Siku ya Tatu, 5 Mwezi wa 11
Kwa musaada wa Mungu tutapata nguvu.—Zb. 108:13.
Namna gani unaweza kutia nguvu tumaini yako? Kwa mufano, kama uko na tumaini ya kuishi milele ku dunia, usome na utafakari maandiko ya Biblia yenye kufasiria namna Paradiso itakuwa. (Isa. 25:8; 32:16-18) Fikiria namna maisha itakuwa mu dunia mupya. Ujiwazie uko pale. Kama tunaendelea kukazia akili tumaini ya dunia mupya yenye tuko nayo, magumu yetu itakuwa “ya wakati kidogo na ya nyepesi.” (2 Ko. 4:17) Yehova atakutia nguvu kupitia tumaini yenye amekupatia. Amekupatia mambo yenye uko nayo lazima ili upate nguvu kutoka kwake, kwa hiyo wakati uko na lazima ya musaada ili kutimiza mugao fulani, kuvumilia magumu, ao kuendelea kuwa na furaha, usali kwa Yehova kwa moyo wote na utafute muongozo wake kupitia funzo ya kipekee. Ukubali vitia moyo vyenye ndugu na dada wanakutolea. Tafakari juu ya tumaini yako ya wakati wenye kuya. Kisha “utafanywa kuwa imara kwa nguvu zote kulingana na uwezo [wa Mungu] wenye utukufu ili uvumilie kwa ukamili kwa subira na furaha.”—Kol. 1: 11. w23.10 17 fu. 19-20
Siku ya Ine, 6 Mwezi wa 11
Mushukuru kwa kila jambo.—1 Te. 5:18.
Tuko na sababu mingi za kumushukuru Yehova mu sala. Tunaweza kumushukuru juu ya jambo yoyote ya muzuri yenye tuko nayo. Zaidi ya ile, zawadi yote ya muzuri inatokaka kwake. (Yak. 1:17) Kwa mufano, tunaweza kumushukuru juu ya dunia na juu ya vitu vya muzuri vyenye aliumba. Tunaweza pia kumushukuru juu ya uzima wetu, familia yetu, marafiki wetu, na tumaini yetu. Na tunapenda pia kumushukuru Yehova juu anaturuhusu tukuwe marafiki wake. Inaweza kuwa muzuri kujikaza sana ili kufikiria sababu zenye zinatufanya siye kipekee tumushukuru Yehova. Tunaishi mu dunia yenye watu wengi hawakuwake na shukrani. Mara mingi watu wanahangaikia mambo yenye wanapenda kuliko kuhangaikia mambo yenye wanaweza kufanya ili kuonyesha shukrani juu ya mambo yenye wako nayo. Kama na siye tunaanza kuwa vile, tutakuwa nasali Yehova juu tu ya kumuomba mambo fulani. Juu ya kuepuka ile, tunapaswa kuendelea kumushukuru Yehova juu ya mambo yote yenye anatufanyiaka.—Lu. 6:45. w23.05 4 fu. 8-9
Siku ya Tano, 7 Mwezi wa 11
[Endelea] kuomba kwa imani, bila kuwa na mashaka hata kidogo.—Yak. 1:6.
Juu Yehova ni Baba yetu mwenye upendo, hafurahi wakati anatuona tuko nateseka. (Isa. 63:9) Hata vile, haiko mateso yote njo Yehova anazuiaka isitupate, mateso yenye inaweza kulinganishwa na mito ao moto. (Isa. 43:2) Lakini, anatuahidi kama atatusaidia “kupita” mu ile mateso. Na hataruhusu ile mateso iharibu uhusiano wetu pamoya naye. Yehova anatupatia pia roho yake takatifu yenye nguvu ili kutusaidia kuvumilia. (Lu. 11:13; Flp. 4:13) Kwa hiyo, tunaweza kuwa hakika kama sikuzote tutakuwa na yote yenye tuko nayo lazima ili tuendelee kuvumilia na kuendelea kuwa waaminifu kwa Yehova. Yehova anatazamia tumutumainie. (Ebr. 11:6) Wakati fulani tunaweza kuona kama magumu yetu ni ya nguvu sana, yenye hatuwezi kuvumilia. Tunaweza kuanza kujiuliza ikiwa Yehova atatusaidia kabisa. Lakini Biblia inatuhakikishia kama kupitia nguvu ya Mungu tunaweza “kupanda ukuta.” (Zb. 18:29) Kwa hiyo, kuliko kuwa na mashaka tunapaswa kusali kwa imani kabisa na kuwa hakika kabisa kama Yehova atajibia sala zetu.—Yak. 1:6, 7. w23.11 22 fu. 8-9