Siku ya Tatu, 30 Mwezi wa 7
Hatuwezi kuacha kusema juu ya mambo yenye tumeona na kusikia.—Mdo. 4:20.
Tunaweza pia kuiga wanafunzi wa Yesu kwa kuendelea kuhubiri hata kama wenye mamlaka wanatukataza kufanya vile.Tuko hakika kama Yehova atatusaidia kutimiza utumishi wetu. Kwa hiyo, umuombe Yehova uhodari na hekima na akusaidie ili uvumilie magumu. Wengi kati yetu wako napambana na magumu ya kimwili ao ya kihisia, magumu ya kupoteza mupendwa wao, magumu fulani mu familia, mateso, ao magumu ingine. Na mambo sawa vile, magonjwa ya kuambukiza na vita imefanya ikuwe nguvu kuvumilia magumu mingi kati ya ile. Umufungulie Yehova moyo wako. Umuambie hali yako sawa vile tu unaweza kumuambia rafiki yako wa karibu sana. Ukuwe hakika kama Yehova “atatenda kwa ajili yako. (Zb. 37:3, 5) Kuendelea kusali kutakusaidia “uvumilie chini ya taabu.” (Ro. 12:12) Yehova anajua mambo yenye watumishi wake wako napambana nayo. “Anasikia kilio chao cha kuomba musaada.”—Zb. 145:18, 19. w23.05 5-6 fu. 12-15
Siku ya Ine, 31 Mwezi wa 7
Muendelee kuhakikisha ni nini yenye kukubaliwa kwa Bwana.—Efe. 5:10.
Wakati tunataka kukamata maamuzi ya maana, ni muzuri tutafute kujua “mapenzi ya Yehova” na kisha tutende kulingana nayo. (Efe. 5: 17) Wakati tunapata kanuni ya Biblia yenye inahusu hali yetu, ni sawa vile tuko natafuta mawazo ya Yehova kuhusu ile jambo. Na wakati tunatumikisha ile kanuni, tutaweza kukamata maamuzi ya muzuri. “Ule muovu,” adui yetu Shetani, anapenda tutumie wakati wetu wote ili kufuatilia mambo ya huu ulimwengu na tukose wakati wa kumutumikia Mungu. (1 Yo. 5:19) Inaweza kuwa mwepesi kwa Mukristo kutia pa nafasi ya kwanza vitu vya kimwili, elimu ya huu ulimwengu, ao kazi kuliko kutia utumishi wake kwa Yehova pa nafasi ya kwanza. Kama ile inatokea, inaweza kuonyesha kama ule Mukristo iko nachochewa na mawazo ya ulimwengu. Kusema kweli, ile mambo haiko ya mubaya, lakini haipaswe kuwa pa nafasi ya kwanza mu maisha yetu. w24.03 24 fu. 16-17
Siku ya Tano, 1 Mwezi wa 8
Magumu ya mwenye haki ni mengi, lakini Yehova anamuokoa katika magumu hayo yote.—Zb. 34:19.
Ona mambo mbili ya maana yenye kupatikana mu ile zaburi: (1) Mwenye haki anapataka magumu. (2) Yehova anatuokoaka wakati tunapata magumu. Yehova anafanyaka nini ili kutuokoa? Anatusaidiaka tukuwe na mutazamo wenye kufaa juu ya maisha. Yehova anatutolea ahadi ya kama tutakuwa na maisha yenye furaha wakati tuko namutumikia, lakini ile haimaanishe kama hatutapata magumu leo. (Isa. 66:14) Anatuambia tukaze akili yetu juu ya wakati yenye kuya, ni kusema, wakati yenye tutakuwa na maisha yenye anapenda tufurahie milele. (2 Ko. 4:16-18) Kwa sasa, iko natusaidia ili tuendelee kumutumikia kila siku. (Omb. 3:22-24) Mifano ya waabudu waaminifu wa Yehova wa zamani na wa leo inaweza kutufundisha nini? Tunaweza kupata magumu fulani yenye haitazamiwe. Lakini kama tunamutegemea Yehova, bila shaka, ataendelea kutusaidia.—Zb. 55:22. w23.04 14-15 fu. 3-4