Siku ya Pili, 4 Mwezi wa 11
Ee Kifo, uko wapi uwezo wako wa kuumiza?—Ho. 13:14.
Yehova anapenda kabisa kufufua wafu? Bila shaka anapenda. Alipatia waandikaji wengi wa Biblia roho yake takatifu ili waandike ahadi yake ya kufufua wafu wakati yenye kuya. (Isa. 26:19; Ufu. 20:11-13) Kila mara, Yehova anatimizaka ahadi zote zenye anatoaka. (Yos. 23:14) Kusema kweli, anapenda kabisa kufufua wafu. Fikiria maneno yenye Yobu alisema. Alikuwa hakika kuwa hata kama anakufa Yehova angetamani kumufufua. (Yob. 14:14, 15, maelezo ya chini.) Yehova hayabadilika. Anatamani kufufua waabudu wake wenye walishakufa. Anapenda sana kuwafufua na kuwapatia afya ya muzuri na maisha yenye furaha. Tuseme nini juu ya mamiliare ya watu wenye hawakupata nafasi ya kujifunza kweli juu ya Yehova mbele wakufe? Yehova Mungu wetu wa upendo anapenda kuwafufua pia. (Mdo. 24:15) Anapenda kuwapatia nafasi ya kuwa marafiki wake na kuishi milele ku dunia.—Yoh. 3:16. w23.04 9 fu. 5-6
Siku ya Tatu, 5 Mwezi wa 11
Kwa musaada wa Mungu tutapata nguvu.—Zb. 108:13.
Namna gani unaweza kutia nguvu tumaini yako? Kwa mufano, kama uko na tumaini ya kuishi milele ku dunia, usome na utafakari maandiko ya Biblia yenye kufasiria namna Paradiso itakuwa. (Isa. 25:8; 32:16-18) Fikiria namna maisha itakuwa mu dunia mupya. Ujiwazie uko pale. Kama tunaendelea kukazia akili tumaini ya dunia mupya yenye tuko nayo, magumu yetu itakuwa “ya wakati kidogo na ya nyepesi.” (2 Ko. 4:17) Yehova atakutia nguvu kupitia tumaini yenye amekupatia. Amekupatia mambo yenye uko nayo lazima ili upate nguvu kutoka kwake, kwa hiyo wakati uko na lazima ya musaada ili kutimiza mugao fulani, kuvumilia magumu, ao kuendelea kuwa na furaha, usali kwa Yehova kwa moyo wote na utafute muongozo wake kupitia funzo ya kipekee. Ukubali vitia moyo vyenye ndugu na dada wanakutolea. Tafakari juu ya tumaini yako ya wakati wenye kuya. Kisha “utafanywa kuwa imara kwa nguvu zote kulingana na uwezo [wa Mungu] wenye utukufu ili uvumilie kwa ukamili kwa subira na furaha.”—Kol. 1: 11. w23.10 17 fu. 19-20
Siku ya Ine, 6 Mwezi wa 11
Mushukuru kwa kila jambo.—1 Te. 5:18.
Tuko na sababu mingi za kumushukuru Yehova mu sala. Tunaweza kumushukuru juu ya jambo yoyote ya muzuri yenye tuko nayo. Zaidi ya ile, zawadi yote ya muzuri inatokaka kwake. (Yak. 1:17) Kwa mufano, tunaweza kumushukuru juu ya dunia na juu ya vitu vya muzuri vyenye aliumba. Tunaweza pia kumushukuru juu ya uzima wetu, familia yetu, marafiki wetu, na tumaini yetu. Na tunapenda pia kumushukuru Yehova juu anaturuhusu tukuwe marafiki wake. Inaweza kuwa muzuri kujikaza sana ili kufikiria sababu zenye zinatufanya siye kipekee tumushukuru Yehova. Tunaishi mu dunia yenye watu wengi hawakuwake na shukrani. Mara mingi watu wanahangaikia mambo yenye wanapenda kuliko kuhangaikia mambo yenye wanaweza kufanya ili kuonyesha shukrani juu ya mambo yenye wako nayo. Kama na siye tunaanza kuwa vile, tutakuwa nasali Yehova juu tu ya kumuomba mambo fulani. Juu ya kuepuka ile, tunapaswa kuendelea kumushukuru Yehova juu ya mambo yote yenye anatufanyiaka.—Lu. 6:45. w23.05 4 fu. 8-9