yetu itakuwa “ya wakati kidogo na ya nyepesi.” (2 Ko. 4:17) Yehova atakutia nguvu kupitia tumaini yenye amekupatia. Amekupatia mambo yenye uko nayo lazima ili upate nguvu kutoka kwake, kwa hiyo wakati uko na lazima ya musaada ili kutimiza mugao fulani, kuvumilia magumu, ao kuendelea kuwa na furaha, usali kwa Yehova kwa moyo wote na utafute muongozo wake kupitia funzo ya kipekee. Ukubali vitia moyo vyenye ndugu na dada wanakutolea. Tafakari juu ya tumaini yako ya wakati wenye kuya. Kisha “utafanywa kuwa imara kwa nguvu zote kulingana na uwezo [wa Mungu] wenye utukufu ili uvumilie kwa ukamili kwa subira na furaha.”—Kol. 1: 11. w23.10 17 fu. 19-20